CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Wednesday, June 29, 2011

JIFUNZE KUTENGENEZA MCHUZI WA MBOGA MAJANI NA NAZI


KAA TAYARI KWA RECIPE SAFI KABISA YA CHAKULA HIKI YA NAZI NA MBOGA MBOGA MCHANGANYIKO

MAHITAJI

120 gram Mtindi (yogurt)

1 kilo ya Mchanganyiko wa mboga ( karot, kiazi ulaya, njegere, pilipili hoho, bilinganya, kabichi na kitunguu)
1 kijiko kikubwa cha chakula cha mafuta ya nazi (coconut oil)
1 kijiko kidogo cha chai binzali nyembamba ( cummin seeds)
1 pili pili ya kijani mbichi
120 gram tui la nazi, ( Pia nazi ya kopo au ya paketi inafaa ingawa mimi napendelea nazi fresh)
0.5 kijiko cha chai unga wa manjao (turmeric powder)
5 gram chumvi



JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI

Muda wa kuandaa: 30 dakika mpaka saa 1

Muda wa kupika: Chini ya dakika 15
Idadai ya walaji : Watu 2

 


Saga kwa pamoja machicha ya nazi, pilipili ya kijani na cumin seed upate tui zito.


Baada ya kupata tui zito kisha weka pembeni.


Weka mchanganyiko wa mboga zako katika sufuria yenye maji moto kisha chemsha kwa dakika 3 mpaka 3 kumbuka kuweka unga wa manjano na chumvi.


Baada ya kuchemsha kwa dakika 3 au 5 mboga zako zitakua zimeiva na maji yatakua yamepungua ongezea tui la nazi na endelea kuchemsha.



Wakati inaendelea kuchemka chukua mafuta ya nazi kisha weka katika kikaango na kaanga manjani ya giligilani au coriender leaves .Ikishatoa harufu safi tu toa katika moto



Chukua kikaango na mimina majani hayo kwenye sufuria ili ichemke.


Kisha toa sufuria katika moto. Baada ya chakula hiki kupoa kiasi kwa 37C ongeza mtindi (yogurt)


Hakikisha unachanganya vizuri.


Mchuzi mzito wa mboga mboga na nazi upo tayari! Hapa unaweza kula na wali au chapati au chochote upendacho wewe.

 


Lengo la kusubiri ipoe kiasi ni kusaidia mtindi usikatike ikiwa utachanganya wakati chakula bado ni cha moto

WAANDALIE FAMILIA WAFURAHIE SANA



 



Saturday, June 25, 2011

HABARI NJEMA WAPENZI WA BLOG HII YA MAPAISHI

NIMECHAGULIA KUA MMOJA WA WASHINDANI KATIKA BLOG BORA ZA MAFUNZO YA MAPISHI TANZANIA SOMA MAELEZO HAPO CHINI NA UNIPIGIE KURA

 Tembelea http://www.tanzanianblogawards.com/   Kisha  nemda mpaka kitengo cha Best Food Blog  utaona jina la blog yako uipendayo http://activechef.blogspot.com/ na chini yake utaona neno hili Vote. una clik hapa kisha unakua umeshampigia kura chef Issa. Kura yako ni muhmu sana ili kuonyesha umuhimu na kuthamini mchango wa blog yetu ya culinarychamber.

NAWATAKIA KAZI NA SIKU NJEMA

CHEF ISSA

Friday, June 24, 2011

JIFUNZE KUTENGENEZA WAFFLE YENYE LADHA YA NAZI NA UKALA PAMOJA NA MATUNDA MCHANGANYIKO


KAA TAYARI KWA KUJIFUNZA NAMNA YA KUTENGENEZA WAFFLE YENYE LADHA YA NAZI NA KISHA UKAONGEZA LADHA KWA KULA PAMOJA NA MATUNDA MCHANGANYIKO NA UIFANYE SIKU YAKO KUCHANGAMKA

MAHITAJI

KWAJILI YA MCHANGANYIKO WA MATUNDA


2 Maembe yalioiva menya na kisha kata kata vipande vidogo
450 grams ya matunda strawberries au( mchanganyiko wa apple nekundu na kijani na zabibu)
1 kijiko kikubwa cha chakula sukari


KWAJILI YA WAFFLE

429gram unga wa ngano
2 kijiko kikubwa cha chakula asali
1 kijiko kikubwa cha chakula baking powder
1/2 kijiko kidogo cha chai chumvi
4 kijiko kikubwa cha chakula siagi isiyo na chumvi , iyeyushe
4 kijiko kikubwa cha chakula vegetable oil
300 gram maziwa ya maji cup
4 ute mweupe wa yai, yapige wastani
120 gram tui la nazi
60 gram machicha ya nazi
Fresh mint kwajili ya kupambia 



JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAFUNZO HAPO CHINI


Katika bakuli weka vipande vya maembe, strawberries na sukari



Funika matunda na karatasi ya nailoni mapak amatunda yatoe juices, kwadakika 90.Ni vizuri kama ukiandaa matunda haya usiku kucha yakakaa katika friji kisha ukayatumia asubuhi ya siku inayofuata.



Katika bakuli changanya unga, sukari, baking powder na chumvi.



Katika bakuli nyingine safi changanya siagi iliyoyeyushwa, maziwa, mayai na tui la nazi.



Chukua mchanganyiko wa unga na mimina pole pole kwenye mchanganyiko wa mayai na maziwa kisha koroga pole pole mpaka ilainike na kuchanganyika vizuri.



Mwisho weka machicha ya nazi



Hutakiwi kukoroga kwa nguvu sana itaharibu mchanganyiko wako koroga pole pole sana kiasi tu nazi hiyo ichanganyike na mchanganyiko wa unga



Washa ipate moto kwa mujibu wa maelekezo ya waffle maker's na pika mpaka iwe na rangi ya kahawia.



Muonekano huu ndio hasa inavyuotakiwa kua na ni tayari kwa mlaji kufurahia.



Mpatie mlaji ikiwa ya moto pamoja na mchanganyiko ule wa matunda yakiwa na ubaridi saafi 




MWISHO KABISA WEKA JANI LA MINT KWA KUPAMBA NA MLAJI ATAVUTIWA SANA NA MCHANGAYIKO SAFI WA RANGI NA LADHA. 


Tuesday, June 21, 2011

WAPENZI WA KINYWAJI KIZITO AU SMOOTHIE


 MAHITAJI

1 ndizi mbivu kubwa, chop chop
1 apple jekundu toa kokwa la kati kisha kata kata vipande vidogo iwe baridi
200 gram vipande vya embe dodo ilioiva vizuri iwe baridi
400 gram  frozen strawberries
240 gram juice ya chungwa ya baridi
120 gram mtindi (yogurt) baridi



JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAFUNZO HAPO CHINI

 Muda wa kuandaa: Dakika 15
Muda wa kupika: Dakika 15
Idadi ya walaji: Watu wawili 

Chukua mchanganyiko wako wa matunda yote weka katika blender au smoothie maker. Blend
vizuri kisha mimina kwenye glasi tarayi kwa kunywa


 


Hii ni smoothie safi sana ikiwa na nutrition ya kutosha. Ingawa ina fiber nyingi sana, vitamin C, potassium na antioxidants. Mtindi (yogurt inachangia acidophilus)


                                                                                                                                                                 



MAHITAJI

1 Avocado (menya kisha chop chop)

1 pear (menya kisha chop chop)
1/2 ndizi mbivu (chop chop)
120 gram mtindi halisi (plain yogurt)
1 asali kijiko kikubwa cha chakula




JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI

Muda wa maandalizi: Dakika 15
Muda wa mapishi: Dakika 15
Idadi ya walaji: watu 2

Katika blender weka mchanganyiko wa matunda yote kisha saga na weka katika friji ipoe kisha mpatie mlaji



Pia kuongeza ladha zaidi unaweza weka juisi ya limao.

Ni bora san wka afya na ina vitamin C kwa wingi, folic acid, flavanoids na potassium. Ni tamu sana na inafaa kwa mtu wa umri wowote ule. 


