CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Monday, January 25, 2010

NAMNA YA KUTENGENEZA CHAPATI



Unga kilo moja weka sukari kijiko kimoja cha chai pamoja na chumvi kijiko kimoja cha chai




weka mafuta ya kupikia yamoto kikombe kimoja cha chai kidogo kisha changanya




Kisha weka maji ya uvugu vugu kikombe kimoja cha chai kidogo na endelea kuchanganya















Kanda mpaka upate mchanganyiko mzuri laini na mkavu



Kata saizi ya unga ambao ukisukuma itatosha kwenye kikaango chako



huu ni muonekano wa chapati ndogo itakayoweza kuenea katika kikaango kidogo hata kwa matumizi ya nyumbani iweke kwenye kikaango cha moto  bila mafuta pika pande zote mbili



kisha weka mafuta naigeuze geuze





hii ni chapati yako imekamilika na ni laini na ina lea kama daftari na ni tamu kupita maelezo


NAMNA YA KUTENGENEZA MAANDAZI



Chukua Amira ya chenga gram 11




Chumvi nusu kijiko kidogo cha chai



Sukari gram 250



Unga wa ngano kilo moja


Maji ya uvugu vugu nusu lita




Mafuta ya kupikia lita 2 na nusu


Weka pakiti ndogo ya amira yenye ujazo wa gramu 11 yoote kwenye unga wako wa kilo moja





Kisha weka chumvi nusu kijiko kidogo cha chai chumvi hii husaidia kupunguza mafuta ndai yaa andazi baada ya kuiva andazi lako litakua halina mafuta safi na salama kwa mlaji


Weka sukari gram 250 katika unga wako



Baada ya hapo weka mafuta ya moto ujazo wa kikombe kidogo cha chai au gr 250
 changanya vizuri mafuta bado yakiwa yamoto




Kisha weka maji ya uvuguvugu ili kuuwa ngano nakufanya amira kuweza kumuka haraka





Kanda mchanganyiko wako safi kwa kutumia nguvu na umakini mpaka mchanganyiko wako uwe laini



Mchangyanyiko wako kama uko bado ni teketeke na ulizidisha maji kidogo weka unga kiasi kisha endelea kukanda mpakja uwe mkavu na laini


Hapa safi sasa



 Shepu vizuri tayari kwa maandalizi ya kusukuma na kukata






Sukuma unga wako mpaka saizi ya unmene halisi wa andazi lako utakavyopenda liwe


Kisha tumia kitu chechote kile kukatia kwa umbo lolote lile utakalo lipenda





Yaache kwa muda wa dakika 10 baada ya kuyakata yaumuke kisha itakua tayari kwa kuyachoma



Baada ya kukata maumbo mazuri ya duara unga unaobakia unaweza viringisha maumbo tofauti kama uonavyo katika picha pia unaweza tengeneza hata herufi


 Pasaha mafuta yako katika moto wa wastani yasiwe na moto mkali utapelekea maandazi yako kuungua kisha yaweke katika moto na geuza kila mara ili yasivimbe upande mmoja na ikawa vigumu kuyageuza






Hili ni anfazi lako safi limeshaiva na halina mafuta ndani na safi kabisa


Tuesday, January 19, 2010

NAMNA YA KUCHONGA NDEGE KWA KUTUMIA TUNDA AINA YA APPLE

Hapo chini ni seti ya aina ya vifaa vinavyotumika kuchongea mboga na matunda katika mitindo tofauti






Hapo chini ni vifaa pekee tulivyotumia katika kuchongea tunda letu hili aina ya apple fatilia picha vizuri utaona jinsi ya kuchonga mpaka mwisho anatokea ndege mzuri aina ya bata mzinga kama utakua na swali lolote uliza.


































































Ndugu wapenzi wa blog yetu ya mafunzo ya chakula kama nilivyoahidi kuhusu kufundisha mapishi na sanaa ya marembo ya mboga na matunda sasa tunaendelea na mafunzo naimani wengi mtafurahia utaalamu huu pia maoni yenu ndio yananipa mwanga nijue hasa kama mnaelewa na mnafatilia. Mafunzo yanayofuata ni utengenezaji wa maandazi safi na salam pamoja na chapati wapenzi wa vyakula hivyo kaeni tayari kupata utaalamu