CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA

Thursday, May 16, 2013

 
HABARI WAPENZI WA BLOG HII NIPO ONLINE KWASASA NINAWEKA MAELEZO KATIKA VYAKULA VYOTE MUDA SI MREFU VYAKULA VYOTE VITAKUA NA MAELEZO KAMILI PAMOJA NA RECIPE MPYA
 
CHEF ISSA

Friday, May 10, 2013

JIFUNZE KUPANGA RATIBA YA MLO WA NYUMBANI KWA WIKI NZIMA

 
BAADA YA MAOMBI YA WANAFAMILIA WENGI WA KITANZANIA SASA NIMEAMUA KUFANYIA KAZI PIA RATIBA YA CHAKULA YA WIKI NZIMA KWA FAMILIA KUANZIA CHAI ASUBUHI, CHAKULA CHA MCHANA NA CHAKULA CHA JIONI.
 
KITABU KITAZINGATIA SANA MBINU ZA MAPISHI BORA KWA GAHARAMA NA FUU NA LADHA SAFI KWA CHAKUAL KITAKACHOKUA NA FAIDA NA MWILI WAKO.
 
PIA NITATENGENEZA NA DVD ITAKAYOKUA INAELEKEZA MAFUNZO YOTE YALIYOKUWEPO KWENYE KITABU HIKI. KITAKAPOKUA TAYARI NITAWAFAHAMISHA KUPITI UKURASA WA FACEBOOK.COM Active Chef NA www.activechef.blogspot.com
 
 
TUOMBEANE UZIMA, AFYA NA MAISHA MAREFU AMIIN ILI KILA ZURI NILILOJAALIWA TUWEZE KUGAWANA KWA NJIA MOJA AU NYINGINE AMIIN
 
 


JIFUNZE KUANDAA CHAKULA BORA NA SALAMA KWAJILI YA MWANAO

 
HABARI NJEMA WAPENZI WA BLOG www.activechef.blogspot.com MAMA YANGU MZAZI NI MTAALAMU WA CHAKULA NA LISHE NAMI NI MTAALAMU WA KUPIKA CHAKULA BORA NA SALAMA.
 
TUNASHIRIKIANA KUANDAA KITABU KITAKACHOKUA NA RATIBA YA WIKI NZIMA YA CHAKULA CHA WATOTO WA UMRI TOFAUTI, MAELEZO JINSI YA KUKIANDAA CHAKULA NA MAELEZO YA FAIDA YA CHAKULA HICHO KATIKA MWILI WA MTOTO KWA LUGHA YA KISWAHILI FASAHA NA VYAKULA VINAVYOPATIKANA POPOTE KWA URAHISI.
 
KITABU KITAKAPOKUA KIMECHAPISHWA TAYARI NITAWAFAHAMISHA WAPI VINAUZA NA KIASI GANI BADO TUPO KATIKA MAANDALIZI KWA HABARI ZAIDI USIACHE KUJIUNGA KATIKA UKURASA WETU WA FACEBOOK KWA HABARI ZAIDI NI facebook.com Active Chef
 
 
 
 
 

Wednesday, May 8, 2013

HABARI NJEMA ZITAWADIA MUDA SI MREFU LEO HII

 
 
HABARI WAPENZI WA BLOG HII YA CHAKULA BORA NA SALAMA NIMEKUA KIMYA KWA MUDA KUTOKANA NA MAJUKUMU YA KIMAENDELEO LEO
 
 
NIMERUDI TENA NDUGU ZANGU NA HABARI NJEMA KWENU KWANZA ANGALIA CHAKULA HIKI KISHA NIAMBIE UMEGUNDUA NINI?
 