Thursday, June 16, 2011

JIFUNZE KUTENGENEZA MAHARAGE YA LADHA YA KUOKA


WATU WENGI WAMEKUA WAKINUNUA KATIKA MADUKA AU KULA KATIKA MAHOTEL MAHARAGE HAYA YA LADHA YA KUOKA AU BAKED BEANS SASA NI WAKATI MUAFAKA WA KUJUA JINSI YA KUYATENGENEZA NYUMBANI

MAHITAJI

480gram maharage mekundu, Loweka usiku kucha (Unaweza tumia maharage aina ya pinto)

1 Kitunguu kikubwa
1 fungu celery chop chop miti na majani yake
1 carrot kubwa kata mara 4
5 gram kitunguu swaumu kusagwa
5 gram tangawizi ya kusagwa
1 bay leaf
150 gram sukari
3 mbegu za karafuu
3 kijiko kikubwa cha chakula soy sauce
2 kijiko kikubwa cha chakula olive oil
5 gram chumvi
5 gram pili pili manga
JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI

Muda wa kuandaa : 8 masaa mpaka siku 1
Muda wa kupika: 30 dakika hadi saa 1
Idadi ya walaji: Watu 4


Chukua  pressure cooker, weka maharage, caroti, celery, kitunguu, kitunguu swaumu, karafuu, tangawizi na bay leaf. Weka maji kwenye sufuria yafunike urefu wa 1 inch.



Pika kwenye Pressure cook kwa dakika 10-15.



Baada ya hapo maji yatakua yamekauka weka chumvi, pili pili manga kisha ongezea soy sauce, sukari, olive oil na unendelee kukoroga  kwa dakika 1.



Kisha rudisha katika jiko kwa moto mdogo na usifinike sufuria yako, weka maji 400 gram chemsha kwa dakika 20 au mpaka utakapo ona yamelainika maharage. 

 


Baada ya hapo mchuzi wote utakua umekauka na utaona mchuzi mzito kabisa.


Muonekano mzuri wa maharage katika bakuli tayari kw amlaji kushambulia




Hakikisha unampatia mlaji yakiwa yamoto, maharage haya unaweza kula wakati wowote ule ingawa watu wengi hupenda kula asubuhi wakati wa chai. Pia Unaweza kula na mkate au chapati au viazi aina yeyote ile.

WAANDALIE FAMILIA YAKO WAFURAHIE

Wednesday, June 15, 2011

JIFUNZE KUANDAA SALAD HII YA AVOCADO NA NJEGERE

KAA TAYARI KWA RECIPE SAFI YA AVOCADO NA NJEGERE

Muda wa maandalizi dakika 30

Muda wa kupika dakika 15
Chakula kinatosha watu 2
MAHITAJI

480 gram njegere za kijani mbichi (chickpeas)

1 kubwa parachichi lililoiva limenye maganda (avocado)
1 fungu la gili gilani chop chop
120 gram kitunguu maji chop chop mimi natumia kitunguu cheupe (white onion)
1 pili pili hoho toa mbegu za ndani
1 limao kamua maji yake
1 kijiko kidogo cha chai chumvi
120 gram nyanya mbivu chop chop bila mbegu za ndani


JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA HAPO CHINI



Menya njegere zako kisha weka katika jagi la kupimia na upime kisha unaweka katika steamer mimi nilitumia hii hapo chini bamboo steamer ni kama chujio kwa chini unaweka juu ya sufuria yenye maji yaliochemka



Chemsha katika mvuke kwa dakika 6 mpaka 8. Kwenye maji unaweza chemsha kwa dakika 2 mpaka 3.


Kisha weka katika blenda au food processor pamoja na chumvi, limao na majani ya gili gilani



Saga mpaka iwe laini kabisa.



Kisha toa njegere katika blenda na uweke katika bakuli ´lenye avocado uliokwisha menya na uchanganye vitunguu chop chop, pili pili hoho chop chop na majani ya giligilani uliobakiza.



Kisha weka katika bakuli utakalo tumia mlaji na upambe juu pamoja na nyanya chop chop na majani ya gili gilani kwa kuongeza utanashati wa rangi. We enjoyed them along with tortillas, tortilla chips, tacos pia kwa chapati inapendeza sana.



