CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Tuesday, December 30, 2014

CHEF ISSA AFANYA MAAJABU KWENYE KOMBE LA DUNIA LA MAPISHI 2014 NCHINI LUXEMBORG

K
 Executive Chef Issa Kipande  tunayemfahamu kama Chef Issa (aliyeshika kombe) wiki hii amefanya makubwa kwa kuwa mmoja wa ma-Chef  wa timu ya Stockholm, Sweden, kushiriki na hatimaye kushika nafasi ya kwanza katika kipengele cha timu za kanda kwenye mashindano ya Kombe la Dunia la Mapishi  2014 yajulikanayo kama  Villeroy & Boch Culinary World Cup 2014  yaliyofanyika nchini Luxemborg. Mshindi wa jumla alikuwa Singapore.

Kushinda kombe la dunia si mchezo katika tasnia yoyote ile nasi hatuna budi kumpongeza Chef Issa kwa kuwakilisha vyema Watanzania na Waafrika kwa jumla.
 Mtanzania huyu anayefanya kazi huko Sweden na Mtwara kuliko na hoteli yake aliyoifungua hivi karibuni, ameshiriki katika mashindano hayo makubwa yanayofanyika kila baada ya miaka minne na yaliyoshirikisha ma-Chef zaidi ya 3000 kutoka nchi 56 za mabara yote matano ya dunia.

Mpaka sasa Chef Issa Kapande mbali ya kushinda tuzo nyingi tofauti katika fani yake ya upishi pia anashikilia rekodi ya kuwa Chef Mtanzania Msomi na mdogo kuliko wote aliyewahi kufungua na kuongoza hotel ya nyota tano  akiwa Internationally  Certified Executive Chef  akiwa na umri wa miaka 25 tu. Hili ni jambo la kujivunia sana.
Chef Issa anasema kuwa Mola ajaliapo anatamani sana mwaka 2018 aipeleke Timu ya Taifa ya Tanzania mashindano haya. "Na nina imani tutafanya vizuri tu kwani kuna wapishi wazuri sana nyumbani Tanzania ingawa wamekosa nafasi au muongozo wa kuweza kuonyesha uwezo wao. Mungu ibariki Tanzania", anasema.
 Executive Chef Issa Kipande  tunayemfahamu kama Chef Issa (aliyeshika kombe) akiwa na  timu yake ya  Stockholm, Sweden,
Switzerland 
 Executive Chef Issa Kipande alipoitwa mbele kwenda kupokea tuzo akiwa mtu  mweusi peke yake
 Executive Chef Issa alipata heshima kubwa sana ya kuhudhuria executive lunch kwa watu maalumu tu iliofanyika  wakati wa kutoa kombe la dunia kushoto ni Raisi wa mashindano hayo na kulia ni mtoto wa mfalme wa nchi ya Luxembourg Crown Prince Guillaum
Executive Chef Issa akiwa na Raisi wa chama cha ma-chef dunia nzima 
Bw. Gissur Gudmundsson. 

Friday, November 7, 2014

JIFUNZE KUTENGENEZA VITAFUNWA HIVI VYA AINA TATU KWA WAKATI MMOJA

 
KAA TAYARI KWA RECIPE SAFI KABISA YA VITAFUNWA HIVI VITATU KWA WAKATI MMOJA INAPENDEZA SANA KWA CHAI YA SAA KUMI JIONI AU SAA NNE ASUBUHI
 
MAHITAJI
 
JINSI YA KUANDAA FATA MAELEZO NA PICHA HAPO CHINI
 













 
 


Saturday, October 25, 2014

JIFUNZE KUTENGENEZA BISIKUTI ZENYE MCHANGANYIKO WA KARANGA YA KUSAGA

 
JIFUNZE KUTENGENEZA BISIKUTI ZENYE MCHANGANYIKO WA KARANGA YA KUSAGA NA MAYAI
 
MAHITAJAI
8 kijiko kikubwa cha chakula butter au siagi
120 gram karanga ya kusagwa ilainike
180 gram sukari ya kahawia
2 kijiko kikubwa cha chakula asali
1 yai la kuku ( kama hutumii mayai weka 2 vijiko vya vegetable oil)
1 kijiko kidogo cha chai vanilla essence
360 gram unga wa ngano
1 kijiko kidogo cha chai baking soda
120 gram karanga za kumenywa zilizokaangwa
 
JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI
 
 

 
 









 
 


Wednesday, October 15, 2014

JIFUNZE KUPIKA KITUMBUA CHENYE MCHANGANYIKO WA UNGA WA NGANO NA UNGA WA MCHELE

 RECIPE SAFI KABISA YA KUPIKA KITAFUNWA AINA YA KITUMBUA KWA MCHANGANYIKO WA UNGA WA MCHELE NA UNGA WA NGANO OOOHH LADHA SAFI SANAA
 
MAHITAJI
250 gram unga wa ngano
120 gram unga wa mchele
1kijiko kidogo cha chai hiliki ya unga au unaweza saga mbegu ikawa chenga chenga
120 gram sukari
120 gram maji ya vugu vugu
nusu kijiko kidogo cha chai amira ya chenga
 
JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI
 
 
Chukua maji ya vugu vugu changanya na amira ya chenga, sukari pamoja na hiliki.

