CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Tuesday, July 1, 2014

JIFUNZE KUTENGENEZA PIZZA KEKI


MUDA SI MREFU KAA TAYARI JIFUNZE KUTENGENEZA  PIZZA KEKI
 
MAHITAJI

  •  480 gram unga wa ngano
  • 2 sukari kijiko kikubwa cha chakula
  • 1 kijiko kikubwa cha chakula Baking Powder
  • 1 kijiko kidogo cha chai Dried Basil
  • 1 kijiko kidogo cha chai chumvi
  • 1/2 kijiko kidogo cha chai Baking Soda
  • 240 gram Cheddar cheese kata cubes
  •  180 gram mtindi halisi
  •  60 gram maziwa ya maji
  • 4 ute mweupe wa yai
  •  60 gram siagi iliyoyeyushwa
  • 120 gram mchanganyiko wa kitunguu, pilipili hoho, nyanya na bilinganya chop chop
  • 60 gram Pizza Sauce
  • 120 Mozzarella cheese iliyokwaruzwa
  •  
    JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI
     
     
    Washa moto wa oven nyuzi joto (200 C). Chukua bakuli kubwa safi na kavu kasha changanya unga wa ngano, sukari, baking powder, salt, basil and baking soda

     
    Changanya vizuri ichanganyike kasha tupia katika mchanganyiko wako vipande vya cheddar cheese.

     
    Chukua bakuli jingne na weka mtindi, ute mweupe wa yai na siagi piga piga mpaka ichanganyike vizuri.

     
    Chukua mchanganyiko wa mtindi na mayai kisha mwagia kwenye mchanganyiko wenye unga wa ngano.

     
    Hakikisha una changanya vizuri pole pole ichanganyike vizuri. Don't be too rough,

     
    hakikisha inachanganyika vizuri na unga wote umelowana kusiwe na unga mkavu au mabonge bonge.

     
    Tupia mboga majani na uendelee kuchanganya

     
    Sasa mchangayiko wako utakua mzito na safi kabisa

     
    Chota mchanganyiko wako na kisha weka kwenye muffin cups.  Hakikisha kabla ya kuweka mchanganyiko wako unapaka mafuta katika hizo cups ili pizza yako isishike baada ya kuiva.

     
    Chota pizza sauce 1 kijiko kidogo cha chai kisha weka juu ya kila moja wapo

     
    Mwisho unachukua ile mozzarella cheese ilyokwaruzwa na unamwagia kwa juu.

     
    Choma katika oven kwa dakika 20

     
    Choma mpaka upate rangi ya kahawia au mpaka ukichoma toothpick  katikati inatoka safi kabisa.  Kisha toa katika oven na iache ipoe kwa dakika 5 kabla hujazitoa kwenye tray uliochomea,

     
    Zikishapoa muonekano ndio huo weka juu ya mweza kisha anza kuzitoa moja moja.  Unaweza kuigandisha pizza hii kwenye freezer tumia an airtight container na inaweza kukaa kwa mwezi mzima; siku ukitaka kula basi toa kwenye freezer na yeyusha katika joto la chumba au  room temperature pole pole usitumie microwave.


    Ukikata kwa ndani muonekano ndio huu, safi sana waaandalie family wafurahie
     

    No comments: