CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Thursday, December 31, 2009

KARIBUNI SANA KATIKA LIBENEKE LA CHAKULA

Ndugu zangu namshuku sana mwenyezi mungu kwakuniwezesha kumaliza masomo yangu salama Pia natoashukurani zangu za dhati kwa Familia yangu yooote kwa sapot yenu kubwa.

Mimi chef Issa nimeamua kuanzisha libeneke la fani ya chakula ambapo wale wote wenye taaluma hii na wapenda chakula cha aina yeyote watapata fursa ya kujifunza kutoa maoni na kufundisha pia mapishi ya aina mbali mbali tutakaribisha recipe mbalimbali toka kwa yeyote atakaye penda kuchangia mawazo lengo nikubadilishana ujuzi ili kila mmoja wetu afaidike na utaalamu wa mapishi ya ladha zote, mchango wowote ule utaheshimiwa sana.

Tutakua na historia ya vyakula toka mataifa ya ulaya magharibi ambayo ni maarufu kwa vyakula vyao toka enzi hizo vikipikwa kwamtindo wa zamani tuliouzoea na pia vikibadilishwa kwamtindo mpya wa kisasa vikibaki na majina yaleyale hubadilika kwa kunakishiwa kwa mitindo mbalimbali pia tutapata wasaha wakujua historia ya vyakula na utambulisho kinatoka nchi gani na hasa tutagusa mataifa mama kwa nchi za magharibi katika sanaa hii ya chakula ikiwa ni Spain, England, France, German, Austria, Switzerland na Italy pia tutaangalia utaalamu sifa na aina za cheese, utundu wa kutengeneza na kunakshi chocolate na historia yote kwaujumla pia tutapata nasaha ya kuona vifaa mbalimbali na kujifunza kuchonga matunda na mboga ktk maumbile tofauti mfano tunda kama apple unatengeneza bata mzinga inapendeza sana.

Hakika ushirikiano wenu ndugu zangu utaifanya blog hii iwe chuo bora cha kubadilishana utaalamu wa fani hii ya chakula. Kwasasa nakaribisha maoni yenu tuanze na nini baada ya maelezo yote hapo juu ili blog hii iboreshwe zaidi na kila mmoja wetu afaidi? Pia nashughulikia uwezekano wa kufundisha kwa njia ya video hapa hapa katika blog yetu wanajamvini na ma chef wenzangu wazalendo karibuni sana sana sana. Nawatakia kheri ya mwaka mpya 2010 cheers!!

TAMBUA UMUHIMU NA FAIDA YA KULA MATUNDA NA MBOGA MAJANI


  APPLES Protects your heart, prevents constipation, Blocks diarrhea, Improves lung capacity Cushions joints

APRICOTS Combats cancer, Controls blood pressure ,Saves your eyesight ,Shields against Alzheimer's ,Slows aging process

 ARTICHOKES Aids digestion, Lowers cholesterol, Protects your heart, Stabilizes blood sugar Guards against liver disease

AVOCADOS Battles diabetes, Lowers cholesterol, Helps stops strokes, Controls blood pressure Smoothes skin

 BANANA Protects your heart, Quiets a cough, Strengthens bones, Controls blood pressure, Blocks diarrhea

BEANS Prevents constipation, Helps hemorrhoids, Lowers cholesterol, Combats cancer, Stabilizes blood sugar

 BEETS Controls blood pressure, Combats cancer, Strengthens bones, Protects your heart, Aids weight loss

 BLUEBERRIES Combats cancer, Protects your heart, Stabilizes blood sugar, Boosts memory , Prevents constipation

BROCCOLI Strengthens bones, Saves eyesight, Combats cancer, Protects your heart, Controls blood pressure

CABBAGE Combats cancer, Prevents constipation, Promotes weight loss, Protects your heart, Helps hemorrhoids

CANTALOUPE Saves eyesight, Controls blood pressure, Lowers cholesterol, Combats cancer Supports immune system

CARROTS Saves eyesight, Protects your heart, Prevents constipation, Combats cancer, Promotes weight loss