Muonekano safi baada ya kupamba katika bakuli





WAANDALIE FAMILIA KWA KUBADILI LADHA YA CHAKULA NA KUBORESHA AFYA YA FAMILIA YAKO NAIMANI WATAIFURAHIA SANA


Friday, June 10, 2011

JIFUNZE KUTENGENEZA WALI WA NJEGERE

KAA TAYAI KWA RECIPE SAFI SANA YA WALI HUU WA NJEGERE

MAHITAJI
240 gram mchele wa Basmati
120 gram njegele za kumenywa (chickpeas)
3 majani ya kitunguu maji (spring onions), kata kata
1 fungu la giligilani chop chop
 1 fungu la parsley chop chop
1 kijiko kikubwa cha cakula siagi (butter) kwakuongeza ladha ya chakula
5 gram chumvi

UTAALAMU ZAIDI


Ukitaka kuongeza ubora wa muonekano na ladha unaweza weka zafarani au safron rangi yeyote ile wakati unapika wali wako. Pia unaweza kuweka aina tofauti ya viungo ipendavyo na wali ukaendelea kuvutia mlaji. 


JINSI YA KUANDAA FATILIA MAELEZO NA PICHA HAPO CHINI


Loweka mchele kwa dakika 30, sio lazima ingawa nakushauri tu kitaalamu.Binafsi huwa naloweka ili kusaidia kulowana na uive haraka pia uchambuke. Chukua kikaango weka siagi kisha ikiyeyuka weka majani kiasi ya kitunguu maji na uendelee kukaanga. Kisha chuja mchelewako wa basmati nao weka ukiwa mkavu na endelea kukaanga mpaka unukie.



 kisha weka chumvi pamoja na njegere koroga kiasi.



Kisha weka maji safi 400 gram hii inategemea na kiwango cha mchele wako,Funika mfuniko wa kikaango au sufuria yako na pika kwa dakika 10



Unaweza funua sufuria yako hata kabla ya dakika 10 hii inategemea na aina ya mchele pia kama uliloweka unaweza iva mapema zaidi. Ukiweka njegere mbichi kaaida zinaiva pamoja na wali wako na zinakua laini safi kabisa.


Kisha funua sufuria yako uangalie maendeleo.



Kisha weka chop parsley na chop giligilani kisha koroga zichanganyike na wali wako.



Baada ya hapo wali wako utakua umeiva na unaweza kula na mboga yoyote upendayo.




Chakula hiki kwa vipimo vilivyopo hapa kinatosha kuliwa na watu 3. waandalie familia yako wafurahie mapishi haya weekend hii.

Thursday, June 2, 2011

JIFUNZE KUANDAA CAROT HALWA

KAA TAYARI KWA KUJIFUNZA KUTENGENEZA KAROTI HALWA

Kuandaa ni dakika30 

Kupika ni dakika 30
Idadi ya watu kula ni 2

MAHITAJI
 
480 gram ya karoti ya kukwaruzwa (grated)
240 gram ya maziwa
1 240 gram ya fresh cream
120 gram ya samli (ghee)
240 gram ya sukari
1 kijiko kidogo cha chai unga wa hiriki (cardamom powder)
1 kijiko kikubwa cha korosho zivunje vunje


JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA HAPO CHINI



Pasha kikaango katika moto, kisha weka samli iyeyuke na weka karoti, kaanga mapaka upate harufu nzuri ya kuiva (distinct aroma).




Kisha weka maziwa pamoja na cream pika kwa dakika 10 mpaka maziwa na cream yakaukie kwenye caroti (absorbed).


Kisha weka sukari pamoja na hiriki pika mapaka ishikane kabisa.


KIsha chukua chombo chochote au kikombe na weka halua yako kisha mimina katika sahani juu yake weka zile korosho zilizo kaangwa au kuokwa kama pambo kwajuu na pamoja kuongeza ladha. Pia unaweza tumia Zabibu kavu (raisins)na zinapendeza sana.



HUU NI MUONEKANO WA HALUWA IKIWA KATIKA SAHANI TAYARI KWA KULA WATENGENEZEE FAMILIA YAKO WAFURAHIE.