CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Monday, November 25, 2013

JIFUNZE KUTENGENEZA ENCHILADA YA KUKU NA MAHINDI MABICHI

KAA TAYARI KWA RECIPE SAFI KABISA YA ENCHILADA YA KUKU NA MAHINDI MABICHI PIA HISTORIA YAKE

MAHITAJI
12pc tortilla za mahindi
480 gram nyama ya kuku
480gram mahindi mabichi (sweet corn) 
480 gram shredded cheese (cheddah)
1 kopo kubwa la enchilada sauce
sour cream (Sio lazima nikwajili ya kupambia)

JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI








Thursday, November 21, 2013

JIFUNZE KUTENGENZA KEKI YA NDIZI MBIVU

RECIPE SAFI KABISA NA JINSI YA KUETENGENEZA KEKI YA NDIZI MBIVU

MAHITAJI
360gram unga wa ngano
180 gram sukari
1 kijiko kidogo cha chai baking powder
1/2 teaspoon baking soda
1/4 kijiko kidogo cha chai chumvi
4 kijiko kikubwa cha chakula mafuta ya karanga
6 ndizi za kuiva zigandishe kwenye freezer
1/2 kijiko kidogo cha chai vanilla essence
100 gram korosho au karanga za kuoka

Kwajili ya Honey Cinnamon Frosting (Sio lazima)
300 gram Icing sugar
120 gram siagi isiyo na chumvi iyeyuke kama mafuta mgando yakupaka
1 kijiko kikubwa cha chakula Asali
1/8 kijiko kidogo cha chai unga wa cinnamon (Mdarasini)
 
JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAFUNZO HAPO CHINI


Washa oven yako katika moto wa 350 degrees. Chukua backing tray yenye mashimo 12 ya muffin kisha weka zile karatasi maalumu za kuokea au paper liners. Chukua bakuli safi kavu kasha changanya Unga wa ngano, sukari, baking powder na chumvi salt.


Kisha toa ndizi zilizokua katika freezer ziweke nje kwa dakika 20 zitoe barafu.
 
Menya ndizi na ziweke kwenye blenda saga mpaka upate rojo safi kabisa.

Kisha mwagia mchanganyiko wako wa ndizi kwenye mchanganyiko wa unga pamoja na mafuta ya karanga na vanilla.

Tumia mwiko kuchanganya pole pole mpaka mchanganyiko wako uchanganyike vizuri.
 
Chukua kijiko kikubwa au mwiko kisha anza kumimina pole pole kwenye mashimo ya muffin.

Hakikisha umegawanya vizuri mchanganyiko wako utimie maffin 12 na ujazo uwe kama muonekano katika picha.

Oka ukiweka toothpick kati kati ya muffin na ukitoa inatoka safi bila uji uji,  kwa dakika 25 hadi 30.

Zitoe muffin zako zikiwa bado katika zile karatasi maalumu za kuokea na weka zipoe ktk wire rack.

Kwajili ya Frosting ya asali:  Kisha chukua Asali, sukari ya unga, unga wa mdarasini na siagi ilyoyeyuka kama mafuta mgando ya kupaka.

Nakushauri kutumia mixer ya umeme, piga kwadakika 4 hadi 5 mchanganyiko utakua laini.

Unaweza tumia walnut au karanga au korosho chaguo ni lako kisha zi chop chop.
 
Nakushauri tumia piping bag kupambia kwajuu. Unaweza tumia hata kijiko kupambia.
 
Sio lazima kuweka frosting lakini ukiweka inapendeza zaidi na utamu ndio unazidi na harufu safi ya mdalasini.

Mafuta ya karanga yanasaidia sana keki yako isishike na iwe rahisi kutoa wakati wa kula pia kwa wenye matatizo ya kiafya hasa sukari usitumie frosting.

Unaona vizuri spongy kwa ndani? Ipo fluffy, light and very flavorful.

We enjoyed them the day I made them (for evening tea or breakfast the next morning after warming them up slightly. It makes a great breakfast too.
 
Mwagia kwa juu hizo karanga  zitaongeza ladha safi pia


Kama mchanganyiko wako utakua mzito basi unaweza ongeza maji ya vugu vugu 60 gram usitumie maziwa yataifunika ladha ya ndizi.

RECIPE SAFI SANA YA KITAFUNWA HIKI CHENEY LADHA YA NDIZI, MDARASINI NA ASALI

Saturday, November 16, 2013

JIFUNZE KUTENGENEZA KWA UMARIDADI NA UFASAHAA KIFUA CHA KUKU

KAA TAYARI KWA RECIPE SAFI KABISA YA KUTENGENEZA KIFUA CHAKUKU

MAHITAJI
1 kijiko kidogo cha chai Kosher Salt
1 kijiko kidogo cha chai Freshly Ground Black Pepper
1 kijiko kidogo cha chai Onion Powder
1 kijiko kidogo cha chai Garlic Powder
1 kijiko kidogo cha chai Dried Parsley Flakes

JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI

Changanya viungo vyote kwa mara moja kisha mwagia juu ya vifua vya kuku

Ukitaka upate harufu na ladha safi toka katika viungo hivi hakikisha umeasha moto na kikaango kipate moto wa kutosha kisha mwagia mafuta yakupikia yakutosha na mwagia pia viungo vilivyobakia kwenye kikaango kisha weka hivyo vifua vyakuku na upunguze moto uwe wa wastani.

Chukua mfuniko funika ila acha wazi kiasi kama muonekano kwenye picha lengo ni kupunguza mvuke isiwe kama tunachemsha badala ya kukaanga. Kaanga kwa dakika 3 kisha geuza upande wa pili uweze pata rangi ya kahawia nzuri.
 
Baada ya kugeuza upande wa pili huu ndio muonekano wake na kisha pika pia kwa dakika 3 na kifua cha kuku kitakua kimeiva. Kumbuka unapogeuza upande wa pili toa na mfuniko usifunike tena.

Huu ni muonekano wa perfectly cooked and seasoned chicken breast baada ya kukata ndani inakua laini na ladha safi kabisa sio kau kau na kupoteza ladha.


KIfua hiki cha kuku mimi na familia yangu tulikula na mchanganyiko wa parachici, slice za vitunguu, slice za nyanya mbivu limao na giligilani mhhhhhh safi sana.
 
NDANI YA DAKIKA 10 CHAKULA TAYARI
 

JIFUNZE RECIPE ZA CHAPATI, MAANDAZI NA SAMOSA

HABARI WAPENZI WA BLOG HII YA CHAKULA BORA NA SALAMA
KWA WALE WOTE WASOMAJI WAPYA MTAKUA MMEPITWA NA MAFUNZO MAZURI NA KIPENZI CHA WATU WENGI YANAYOELEZEA UPISHI WA VYAKULA NILIVYOTAJA HAPO CHINI. JARIBU KU CLICK HIZO LINK NA UTAFUNGUKA MOJA KWA MOJA UKURASA WENYE MAFUNZO HAYO KAMA INAVYOELEKEZA HAPO CHINI.


PIA KWA WALE WANAOPENDA KUPIKA CHAPATI NA NYAMA YA MBUZI UNAWEZA CLICK LINK HII HAPO CHINI


NA WALE WANAOPENDA KUPIKA MAANDAZI YA LADHA YA NAZI NA HIRIKI CLICK LINK HIYO HAPO CHINI KWA MAFUNZO ZAIDI


WAPENZI WA SAMOSA PIA UNAWEZA CLICK LINK HIYO HAPO CHINI NA UTAONA JINSI YA KUANDAA KWA UFASAHA

NAWATAKIA WEEKEND NJEMA
CHEF ISSA

Monday, November 4, 2013

JIFUNZE KUTENGENEZA MTINDI FRESH AU YOGURT

RECIPE SAFI KABISA YA KUTENGENEZA MTINDI FRESH UKIWA NYUMBANI AU HOTELINI KWA URAISHI SALAMA NA HARAKA ZAIDI
MAHITAJI
1 lita ya maziwa mabichi
100 gram mtindi uwe fresh au wa kopo
 
MAMBO YA MSINGI YA KUZINGATIA
Aina ya maziwa.  Aina hizi za maziwa unaweza tumia Goat Milk, Full fat milk, Pasteurized Milk, Homogenized Milk, Raw Milk, 2% Milk, 1% Milk, Fat free] kumbuka aina ya maziwa utakayotumia na matokeo yake yatakuwa tofauti maziwa yakiwa na mafuta kiasi ndio na mtindi wako utakua mzito
 
Thermometer ni lazima?: Sio lazima kabisa kwani bibizetu sikumbuki kama walikua wanatumia kumbuka maziwa hayatakiwi kuwa yamoto yanatakiwa kuwa yavugu vugu weka kwenye kiganja kupima kama tayari yanauvugu vugu kabla ya kuweka mtindi fresh.

Mtindi wangu haujawa bado ni maziwa tatizo nini?  sababi ya kwanza unaweza ukawa umetumia maziwa ya  UHT (Ultra High Temperature) processed milk. ingawa pia unaweza kutengenezea yogurt ikiwa utafata vipimo na maelezo vizuri,  Sabau ya pili unaweza ukawa umetumia mtindi ulioharibika katika kuchanganyia na sababu ya tatu ni kutochemka kwa maziwa kwa joto la 105-110 F temperature au umechanganya mtindi kwenye maziwi yamoto sana au yabaridi sana.
 
