CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Sunday, December 5, 2010

JIFUNZE KUTENGENEZA TAMBI KWA MTINDO WA KIMOROKO


TAMBI HIZI NI MAARUFU SANA NCHINI MOROKO, NI RAHISI KUANDAA NA NI
TAMU SANA KWA LADHA KAA TAYARI KWA RECIPE SAFI KABISA


MAHITAJI

2 paketi za spaghetti 
60 gram olive oil 
1kitunguu maji kikubwa, chop chop
5 gram kitunguu swaumu
240 gram nyanya ndogo ndogo kata nusu
1 kijko cha chai unga wa coriander
1 kijiko kidogo cha chai unga wa cumin
1/2 kijiko kidogo cha chai unga wa turmeric 
240 gram za chickpeas (Kumbuka kuhifadhi maji utakayochemshia) 
1 kijiko kikubwa cha chakula tomato paste 
6 au 7 mbegu za green olives(sio lazima) 
1 fungu la majani ya giligilani na majani ya mint kwajili ya kupambia
60 gram  korosho au karanga
5 gram chumvi

    JINSI YA KUPIKA FATILIA PICHA NA MAELEKEZO HAPO CHINI




    Chemsha chickpeas ziive kabisa ziwe laini kisha chuja maji na . Zichemshe spaghetti fuata maelekezo katika paketi yake. Kisha kaanga vitunguu katika mafuta pamoja na kitunguu swaumu mpaka vilainike.



    Ongezea zile nyanya ndogo ndogo ulizokata nusu, tomato paste pamoja na viungo vyote kaanga mpaka upate harufu nzuri ya mchanganyiko wako kuiva na kua rojo rojo .



    Kisha ongezea chickpeas na kaanga kwa dakika 2 au 3



    KIsha weka spaghetti zilizochemshwa, olive oil, olives na korosho kisha endelea kukoroga pole pole.



    Kisha juu yake pamba kwa kutumia majani ya gili gilani na mint. Majani haya yanaongeza harufu safi na ladha nzuri sana, korosho au karanga zinakupa crunch safi sana.




    FURAHIA MLO HUU RAHISI MTAMU NA SAFI SANA KWA AFYA YA MLAJI



    No comments: