CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Monday, November 4, 2013

JIFUNZE KUTENGENEZA MTINDI FRESH AU YOGURT

RECIPE SAFI KABISA YA KUTENGENEZA MTINDI FRESH UKIWA NYUMBANI AU HOTELINI KWA URAISHI SALAMA NA HARAKA ZAIDI
MAHITAJI
1 lita ya maziwa mabichi
100 gram mtindi uwe fresh au wa kopo
 
MAMBO YA MSINGI YA KUZINGATIA
Aina ya maziwa.  Aina hizi za maziwa unaweza tumia Goat Milk, Full fat milk, Pasteurized Milk, Homogenized Milk, Raw Milk, 2% Milk, 1% Milk, Fat free] kumbuka aina ya maziwa utakayotumia na matokeo yake yatakuwa tofauti maziwa yakiwa na mafuta kiasi ndio na mtindi wako utakua mzito
 
Thermometer ni lazima?: Sio lazima kabisa kwani bibizetu sikumbuki kama walikua wanatumia kumbuka maziwa hayatakiwi kuwa yamoto yanatakiwa kuwa yavugu vugu weka kwenye kiganja kupima kama tayari yanauvugu vugu kabla ya kuweka mtindi fresh.

Mtindi wangu haujawa bado ni maziwa tatizo nini?  sababi ya kwanza unaweza ukawa umetumia maziwa ya  UHT (Ultra High Temperature) processed milk. ingawa pia unaweza kutengenezea yogurt ikiwa utafata vipimo na maelezo vizuri,  Sabau ya pili unaweza ukawa umetumia mtindi ulioharibika katika kuchanganyia na sababu ya tatu ni kutochemka kwa maziwa kwa joto la 105-110 F temperature au umechanganya mtindi kwenye maziwi yamoto sana au yabaridi sana.
 
JINISI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI
Muda wa maandalizi : Masaa 4 hadi 8
Muda wa mapishi : Dakika 15
Idadi ya walaji : Watu 4


Chemsgha maziwa mabichi kwa nyuzi joto 110F. Ukiyachemsha mziwa katika joto la 110F, bado maziwa yanakua katika ladha ya uhalisia ya ubichi.

Note: sio lazima kutumia maziwa mabichi kwa recipe hii


Note: kama utataumia maziwa ambayo yameshachemshwa basi kumbuka kuyapoza mpaka joto lifikie 110F before the next step.


Nilibakisha yogurt kiasi ndio naitumia tena kama huna unaweza nunu mtindi fresh na ukatumia katika hatua inayofuata baada ya kuchemsha maziwa.

Kisha mwagia mtindi huo ndani ya maziwa .

Stir and whisk it so that it dissolves and is well distributed  throughout.

Funika na mfuniko hakikisha kua joto lilikua ni 105F to 110F . Ili iweze kuganda na kuset haraka unatakiwa uwashe oven kwa dakika mbili kasha Zima halafu weka sufuria yako itachukua masaa 3 hadi 5 kuganda na kuset,kwasehemu zenye joto kama Tanga , Dar es salaam, Zanzibar na mtwara unaweza weka tu pembei ya jiko na baada ya masa 5 ikawa imeganda vizuri kabisa sababu ya hali ya hewa na mgandamizo wa hewa wa juu.
 
See that set yogurt with a yellow layer on top?.

Kwasababu maziwa tuliotumia ni fresh basi cream inakuja juu na nzito kabisa.

 Ukitaka mtindi wako uwe mzito basi chukua kitambaa na chuza maji kisha itabakia cream nzito nasfi kabisa.


Weka katika bakuli na unaweza kuongezea ladha za matunda mfano embe, chungwa, nanasi au ndizi familia au wateja wako wakafurahia sana.
 

No comments: