CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Sunday, October 27, 2013

JIFUNZE KUTENGENEZA KEKI HII YENYE MCHAGANYIKO WA MATUNDA

RECIPE SAFI KABISA YA KEKI HII YA TUNDA AINA YA CHUNGWA 
MAHITAJI
420 gram unga wa ngano
240 gram Sukari
2 kijiko kidogo cha chai Baking Powder
1/2 kijiko kidogo cha chai chumvi
120 gram siagi au Vegetable Oil
240 gram juice ya chungwa
1 chungwa kwaruza ganda lake
2 pc ute mweupe wa yai
2 kijiko kikubwa cha chakula Icing sugar
JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI

Chukua bakuli safi kavu kisha weka unga wa ngano, sukari, baking powder pamoja na chumvi



Kisha weka juisi ya machungwa pamoja na vegetable oil au siagi itategemea unachopenda au aina ya mafuta uliyonayo tumia mchapo piga mpaka ilainike.


Chukua bakuli nyingine safi na kavu weka ute mweupe wa yai kasha piga mpaka ilainike na upate povu kama muonekano katika picha.


Kisha chukua ule mchanganyiko wa chungwa mwagia pole pole kwenye povu la ute mweupe na tumia mwiko kukoroga pole pole ichanganyike fanya hivyo mpaka mchanganyiko wote umalizike.


Paka mafuta mazito pembeni mwa chombo cha kuokea keki yako na kasha mwagia mchanganyiko wako wa keki kwenye chombo cha kuokea.


Bake kwa muda wa saa 1 kwenye oven ambayo tayari inamoto wa wastani, kama huna uhakika tumia toothpick choma kati kati ya keki ikitoka kavu basi kekei imeiva na ikitoka na uji basi bado haijaiva ongeza muda.


Ikishaiva toa nje ya chombo cha kuokea kwadakika 10, kisha mwagia kwa juu icing sugar



MUONEKANO MZURI WA KEKI FURAHI NA FAMILIA


Friday, October 25, 2013

JIFUNZE KUTENGENEZA KITAFUNWA HIKI CHA MCHANGANYIKO WANDIZI MBIVU MGANDO NA CHOCOLATE

KWA RECIPE NA UPDATE ZA MAPISHI CLICK LIKE active chef kwenye facebook.com
 KITAFUNWA HIKI CHA MCHANGANYIKO WA NDIZI MBIVU MGANDO NA CHOCOLATE NA MCHANGANYIKO WA KARANGA NI RAHISI SANA KUANDAA
 
MAHITAJI
 
 3 pc ndizi mbivu
240 gram Semi-Sweet Chocolate Chips ( Vipande vya chocolate)
2 Kijiko kikubwa chachakula siagi iliyoyeyushwa
3 Kijiko kikubwa chachakula mchanganyiko wa karanga aina yeyote utakayokuanayo mfano (Almonds, Pistachios, Pecans, Hazelnuts, Walnuts, karang au korosho), weka zote au chagua uzipendazo tu.

JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPA CHINI
Muda wa maandalizi : Dakika 15
Muda wa mapishi : Dakika 15
Idadi ya walaji : Watu 4 vipande 15 hadi 20

 
 
Kata kata ndizi katika vipande vidogo vidogo mfano kama muonekano kwenye picha.
 
 
Chukua alluminium foil kisha ifunike katika sahani pan au tray vizuri na upande juu yake vipande vya ndizi mbivu vilivyokwisha katwa.
 
 
Kisha chukua cocktail forks au uma ya plastic zinapatiana katika supermarket pia unaweza weka chochote kitakachokua rahisi kushika . Kisha zigandishe kwenye friza kwa masaa 2 au mpaka zitakapo ganda tu toa.
 
 

Wakati unaweka katika friza muda huo huo anza kukaanga pamoja karanga za mchanganyiko ulionao .
 
 
Zikaange tu kwa wastani zinukie harufu safi kisha zitoe na uzikate kate katika vipande vidogo na ziweke pembeni  zipoe.
 
 
Baada ya ndizi kuganda sasa Chukua sufuria dogo weka maji robo kisha chukua akuli ya kioo kubwa na uweke juu yake acha maji yachemke kisha weka mchanganyiko wa siagi na chocolate chips ndani ya bakukuli ya kioo juu ya sufuria. Kumbuka kuendelea kukoroga mpaka siagi yote iyeyuke na chocolate yote iyeyuke na kua laini safi kabisa.