JINISI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI
Muda wa maandalizi : Masaa 4 hadi 8
Muda wa mapishi : Dakika 15
Idadi ya walaji : Watu 4


Chemsgha maziwa mabichi kwa nyuzi joto 110F. Ukiyachemsha mziwa katika joto la 110F, bado maziwa yanakua katika ladha ya uhalisia ya ubichi.

Note: sio lazima kutumia maziwa mabichi kwa recipe hii


Note: kama utataumia maziwa ambayo yameshachemshwa basi kumbuka kuyapoza mpaka joto lifikie 110F before the next step.


Nilibakisha yogurt kiasi ndio naitumia tena kama huna unaweza nunu mtindi fresh na ukatumia katika hatua inayofuata baada ya kuchemsha maziwa.

Kisha mwagia mtindi huo ndani ya maziwa .

Stir and whisk it so that it dissolves and is well distributed  throughout.

Funika na mfuniko hakikisha kua joto lilikua ni 105F to 110F . Ili iweze kuganda na kuset haraka unatakiwa uwashe oven kwa dakika mbili kasha Zima halafu weka sufuria yako itachukua masaa 3 hadi 5 kuganda na kuset,kwasehemu zenye joto kama Tanga , Dar es salaam, Zanzibar na mtwara unaweza weka tu pembei ya jiko na baada ya masa 5 ikawa imeganda vizuri kabisa sababu ya hali ya hewa na mgandamizo wa hewa wa juu.
 
See that set yogurt with a yellow layer on top?.

Kwasababu maziwa tuliotumia ni fresh basi cream inakuja juu na nzito kabisa.

 Ukitaka mtindi wako uwe mzito basi chukua kitambaa na chuza maji kisha itabakia cream nzito nasfi kabisa.


Weka katika bakuli na unaweza kuongezea ladha za matunda mfano embe, chungwa, nanasi au ndizi familia au wateja wako wakafurahia sana.
 

Saturday, November 2, 2013

JIFUNZE KUTENGENEZA MCHANGANYIKO WA YAI LA KUKAANGA NA CHEESE

KAA TAYARI KWA KUJIFUNZA JINSI YA KUKAANGA YAI KWA KUCHANGANYA NA CHEESE
 
MAHITAJI
2 pc yai vunja tenga ute mweupe tu
1 pc yai Zima usilitenganishe
2 kijiko kidogo cha chai maji safi
5 gram chumvi
5 gram pili pili manga
60 gram Gruyere Cheese au Cheddar cheese
1 fungu Chives

JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI
Vunja mayai 2 kwenye bakuli safi hakikisha unaweka ute mweupe tu kasha vunja yai moja Zima mwagia katika bakuli ulilitenganishe kasha weka chumvi na pili pili manga. Tumia mchapo kupiga piga ichanganyike

Kisha weka maji safi au unaweza tumia maziwa badala ya maji. Ukitaka yai lako liwe fluffier au spongy basi tumia maji.

Hutakiwi kupiga piga sana maana utasababisha mapovu kama unavyoona kwenye picha hii haitakiwi. pia unaweza kutumia uma kwenye kupiga piga na mchanganyiko wako ukawa safi. Unaweza kuweka hebs ya aina upendayo mfano parsley au korienda au chives

Weka kikaango katika moto kwa muda kiasi ipate moto. Kisha mwagia siagi ukiona imeaanza foaming and sizzling basi moto up safi. Tumia vijiko viwili vidogo vya chai siagi kasha mwagia mchanganyiko wako wa yai kwenye kikaango.

Kumbuka kulivuruga vuruga yai kwa sekunde 6 hadi8 ili liweze kuiva haraka upande wa chini

Kisha lisambaze vizuri na uliache liweze kuiva 
 
Baada ya dakika chahe utaona yai lote mieshakauta ute na kua na muonekano kama kwenye picha Zima jiko.

Mwagia  cheese kwa kufata mstari kati kati ya yai kama muonekano katika picha. Kumbuka usimwagie kwenye yai lote.

Chukua upande wa kwanza funika yai lako kisha chukua upande wa pili na ufunike pia na kupata umbo lionekanalo katika picha.

Ukilikata yai lako baada ya kuiva utaona cheese inamwagika ooooh safi sana. See that cheese oozing out from the middle?
 
    Unaweza ongeza ladha ya yai kwa kuweka vilivyotajwa hapo chini 
Crumbled Goat Cheese, sautéed shallots and fresh(or dried) thyme
Grated Emmentaler, sautéed Mushrooms and Spinach
Caramelized Onions, Crisped cubed Tempeh and fresh Marjoram
Grated Gouda and lightly stir fried thinly sliced (on the diagonal) Asparagus
 
Maji: Sio lazima kutumia maji unaweza tumia maziwa na utumiaji maziwa unasababisha creamier texture wakati ukitumia maji inasaidia  fluffiness kwenye yai.