CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Monday, January 9, 2012

JIFUNZE KUTENGENEZA CHAKULA HIKI CHA MCHANGANYIKO WA MABOGA, KAROTI, KITUNGUU NA PANEEL CHEESE


 RECIPE HII SAFI KABISA YA CHAKULA HIKI CHA MCHANGANYIKO WA MBOGA

MAHITAJI

120 gram mbegu za alizeti au unaweza tumia mbegu za ufuta

1 Boga dogo, menya, toa mbegu na katakata vipande
1 kitunguu kikubwa, chop chop
5 gram kitunguu swaumu
1 carrot kubwa, kata kata vipande vya ukubwa kama kwenye picha
240 gram paneel cheese au unaweza tumia ( mushrooms , uyoga )
1 kijiko kikubwa cha chakula korosho za kuoka, chop chop
1 fungu la corriender na parsley kwajili ya kupambia
5 gram chumvi
5 gram pili pili manga



JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI

Muda wa maandalizi : Dakika 30

Muda wa kupika : 30 dakika mpaka saa 1
Idadi ya walaji :  Watu 2



Weka maboga katika baking pan, nyunizia kiasi mafuta pamoja na pili pili manga. 



Roast katika oven kwa moto wa 400F kwa muda wa dakika 20 hadi 30 hakikisha inaiva na ukibonyeza inabonyezeka yaani laini wastani.


Kisha weka mafuta katika kikaango na kikishapata moto weka kitunguu, karoti na paneel cheese pampoja na chumvi na kitunguu swaumu endelea kukaanga.

 

Kisha weka maboga yaliookwa kwenye oven pamoja na mbegu za ufuta au mbegu za alizeti pia unaweza tumia hata mbegu za maboga endelea kukaanga na onja kama chumvi au pili pli manga haitoshi ongezea kiasi.


Kisha mwagia kwa juu majani ya korrienda na parsley kuongeza ladha na kuongeza rangi katika muonekano wa chakula chako.

 

Chakula hiki ni safi sana kwa afya ya mlaji kwani hakina mafuta kabisa pia ni tajiri sana kwa nutrition, Kumbuka kumwagia kwajuu zile korosho za kuokwa kwa juu kabla ya kumpatia mlaji.


Chakula hiki unaweza kula kama kilivyo au ukaongeza nyama, samaki au chapati au mkate pia na ukafurahia mlo huu wewe na familia yako.

 



NI RAHISI SANA KUANDAA NA HAKINA GHARAMA KABISA WAANDALIE FAMILIA YAKO CHAKULA BORA WAFURAHI.



 

1 comment:

Unknown said...

This is wow! napenda kuisoma blog yako na huwa najaribu kupika kwa kufuata maelekezo yako.
Nafikiria kupika hiki chakula hivi karibuni.I hope kitakuwa chakula kizuri.