 
KAZI KUBWA NI YA UTAFITI WA CHAKULA, MIMI NA WENZANGU TUNAFANYA UTAFITI WAKUCHANGANYA UTAALAMU WA UPISHI WA MATAIFA YA SCANDINAVIA NA AFRIKA NA KUONA WALAJI WATAIPOKEAJE BAADA YA HAPO TUTAANDAA KITABU CHA MCHANYIKO HUO WA TAALUMA SIPATI PICHA NITAKAVYOWALISHA WAZUNGU UGALI, KISAMVU, MLENDA NA MAKANDE HAHAHAAAAA
 
 
HALI YA HEWA NI NZURI SANA HAPA KISIWANI
 
 
SAFARI YANGU YA KUELEKEA KISIWANI ILIANZIA HAPA NIKAPANDA BOAT NA KUELEKEA KISIWANI KWAJILI YA KUANZA KAZI
 


Friday, April 12, 2013

JIFUNZE KUPIKA KITAFUNWA HIKI CHA MAHARAGE YA SAOYA PIA UNAWEZA KULA KAMA MBOGA

 
KAA TAYARI KWA RECIPE SAFI KABISA YA KITAFUNWA HIKI CHA MAHARAGE YA SAOYA PIA UNAWEZA KULA KAMA MBOGA WEEKEND HII NI TAMU RAHISI NA NI NAFUU KUANDAA

MAHITAJI

JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI














 
 
 
Picha na maelezo yanakuja muda si mrefu


JIFUNZE KEKI YENYE MCHANGANYIKO WA KARANGA SUKARI YA KAHAWIA NA KAHAWA YA UNGA

 
 
HEHEHEEEEEEEEEEEEE UNAKUMBUKA ENZI ZA PIPI TOFFIIIII?? KAA TAYARI KWA RECIPE SAFI KABISA YA KEKI YENYE MCHANGANYIKO WA KARANGA SUKARI YA KAHAWIA NA KAHAWA YA UNGA WEEKEND HII NI TAMU RAHISI NA NI NAFUU KUANDAA

MAHITAJI

JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI













 
 
 
maelezo yanafatia muda si mrefu


JIFUNZE KUPIKA YA MUFFIN YENYE MCHANGANYIKO WA VIPANDE VYA CHOCOLATE NA KARANGA

 
RECIPE SAFI KABISA YA MUFFIN YENYE MCHANGANYIKO WA VIPANDE VYA CHOCOLATE NA KARANGA NI TAMU RAHISI NA NI NAFUU KUANDAA

MAHITAJI

250 gram siagi laini
250 sukari
2 mayai
250 gram plain yogurt
1 kijiko kidogo cha chai vanilla
500 gram  unga wa ngano
1 kijiko kidogo cha chai baking soda
1/2 kijiko kidogo cha chai baking powder
1/2 kijiko kidogo cha chai chumvi
180 gram vipande vya chocolate
1 kijiko kidogo cha chai cinnamon powder
4 kijiko kikubwa cha chakula karanga za kuoka
2 kijiko kikubwa cha chakula sukari ya brown
60  gram vipande vya chocolate

JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI
 
Muda wa maandalizi : Dakika 30
Muda wa mapishi : Dakika 30
Idadi ya keki : 12 Muffins
 

Katika bakuli changanya sukari na siagi pamoja.

 
Kisha mimina mayai pole pole endelea kuchanganya katika mchanganyiko wa sukari na siagi.

 
Kisha ongeza yogurt na vanilla na uchanganye ichanganyike vizuri.

 
Kisha chukua bakuli safi na uchanganye unga wa ngano pamoja na baking soda, baking powder na chumvi.

 
Kisha chukua mchanganyiko wa unga kisha mimina polepole katika mchanganyiko wa mayai.

 
Kisha mimina vipande vya chocolate na uendelee kuchanganya polepole.

 
KIsha chukua tray ya kuokea na weka vikombe vya karatai kisha mimina mchanganyiko wako 2/3 hakikisha isijae kabisa.

 
Kisha chukua bakuli kavu weka vipande vya chocolate vilivyobakia, cinnamon powder na karanga changanya pamoja.

