CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Monday, August 23, 2010

SPAGHETTI WITH MUSHROOM SAUCE

Tambi na mchuzi wa uyoga recipe hii safi sana pia kwa wanaofunga kwasasa unaweza badilisha mapishi ya tambi zako kwa mapishi haya

MAHITAJI

1 paketi ya Tambi
200 gram uyoga
1 kitunguu maji
50 gram pili pili hoho
20 gram kitunguu swaumu
100 gram fresh cream
50 gram maziwa ya maji
50 gram parmesan cheese
5 gram kungu manga ya unga
1 nyanya
1 jani la basil
1 kijiko kikubwa cha chakula mafuta ya olive
5 gram chumvi
5 gram pili pili manga

JINSI YA KUANDAA

Chemsha tambi zako ziive vizuri kumbuka zisiive sana kisha ziweke pembeni zipoe

Kata kata mchanganyiko wa kitunguu maji, uyoga, pili pili hoho kisha weka katika sufuria yenye mafuta ya oilive yamoto kaanga kiasi kisha weka kitunguu swaumu.

kisha weka maziwa ya maji pamoja na fresh cream changanya kwa kadika1 tu ikishapata moto weka tambizako pamoja na parmesana cheese koroga mapaka ichanganyike safi kabisa kisha weka chumvi na pili pili manga pamoja na kungu manga ya unga itakua imeva safi kabisa tayari kwa kuliwa.

kwenye sahani pamba na kipande cha nyanya na jani la basili pembeni unaweka cheese kiasi ukizingatia cheese inapendeza sana kuliwa na tambi.



Huu ni muonekano wa Tambi ya uyoga ni tamu sana inafaa kwa futari na ni rahisi sana kuandaa hasa kwa wafanyakazi au wafanya biashara unarudi nyumbani umechoka chakula hiki ni rahisi sana kuandaa. Unaweza chemsha tambi nyingi na ukahifadhi kwenye friji ukawa unapika kidogo kidogo kwa mitindo tofauti.

ENJOY!!


No comments: