CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Wednesday, June 5, 2013

JIFUNZE KUPIKA SAMAKI KATIKA OVEN KWA KUTUMIA FOIL

 
NI RAHISI, NAFUU NA HARAKA SANA KUANDAA AINA HII YA MAPISHI YA SAMAKI KWA KUTUMIA FOIL NA KUOKA KATIKA OVEN LAKINI SAMAKI ATATOKA KAMA AMECHEMSHWA NA AKIWA NA LADHA SAFI SANA BILA YA KUPOTEZA VIRUTUBISHO VYOTE MUHIMU.
 
MAHITAJI
1pc kitunguu maji kikubwa
1 pc limao kubwa
5 gram binzali
5 gram chumvi
5 gram pili pili manga
1 pc pili pili hoho kubwa
50 gram tomato pest ( nyanya ya kopo)
kipande cha foil kutokana na ukubwa wa samaki
 
JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI
 
 
Huu ni muonekano wa samaki akiwa mbichi tayari umeshamsafisha vizuri kwa maji baridi na mapishi haya unaweza tumia kwa samaki aina ya sato, sangara, kibua, change, jodari au kole kole na akaiva na ladha safi kabisa.

 
Katika picha unaona mchanganyiko wa vitunguu, pilipili hoho, maji ya limao, binzali, chumvi, pili pili manga na nyanya ya kopo baada ya kuchanganya pamoja kasha mpakae samaki pande zote mbili ulizompasua ili mchanganyiko huu uingie vizuri katika nyama kasha mabaki ya huo mchanganyiko mjazie tumboni kisha mfunike vizuri na foil muweke katika oven tayari ikiwa na moto.
 
Jana mchana niliporudi nyumbani niliandalia samaki aina ya sato pamoja na maharage ya Nazi na ugali wa mahindi nipo ulaya lakini na kula chakula nilichokizoea nyumbani Tanzania na kwa ladha na ubora ule ule.
 
 
 
Unaweza kumpika katika oven kwa dakika 30 kwenye moto wa degree 200 hadi 250 pia kwa mtindo huu unaweza kumchoma katika jiko la mkaa akiwa hivi hivi katika foil na akaiva safi kabisa
 
 
 
Baada ya nusu saa samaki wako atakua ameiva na atakua na muonekano kama huu na ladha safi sana
 

 
Hapa sasa ndio nilikua namfunua vizuri tayari kwa chakula cha mchana

 
Hata kama samaki amekaa kwenye friza kwa muda mrefu mchanganyiko huu wa mboga majani limao na viuongo vinasaidia sana kuamsha ladha ya samaki wako pika familia ifurahie.
 
KESHO YATAENDELEA MAFUNZO YA KUPIKA SAMAKI KWA MITINDO MINGINE


Wednesday, May 22, 2013

MUDA SI MREFU NITAWEKA MAFUMNZO MBALI MBALI YA JINSI YA KUPIKA SAMAKI MAARUFU SANA AINA YA CHANGU

 
KAA TAYARI KWA MAFUNZO YA KUPIKA SAMAKI MAARUFU SANA AINA YA CHANGU KWA KUTUMIA MBINU MBALI MBALI ZAIDI YA 10 NA UTAALAMU WA KUMPAMBA KATIKA SAHANI AWEZE KUVUTIA WALAJI
 
 
 
Samaki changu mbichi akiwa ameshasafishwa safi kabisa
 

 
Samaki changu wa kuchoma kwa kutumia foil

 
Jinsi ya kuachanisha kati ya mifupa na nyama ya samaki changu

 
Jinsi ya kumchoma samaki changu katika jiko la mkaa

 
Jinsi ya kumuoka samaki changu katika ovena
 
 


Thursday, May 16, 2013

JIFUNZE KUPUNGUZA UZITO MKUBWA AU KULINDA UZITO WA KATI ULIONAO KWASASA

 
SOMA KWA UFASAA NA FATILIA KWA MAKINI MAELEZO HAPO CHINI JINSI VIMIMINIKA VINAVYOWEZA KUKUSAIDIA KUPUNGUZA UZITO MKUBWA NA KUA NA UZITO WA KAWAIDA HASA HASA KITAMBI IWE MWANAMKE AU MWAUME KITAPOTEA KABISA.

 KAMA UNAUZITO WA KAWAIDA ITAKUSAIDIA KUTO KUONGEZEKA NA KULINDA UZITO WAKO KWA AFYA NJEMA.

Fatilia kwa makini maelezo hayo hapo chini yatakusaidia sana.
.
1-
Asali inasaidia sana katika kupunguza uzito, Chukua asali 10 grams kisha tia katika maji safi ya vugu vugu yasiwe ya moto kisha kunywa kikombe kimoja kila siku mchana saa 6 na 12 jioni. Hii ni njia bora sanaya kukufanya wewe upunguze uzito bila ya kusababisha madhara katika mwili wao.
·          
2 - Unapokunywa chai ya asubuhi kumbuka kula vipande vya nyanya mbichi unaweza kuziweka katika mkate kama sandwich au unaweza kula tu zenyewe pamoja na mayai au chapati
·          
3  - Hii ndio iwe chai yako ya asubuhi, weka maji moto katika kikombe kisha ongezea vijiko 3 vya limao, pili pili manga 3 gram au chota kwa kwa vidole kidogo sana kwa ladha tu ili iwe kali pamoja na asali kijiko kimoja cha chai changanya vizuri kisha kunywa kila siku asubuhi.
·          
 4 - Kama una matatizo ya gesi tumboni au vidonda vya tumbo usitumie njia hiyo hapo juu namba 3 kwani maji ya limao na pili pili manga zitakuumiza unaweza kunywa chai ain ya (green tea). Inauzwa kila kona  katika maduka ya vyakula na ni nafuu itafanya kazi vizuri tu. 
·          
5 - Baada ya chakula cha jioni kuanzaia saa 2 hadi saa 3 usiku unaweza kunywa juisi nzito yenye mchanganyiko wa papai na karoti hakikisha hutii maji kabisa kwani papai lina maji ya kutosha. Juisi hii kunywa glasi moja kubwa baada ya mlo wa jioni itakusaidia sana kumeng'enya chakula tumboni na wakati wa usiku nakutoa ruksa kwa chai na jusi utakazokunywa kuanzia asubuhi mchana na jioni zifanye kazi.
Tiba Mbadala yakutumia vimiminika bila kujinyima kula fanya hivi kwa miezi 3 mpaka 4 utaona matunda yake. Ilinde familia yako kwa gharama nafuu sana.
 

Friday, May 10, 2013

JIFUNZE KUPANGA RATIBA YA MLO WA NYUMBANI KWA WIKI NZIMA

 
BAADA YA MAOMBI YA WANAFAMILIA WENGI WA KITANZANIA SASA NIMEAMUA KUFANYIA KAZI PIA RATIBA YA CHAKULA YA WIKI NZIMA KWA FAMILIA KUANZIA CHAI ASUBUHI, CHAKULA CHA MCHANA NA CHAKULA CHA JIONI.
 
KITABU KITAZINGATIA SANA MBINU ZA MAPISHI BORA KWA GAHARAMA NA FUU NA LADHA SAFI KWA CHAKUAL KITAKACHOKUA NA FAIDA NA MWILI WAKO.
 
PIA NITATENGENEZA NA DVD ITAKAYOKUA INAELEKEZA MAFUNZO YOTE YALIYOKUWEPO KWENYE KITABU HIKI. KITAKAPOKUA TAYARI NITAWAFAHAMISHA KUPITI UKURASA WA FACEBOOK.COM Active Chef NA www.activechef.blogspot.com
 
 
TUOMBEANE UZIMA, AFYA NA MAISHA MAREFU AMIIN ILI KILA ZURI NILILOJAALIWA TUWEZE KUGAWANA KWA NJIA MOJA AU NYINGINE AMIIN
 
 


JIFUNZE KUANDAA CHAKULA BORA NA SALAMA KWAJILI YA MWANAO

 
HABARI NJEMA WAPENZI WA BLOG www.activechef.blogspot.com MAMA YANGU MZAZI NI MTAALAMU WA CHAKULA NA LISHE NAMI NI MTAALAMU WA KUPIKA CHAKULA BORA NA SALAMA.
 
TUNASHIRIKIANA KUANDAA KITABU KITAKACHOKUA NA RATIBA YA WIKI NZIMA YA CHAKULA CHA WATOTO WA UMRI TOFAUTI, MAELEZO JINSI YA KUKIANDAA CHAKULA NA MAELEZO YA FAIDA YA CHAKULA HICHO KATIKA MWILI WA MTOTO KWA LUGHA YA KISWAHILI FASAHA NA VYAKULA VINAVYOPATIKANA POPOTE KWA URAHISI.
 
KITABU KITAKAPOKUA KIMECHAPISHWA TAYARI NITAWAFAHAMISHA WAPI VINAUZA NA KIASI GANI BADO TUPO KATIKA MAANDALIZI KWA HABARI ZAIDI USIACHE KUJIUNGA KATIKA UKURASA WETU WA FACEBOOK KWA HABARI ZAIDI NI facebook.com Active Chef
 
 
 
 
 

Wednesday, May 8, 2013

HABARI NJEMA ZITAWADIA MUDA SI MREFU LEO HII

 
 
HABARI WAPENZI WA BLOG HII YA CHAKULA BORA NA SALAMA NIMEKUA KIMYA KWA MUDA KUTOKANA NA MAJUKUMU YA KIMAENDELEO LEO
 
 
NIMERUDI TENA NDUGU ZANGU NA HABARI NJEMA KWENU KWANZA ANGALIA CHAKULA HIKI KISHA NIAMBIE UMEGUNDUA NINI?
 
