CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Tuesday, June 21, 2011

WAPENZI WA KINYWAJI KIZITO AU SMOOTHIE


 MAHITAJI

1 ndizi mbivu kubwa, chop chop
1 apple jekundu toa kokwa la kati kisha kata kata vipande vidogo iwe baridi
200 gram vipande vya embe dodo ilioiva vizuri iwe baridi
400 gram  frozen strawberries
240 gram juice ya chungwa ya baridi
120 gram mtindi (yogurt) baridi



JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAFUNZO HAPO CHINI

 Muda wa kuandaa: Dakika 15
Muda wa kupika: Dakika 15
Idadi ya walaji: Watu wawili 

Chukua mchanganyiko wako wa matunda yote weka katika blender au smoothie maker. Blend
vizuri kisha mimina kwenye glasi tarayi kwa kunywa


 


Hii ni smoothie safi sana ikiwa na nutrition ya kutosha. Ingawa ina fiber nyingi sana, vitamin C, potassium na antioxidants. Mtindi (yogurt inachangia acidophilus)


                                                                                                                                                                 



MAHITAJI

1 Avocado (menya kisha chop chop)

1 pear (menya kisha chop chop)
1/2 ndizi mbivu (chop chop)
120 gram mtindi halisi (plain yogurt)
1 asali kijiko kikubwa cha chakula




JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI

Muda wa maandalizi: Dakika 15
Muda wa mapishi: Dakika 15
Idadi ya walaji: watu 2

Katika blender weka mchanganyiko wa matunda yote kisha saga na weka katika friji ipoe kisha mpatie mlaji



Pia kuongeza ladha zaidi unaweza weka juisi ya limao.

Ni bora san wka afya na ina vitamin C kwa wingi, folic acid, flavanoids na potassium. Ni tamu sana na inafaa kwa mtu wa umri wowote ule. 


No comments: