CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Tuesday, October 25, 2011

JIFUNZE KUTENGENEZA KINYWAJI HIKI CHA STRAWBERY MCHANGANYIKO NA ICE CREAM

KINYWAJI HIKI NI BARIDI NA SAFI KWA LADHA YA TUNDA HILI NA UNAWEZA KUANDAA KWA MITINDO TOFAUTI KAA TAYARI KWA RECIPE

MAHITAJI

Kwajili ya Strawberry Syrup


400gram matunda ya Strawberries
300 gram Sukari


For the Frappucino (Approximate Measurements - Use as a guideline to cater to your preferences)

240 gram maziwa
240 gram Vanilla Icecream
60 gram Strawberry Syrup
6 matunda mazima ya Strawberries, kisha kata kata vipande
3 vipande vya barafu (ice cubes)
Whipped Cream (sio lazima)



JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAFUNZO HAPO CHINI

MUda wa maandalizi: Dakika 15
Muda wa mapishi : Dakika 15
Idadi ya walaji : Watu wa 2

 


Chemsha matunda ya strawbery pamoja na sukari kwa wakati mmoja iive mapaka yapondeke . Kish chukua chujio na chuja ili upate syrup.


Weka syrup kwenye ubaridi ipoe na inashauriwa ipoe kwa masaa 4.



Kisha weka katika blenda whipped cream, vipande vya barafu, maziwa, strawbery syrup na vipande vya strawberries bakisha kiasi kwajili ya kupambia.


Washa blenda mpaka mchanganyiko wako ujiblend. Ladha ya kinywaji hiki inategemea wewe mynwaji au familia yako inapenda nini hasa unaweza weka syrup nyingi au kidogo au ice cream nyingi inategemea nawe unavyopenda na utapata ladha uipendayo.


Kisha weka vipande vya strawberries katika  glasi anayotumia mywaji na pia mimina ule mchanganyiko wa strawberries na creme.


Sasa hapa unaweza ongeza utanashati zaidi kwa kuweka whipped cream juu ya glasi ya mnywaji na unatakiwa umpatie ikiwa yabaridi




MUONEKANO SAFI KABISA WA KINYWAJI HIKI TAYARI KWA KUJIBURUDISHA WAANDALIE FAMILAI YAKO WAFURAHIE KINWAJI HIKI NA UNAWEZA KUNYWA WAKATI WOWOTE PIA UNAWEZA KUNDAA KWA AINA TOFAUTI YA MATUNDA LAKINI KWA KUFATA MTINDO HUU HUU.


Saturday, October 15, 2011

HABARI NJEMA WAPENZI WA BLOG


KWAHERI DAR ES SALAAM NASHUKURU RAFIKI WOTE TULIOONANA

SHUKA MPAKA CHINI KABISA UTAONA JINSI YA KUPIKA NA KUPAMBA KEKI YENYE LADHA SAFI KABISA
.

NAWATAKIA SIKU NA KAZI NJEMA

CHEF ISSA


Wednesday, October 5, 2011

JIFUNZE KUPAMBA CHAKULA KATIKA SAHANI

HUONGEZA MVUTO NA PIA KUHAMASISHA HAMU YA KULA KWA MLAJI, KILA CHAKULA KINA AINA YAKE YA UPAMBAJI