 
Kisha mwagia kwa juu mchanganyiko huo kwenye tray ya kuokea izibe ile nafasi iliyobakia.

 
Hakikisha oven unaiwasha dakika 5 kabla ya kuoka Choma katika ovena katika moto wa 350F kwadakika 20 had 30. Poza keki zako kwa dakika 5 kabla ya kuzitoa katika pan.

 
Naimani ukizieweka sehemu nzuri ukafunika safi zisiguswe na wadudu zinaweza kukaa kwa siku tatu bila ya kuharibika!

 
 WAANDALIE FAMILIA AU WATEJA WAKO WAFURAHIE.
 
 


Saturday, March 30, 2013

JIFUNZE JINSI YA KUPIKA MKATE HUU MWEUPE

JIFUNZE KUTENGENEZA MKATE HUU MWEUPE NI RAHISI NA NAFUU KUANDAA ONYESHA UJUZI WAKO KATIKA FAMILIA
 
MAHITAJI
 
1 kg unga wa ngano
2 kijiko kidogo cha chai chumvi
240 gram maziwa ya maji ya vugu vungu
60 gram maji ya vugu vugu
2 kijiko kikubwa cha chakula siagi, iyeyushe
3 kijiko kikubwa cha chakula asali
2 kijiko kidogo cha chai amira ya chenga

JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI
 
Muda wa maandalizi : Masaa 2 hadi 4
Muda wa mapishi : Dakika 30 hadi saa 1
Idadi ya walaji : Watu 4
Ujazo : Unapata mkate wenye 9-inch
 
 
Chukua robo tatu ya unga pamoja na chumvi kisha chukua mchapo na uchanganye. 

 
 Chukua bakuli safi kavu kisha changanya maziwa, majina, siagi, chumvi pamoja na amira. Hakikisha joto la maziwa na maji liwe 110 degrees.

 
 Mimina mchanganiko wako wenye maziwa katika unga.

 
Anza kukanda pole pole 

 
Hapa mchanganyiko wako umeshaanza kushikana. 

 
Chukua mchanganyiko wako kisha weka juu ya meza hakikisha umemwagia unga kwa juu endelea kukanda vizuri kwa dakika 10.

 
Kama unafikiri mchanganyiko bado una maji maji, basi chukua robo ya unga iliobakia tumia kijiko kikubwa cha chakula ongeza kimoja kimoja epuka kuweka unga wote ukazidisha.

 
Chukua bakuli safi na kavu, kisha lipake mafuta na weka mchanganyiko wako katika hiyo bakuli. 

 
KIsha tumia plastic na funika weka sehemu yenye joto, jikoni kuna joto.

 
Hakikisha mchanganyiko wako umeongezeka mara 2, ndani ya dakika 40 mpaka 50. 

 
Kisha chukua mchanganyiko wako ukande vizuri na weka katika chombo chako cha kuokea kiwe cha chuma au cha kioo kama changu chenye ukubwa wa  8.5 X 4.5 X 2.5 (1.5 Lita).

 
 Kisha funika tena kwa plastic

 
 Weka pembeni kwa dakika 20 mpaka 30 itakua imeshaumuka vizuri kama unavyoona katika picha weka katika oven.

 
 Kumbuka oven yako unatakiwa uiwashe kabla katika joto la 350 degrees, ukishaweka unga katika oven unaweza rushia maji kidogo ili kuweka mvuke utakao saidia kuweka rangi nzuri ya brown na kua na gamba gumu. Oka kwa dakika 40 mpaka 50 mkate wako utakua umeiva.

 
Toa mkate wako katika pan, hamishia katika wire rack, ili mkate uweze kupoa.

 
Kata kata vipande na wapatie walaji, unaona mkate ulivyochambuka. 

 
Unaweza ukavuta picha huu mkate ni mtamu kiasi gani ukishapaka siagi kwajuu? au ukipaka jam pia? Ni mtamu sana sana.