Baada ya utambulisho wa umuhimu na faida ya kula matunda na mboga kwani kila mboga na kila tunda vina nafasi tofauti ya kujenga na kulinda mwili. Watoto wengi wanasumbua sana kwenye kula hasa mboga majani asilimia kubwa sio wapenzi angalu upande wa matunda watoto wengi hupenda matunda lakini kwa kuchagua sio matunda yote watapenda kula tabia hii hujitokeza kwa kila mtoto hakuna aliekamilika nakumbuka hata mimi nilipokua mtoto nilikua nasumbua sana kula kiasi ikapelekea kua na afya dhaifu wakati wa kukua kwangu mpaka nilipobadili tabia na kuanza kula bila ya kufatiliwa.

Unaweza badilisha tabia ya mtoto wako au mtu yeyote unaeishi nae nyumba moja asiyependa kula mboga majani au matunda kwa kubadilisha muonekano wa chakula hicho au tunda hilo kwa kulinakshi kwa mtindo wowote ule ilimradi kionekane kitu tofauti na kinachovutia hii itakua njia rahisi sana kumvutia mtoto au mkubwa chakula kizuri au upambaji wa chakula sio mpaka hotelini hata nyumbani unaweza fanya sanaa hii na wala haiitaji muda mrefu wa maandalizi muonekano bora wa chakula hutia hamasa kwa mlaji leo tutaangalia utengenezaji wa salad na kuipamba na uandaaji wa mboga ktk muonekano wa kuvutia upande wa kuchonga matunda tutaangalia wakati ujao fata maelezo jinsi ya kutengeneza salad yenye mchanganyiko wa mboga mboga hapo chini.




Hili ni jokofu la kutunzia mchanganyiko wa mboga katika nyuzi joto 4 hadi 5 tu kwa hali ya usalama sana kwa manufaa na afya ya mlaji tukianzia juu kushoto ni mahindi mabichi ya njano kabla huifadhiwa katika kopo tayari kwa matumizi, karoti iliyokwaruzwa, Lime stone lettuce, chicory, Radish iliyokwaruzwa, zucchin iliyokwaruzwa, rollo nyekundu, rollo ya kijani, matango yaliyokatwa, celeriac salad, curly endive, chicory nyekundu.



Katika sahani yako anza kupanga mboga ambazo zimekatwakatwa  ambazo ni karoti, matango, mahindi machanga ya njano, celeriac salad na  radish nyeupe

Chota kidogo kidogo kila moja panga kwa mtindo wa duara nusu sahani tu kama mduara wa nusu mwezi kati kati acha nafasi kiasi.

Baada ya hapo chukua jani la salad moja moja toka kila aina ya salad pagange sambamba majani hayo kisha zungusha yabane kama unataka kuyafunga kamba kisha kata kiasi upande wa chini utakua umepata kitako safi utakua umetengeneza kama uwa rozi.

Kisha liweke juu ya zile mboga mboga pembei yake kata kipande cha tikiti maji rangi yeyote ile kama ni la kijani, jekundu au rangi ya chungwa pamba kama invyoonekana katika picha.

Kisha kata slice nyembamba ya chungwa katikati yake weka tunda lolote dogo la mviringo kama zabibu au strawbery chomeka toothpick ili ishikilie chungwa juu ya tikiti maji.

Salad hii unaweza mwagia dresing yeyote ile mfano italian dressing, french dressing au siki na chumvi inatosha salad hii unaweza kula na kipande cha kuku, samaki wakuchemsha au wa kukaanga na unakua umekula mlo safi kabisa bila stach kwa watu wanaofanya dayati hapa ni mahala pake mvuto na muonekano wa sahani utamfanya mlaji avutie hata kama si mpenzi wa mboga na matunda.



Hili ni jokofu la kutunzia mchanganyiko wa mboga katika nyuzi joto 4 hadi 5 tu kwa hali ya usafi sana kwa manufaa na afya ya mlaji tukianzia juu kushoto ni nanasi iliyopikwa katika sukari, embe mafuta, cappers, vitunguu vidogo vya kopo,  chopped chives, chopped onion, olives nyeusi, asparagus, matango machanga yaliyosindikwa, olives zakijani, Nyanya



Katika sahani yako anza kupanga mboga ambazo zimekatwakatwa ambazo ni karoti, matango, mahindi machanga ya njano, celeriac salad na radish nyeupe.

Chota kidogo kidogo kila moja panga kwa mtindo wa duara kuzunguka sahani yote katikati acha nafasi.

Baada ya hapo chukua jani la salad moja moja toka kila aina ya salad pagange sambamba majani hayo kisha zungusha yabane kama unataka kuyafunga kamba kisha kata kiasi upande wa chi utakua umepata kitako safi utakua umetengeneza kama uwa rozi.

Kisha liweke pembeni ya zile mboga mboga katikati ya sahani unaweza weka mchanganyiko wowote ule wa nyama ya kuku, ngo'mbe, samaki au sausage iliyochemshwa ikapoa.

Kata saizi ya kuweza kuingia mdomoni kisha changanya na vitunguu vilivyochopiwa safi pamoja chives.

Mchanganyiko huo unaweza malizia na chaguo lako la dresing yeyote uipendayo kisha unamwagia kati kati ya sahani mwisho kata nyanya kipande weka pamoja na tango dogo la kopo na olive moja ya kijani na moja nyeusi kwa kupamba salad yako.




Kwa upande wa mlo kamili baada ya kupika chakula chako kikaiva kama ni ugali au wali

Chemsha njegere zisiive sana

Kisha kata vitunguu vidogo sana kaanga katika siagi dakika 1 tu

Kisha weka hizo njegere zilizoiva katika sufuria kwa dk 2 usiasahau chumvi kisha zitoe

Chukua nyanya nzuri ngumu iliyokwisha iva kata nusu pia kata kidogo katika kitako ili iweze kukaa katika sahaki

Kisha toa mbegu zote katikati ya nyanya tumia kijiko kuchota na jaza zile njegere kwanye nyanya

Kisha save nyanya hiyo yenye njegere kama mboga majani itakayo ambatana na chakula chako kama ni cha mchana au cha usiku.

Muonekano na mchanganyiko wa rangi inakua kivutio kizuri sana kwa mtu asiependa kula mboga majani.




Sasa hapa ndio utawakamata kweli kweli wasiopenda kula mboga za majani,

Chukua maharage mabichi yachemshe kiasi yasiive sana yabaki na rangi yake nzuri ya kijani

Kisha unachukua bacon slice zipo aina mbili zipo bacon za nguruwe na bacon za ng'ombe chaguo ni lako mlaji.

Kisha chukua maharage hesabu kumi na tano kisha zungushia bacon katika maharage hayo weka katika ubao wa kukatia kata ncha za mwisho ili kuweka usawa na muonekano mzuri zaidi.

Ukishamaliza weka kikaango kwenye jiko la moto wa wastani tu weka mafuta kiasi katika kikaango yakishapata moto weka maharage yaliyozungushiwa bacon kaanga kiasi tu ili ile bacona ikauke.

Kisha toa tayari kwa chakula pia sevu kama mboga majani itakayo ambatana na chakula chako kama ni cha mchana au cha usiku. Muonekano na mchanganyiko wa rangi inakua kivutio kizuri sana kwa mtu asiependa kula mboga majani.
 
KWA KUFATILIA MAELEZO HAYA YOTE UTAKUA UMEFANIKIWA KUMREKEBISHA KAMA NI MUME AU MTOTO ASIEPENDA KULA MBOGA ZA MAJANI AU MATUNDA IKIWA UMESHAFAHAMU PIA UMUHIMU WA VYAKULA HIVYO KWA BINADAMU





Nashukuru sana mdau aliezungumzia upatikanaji wa bacon ya ng'ombe, nikweli kwa ulaya kupata bacon ya ng'ombe ni adimu sana ila hapa kwetu Tanzania zinapatikana kwa wingi ukienda katika supermaket kubwa au maduka makubwa ya nyama utapata.

Endapo umekosa basi chukua mboga hiyo hapo juu inaitwa leeks kata jani lake lisafishe vizuri kisha zungushia vizuri maharage yako hatua za upishi ni zile zile unaikaanga kidogo tu itaiva na italeta harufu nzuri sana kwahiyo kwa asie kula kabisa nyama atakua nae kafaidika.



Wednesday, December 30, 2009

WEWE KAMA MPISHI TAMBUA MAJUKUMU NA THAMANI YAKO YA KAU JIKONI


A Trainee Chef is still at cooking school, but doing a year of practical work in a restaurant’s kitchen, so they are learning while working.

A Commis Chef is an entry-level position, a chef who has just qualified. Commis chefs work under the chefs de parties to learn particulars of a station, through food preparation and plating.

A Chef de Parties is the first level of management in the kitchen, and is responsible for a particular section, such as pastries, sauces, soups, salads, vegetables, meat, poultry or fish.

A Sous Chef is the second in command in the kitchen, and is responsible for an entire shift, such as breakfast, lunch or dinner. They will demonstrate new cooking techniques and equipment to cooking staff.

A Head Chef or Chef de Cuisine is responsible for running a restaurants kitchen

An Executive Chef plans and directs food preparation and cooking activities in restaurants, and also supervises the many kitchens of a hotel, restaurant group, or conference centre. They plan menus and ensure that food meets quality standards.

A Group Executive Chef runs all the kitchens of a hotel or restaurant group, and oversees all the executive chefs.


More about the Chef & Kitchen industry


Chefs and cooks are key figures in the tourism and hospitality industry, and they work in a variety of food service establishments, including restaurants, hotels, spas, conference centres and country clubs. The Chef is responsible for what happens in the kitchen from developing the menu, hiring staff, food costing, ordering and stock control, to picking out the dinnerware and assisting with the design of the restaurant. They should have an advanced knowledge of food preparation and management, as well as knowledge of human resources, administrative procedures and business management.


 Huo ndio mtiririko na mgawanyiko wa madara jikoni vyeo kama jeshini na ni amri moja hakuna tafadhali jikoni kazi kwakwenda mbele na heshima ya hali ya juu ndiomaana wadau unatoaoda ya chakula katika mgahawa baada ya dakika kumi kipo mezani sio mchezo inabidi kujipinda kweli kweli kutoa chakula bora na salama kwa wakati muafaka. Ndugu zangu wapishi mnaochipukia nafasi ya kukua kitaaluma mnayo kikubwa tumienimuda mwingi kujifunza sana sana uweze kumiliki idara zote za jiko.

Tuesday, December 29, 2009

CHEF ISSA PIA ANAPENDA SANA SOKA



Siku ya graduation Timu ya culinary aka machef tulikabidhiwa kombe la ushindi upande wa soka na mmatumbi nilipiga goli mbili safi na kuisaidia timu yangu kunyakua ubingwa mashindano yalikua ni ya pale shuleni tu kila idara walikua na timu yao.



 Baadhi ya wachezaji wa timu ya Culinary kabla ya mechi wengine walikua wanapasha misuli




Chef Issa Akishangilia baada ya kufunga goli dhidi ya timu ya Uongozi wa hotel na matukio





Namshukuru mungu ilikua ni good time si mchezo maana kila baada ya tukio kinachofata ni misosi ya nguvu hapa ilikua BBQ night baada ya Sport day kumalizika spring mpaka summer jua huwa linazama saa 3 usiku



Hii ilikua kona ya salad na cheese kibao pamoja na nyama kavu



Hii ilikua kona ya vyakula vya mboga mboga



Na hapa haswa ndio ilikua ni BBQ yenyewe unachagua unachokitaka mpishi anarushia kwenye moto haraka naona wengi walipendelea kula mbavu za kondoo au sausage au hamburger steak na salad.




MAMBO YA KUCHONGA CHONGA MBOGA NA MATUNDA YATAKUWEPO



Wapenzi wa sanaa ya kuchonga chonga mboga na matunda watapa wasaha wa kufundisha na kujifunza zaidi mbinu mbali mbali za kuchonga maumbo mabli mbali kwa utaalamu zaidi ama kweli sasa fani itanoga kazi kwenu wataalamu wadau wanahitaji utaalamu wenu karibuni jamvini tubadilishane utaalamu.