Pia unaweza tumia njia mbadala ambayo ni microwave lakini unatakiwa uwe mzoefu sana kwani unaweza zidisha muda wa kuyeyusha ikawa mbaya.
 
 
Toa ndizi zilizoganda katika friza, chovya kwenye mchanganyiko wa siagi na chocolate.
 
 
Kisha toa unaweza mwagia mchanganyiko wa karanga kwa juu yake au unaweza kuroll
 
 
KIsha unairudisha kwenye ile sahani ya badidi mpaka ikauke vizuri.
 
 
Kumbuka pia unaweza tumia chocolate hata zapaketi kama utakosa chocolate chips. Endapo itakua imebaki chocolate sauce unaweza itunza kwa kufunika na kuweka jikoni katika kabati kwa muda wa mwezi mmoja na isiharibike na sio kwenye  fridge. Waandalei familia watafurahia au tengeneza kwa biashara.
 

Friday, October 18, 2013

NAMSHUKURU ALLAH NIMEPATA TUZO NYINGINE YA HESHIMA YA MAFANIKIO KATIKA MAPISHI YA KIAFRICA

 
NAFURAHI SANA KUWAFAHAMISHA NDUGU ZANGU KUA NIMETUNUKIWA SARAFU YA HESHIMA YA KUTAMBUA MCHANGO WANGU JUU YA MAFUNZO YA CHAKULA KWA LUGHA YA KISWAHILI PAMOJA NA KUENZI MAPISHI YA KIAFRICA.
 
NILIPATA TUZO HII TOKA KATIKA MASHINDANO YA KUMTAFUTA CHEF BORA WA MWAKA 2014 KWENYE NGAZI YA NUSU FAINALI KATIKA MJI WA LINGKOPING NA FAINALI ITAFANYIKA MJINI STOCKHOLM TAREHE 7/2/2014 UKUMBI WA WATERFRONT.
 
TUZO HII  NILIPATIWA NA ALIEKUA JAJI MKUU WA MASHINDANO HAYO SIKU HIYO Chef Markus Aujalay PIA ALIFANIKIWA KUWACHEF BORA WA SWEDEN MWAKA 2004 PIA NI CELEBRITY Chef ANAEMILIKI RESTAURANT NA AKIONGOZA KIPINDI MAARUFU CHA MAPISHI KATIKA TV SWEDEN MASTERCHEF.
 
 
Safari ilikua ni ya masaa 3 kutoka mji ninaoishi mpaka mji uliokua mashindano yanafanyika namshukuru Allah nilikwenda na kurudi salama amiin.

 
Katika picha hapo juu Chef Issa nikiendelea kutathmini Chefs wakiendelea kupambana
 
 
Huyu ndio alikua Jaji mkuu wa mashindano hayo ya nusu fainali siku hiyo anaitwa Chef Markus Aujalay Chef bora wa mwaka 2004 wa Sweden.

 
Ilitengwa sehemu maalumu ya sisi waalikwa kutathmini vyakula baada ya kupangwa katika sahani na majaji kuonja na kutoa alam a ushindi.

 
Chef waalikwa wakiendelea kupata taswira za vyakula toka kwa chef washindani

 
Walijitaidi sana kwakweli kuonyesha ubora wao, safari bado ni ndefu na mashindano ni magumu sana

 
Taswira ya ukumbi toka kwa juu

 
Taswira ya meza kuu toka kwa juu

 
Taswira hii inakuhakikishia kua chef Issa alikua mweusi pekee katika mashindano haya hivyo ilikua heshima kubwa sana kwangu na kwa taifa langu kutambulika kwa uwezo wangu na mchango wangu na utaifa wangu mhhh Viva Tanzania.

 
Utaratibu ulikua ukimaliza kuandaa chakula unaenda mbele ya kamera na kuanza kujieleza kwa majaji na watazamaji waliokua wanaangalia live aina ya chakula ulichotengeneza na mbinu ulizotumia
 
 
Upande wa pili ilikua ni maonyesho y vyakula ya chef waliopo huoni wenye umri wa kuanzia miaka 13 mpaka 16. Pia makampuni maarufu y chakula na yanayojihusisha na vyombo vya jikoni kama Electrolux, Santamaria, Arla na mabingwa wa visu duniani Global pia walikuwepo kutangaza bidhaa zao.

 
 ALHAMDULILAH HII NDIO TUZO YA HESHIMA NLIOTUNUKIWA.