 
KAZI KUBWA NI YA UTAFITI WA CHAKULA, MIMI NA WENZANGU TUNAFANYA UTAFITI WAKUCHANGANYA UTAALAMU WA UPISHI WA MATAIFA YA SCANDINAVIA NA AFRIKA NA KUONA WALAJI WATAIPOKEAJE BAADA YA HAPO TUTAANDAA KITABU CHA MCHANYIKO HUO WA TAALUMA SIPATI PICHA NITAKAVYOWALISHA WAZUNGU UGALI, KISAMVU, MLENDA NA MAKANDE HAHAHAAAAA
 
 
HALI YA HEWA NI NZURI SANA HAPA KISIWANI
 
 
SAFARI YANGU YA KUELEKEA KISIWANI ILIANZIA HAPA NIKAPANDA BOAT NA KUELEKEA KISIWANI KWAJILI YA KUANZA KAZI
 


Friday, April 12, 2013

JIFUNZE KUPIKA KITAFUNWA HIKI CHA MAHARAGE YA SAOYA PIA UNAWEZA KULA KAMA MBOGA

 
KAA TAYARI KWA RECIPE SAFI KABISA YA KITAFUNWA HIKI CHA MAHARAGE YA SAOYA PIA UNAWEZA KULA KAMA MBOGA WEEKEND HII NI TAMU RAHISI NA NI NAFUU KUANDAA

MAHITAJI

JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI














 
 
 
Picha na maelezo yanakuja muda si mrefu


JIFUNZE KEKI YENYE MCHANGANYIKO WA KARANGA SUKARI YA KAHAWIA NA KAHAWA YA UNGA

 
 
HEHEHEEEEEEEEEEEEE UNAKUMBUKA ENZI ZA PIPI TOFFIIIII?? KAA TAYARI KWA RECIPE SAFI KABISA YA KEKI YENYE MCHANGANYIKO WA KARANGA SUKARI YA KAHAWIA NA KAHAWA YA UNGA WEEKEND HII NI TAMU RAHISI NA NI NAFUU KUANDAA

MAHITAJI

JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI













 
 
 
maelezo yanafatia muda si mrefu


JIFUNZE KUPIKA YA MUFFIN YENYE MCHANGANYIKO WA VIPANDE VYA CHOCOLATE NA KARANGA

 
RECIPE SAFI KABISA YA MUFFIN YENYE MCHANGANYIKO WA VIPANDE VYA CHOCOLATE NA KARANGA NI TAMU RAHISI NA NI NAFUU KUANDAA

MAHITAJI

250 gram siagi laini
250 sukari
2 mayai
250 gram plain yogurt
1 kijiko kidogo cha chai vanilla
500 gram  unga wa ngano
1 kijiko kidogo cha chai baking soda
1/2 kijiko kidogo cha chai baking powder
1/2 kijiko kidogo cha chai chumvi
180 gram vipande vya chocolate
1 kijiko kidogo cha chai cinnamon powder
4 kijiko kikubwa cha chakula karanga za kuoka
2 kijiko kikubwa cha chakula sukari ya brown
60  gram vipande vya chocolate

JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI
 
Muda wa maandalizi : Dakika 30
Muda wa mapishi : Dakika 30
Idadi ya keki : 12 Muffins
 

Katika bakuli changanya sukari na siagi pamoja.

 
Kisha mimina mayai pole pole endelea kuchanganya katika mchanganyiko wa sukari na siagi.

 
Kisha ongeza yogurt na vanilla na uchanganye ichanganyike vizuri.

 
Kisha chukua bakuli safi na uchanganye unga wa ngano pamoja na baking soda, baking powder na chumvi.

 
Kisha chukua mchanganyiko wa unga kisha mimina polepole katika mchanganyiko wa mayai.

 
Kisha mimina vipande vya chocolate na uendelee kuchanganya polepole.

 
KIsha chukua tray ya kuokea na weka vikombe vya karatai kisha mimina mchanganyiko wako 2/3 hakikisha isijae kabisa.

 
Kisha chukua bakuli kavu weka vipande vya chocolate vilivyobakia, cinnamon powder na karanga changanya pamoja.

 
Kisha mwagia kwa juu mchanganyiko huo kwenye tray ya kuokea izibe ile nafasi iliyobakia.

 
Hakikisha oven unaiwasha dakika 5 kabla ya kuoka Choma katika ovena katika moto wa 350F kwadakika 20 had 30. Poza keki zako kwa dakika 5 kabla ya kuzitoa katika pan.

 
Naimani ukizieweka sehemu nzuri ukafunika safi zisiguswe na wadudu zinaweza kukaa kwa siku tatu bila ya kuharibika!

 
 WAANDALIE FAMILIA AU WATEJA WAKO WAFURAHIE.