 
Chukua unga wa ngano na unga wa mchele changanya pamoja

 
Chukua mchanganyiko wa maji mimina kwenye mchanganyiko wa unga wa ngano na mchele na kisha tumia mwiko kukoroga pole pole mapaka ichanganyike vizuri. 

 
Kama mchanganyiko wako ni mwepesi sana basi unaweza tumia mayai au ukaongeza maji au maziwa kiasi hakikisha mchanganyiko huu usiwe mwepesi kabisa na usiwe mzito sana ubora uwe kama unavyoona kwenye picha hapo juu.

 
Chukua kikaango cha vitumbua kisha weka mafuta ya kupikia kijiko kimoja kidogo cha chai.
 

 
Mafuta yakisha pata moto mimina mchanganyiko wako wa unga wa mchele kwenye kikaango.
 

 
Ukishaona rangi ya kahawa kwa chini basi geuza upande wawili na weka mafuta tena. mpatie mlaji chakual kikiwa cha moto atafurahi sana. 

 
 
HUU NI MUONEKANO SAFI KABIS AWA KITUMBUA HIKI CHENYE MCHANGANYIKO WA UNGA WA AINA MBILI SAFI SANA KWA KITAFUNWA CHA NYUMBANI NA RESTAURANT PIA. 
 


Saturday, September 27, 2014

JIFUNZE KUPIKA SUPU YA MAHARAGE AINA YA PINTO PAMOJA NA VIAZI ULAYA

 
JIFUNZE KUPIKA SUPU SAFI SANA YA MCHANGANYIKO WA VIAZI ULAYA NA MAHARAGE AINA YA PINTO
 
MAHITAJI
120 gram pinto beans au maharage ya kitenge
1 kitunguu maji kikubwa chop chop
2 pc za kitunguu swaumu saga
1 kiazi ulaya kikubwa kata kata vipande vidogo
 2 kijiko kikubwa cha chakula tomato paste au nyanya nzima 2
1/4 kijiko kidogo cha chai turmeric powder
1 bay leaf
5 gram chumvi
5 gram pili pili manga
majani ya korienda
 
JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO
 
 
Loweka maharage yako kwa masaa 2 kwenye maji baridi kama utakua unaharaka unaweza kuyapika maharage haya kwenye pressure cooker

 
Baada ya kuyaloweka unaweza kuyapika kwa dakika 20 tu yatakua yameiva na baada ya kuiva hakikisha humwagi maji ya maharage hayo baada ya kuchuja

 
Chukua sufuria na kisha weka katika moto na uweke kijiko kimoja kikubwa cha chakula mafuta ya kupikia, ikisha pata moto weka kitunguu maji, kitunguu swaumu, turmeric powder, bay leaf na pili pili hoho pamoja na chumvi kanga mapaka vilainike na kutoa harufu safi.

 
Kisha ongezea viazi ulaya pika kwa dakika 4 au mpaka vitakapokua laini. Baada ya kulainika viazi ongeza tomato pest na kumbuka kukoroga ili kila kitu kichanganyike.

 
Chukua yale maji yaliyobaki baada kuchemshwa pamoja na maharage weka kwenye mchanganyiko wako wa viazi na mboga majani unaweza ongeneza maji ya kawaida kidogo ili upate supu. Ikisha chemka tu ongezea maharage na pili pili manga acha ichemke dakika mbili itakua imeiva

 
Unapochemsha maharage hakikisha hayaivi yakapondeka kabisa yawe magumu, mpatie mlaji ikiwa bado ni yamoto na pamba kwa juu na majani ya korienda! Yum!

 
Unaweza maatia mlaji kwenye kikombe na bakupi na ukala pamoja na chapatti au makate na ukafurahia kabisa hasa kwa saubuhi au mchana.
 
 


Monday, September 22, 2014

JIFUNZE KUTENGENEZA SUPU SAFI KABISA YA MCHANGANYIKO WA MBOGA MAJANI

 
RECIPE SAFI KABISA YA KUPIKA SUPU YENYE MCHANGANYIKO WA LEEKS, BROCCOLI NA ASPARAGUS SAFI SANA KWA AFYA YA MLAJI
 
MAHITAJI
1 kitunguu kikubwa kichop chop
1 leek, isafishe vizuri kasha kata kata
2 viazi vidogo safika vizuri kasha kata kata na maganda yake bila kumenya
1 lita ya maji au unaweza tumia vegetable stock
1 bay leaf
5 gram chumvi
5 gram pili pili manga
500 gram Asparagus osha kisha kata kata 
500 gram broccoli osha katakata
 
JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI
 
 
Chukua leeks, viazi ulaya, kitunguu maji na bay leaf kisha weka kwenye sufuria lenye maji au vegetable stock na funika chemsha kwa dakika 10.

 
Baada ya dakika 10 kisha weka broccoli na asparagus na uendelee kuchemsha

 
kisha punguza moto uwe wa chini na endelea kuchemsha kwa dakika  10min kumbuka kuweka chumvi na pili pili manga na uonje.

 
Toa kwenye jiko na uache ipoe kiasi baada ya hapo toa bay leaf weka pembeni na mimina mchanganyiko wako kwenye blender na usage.

 
Baada ya kusaga rudishia kwenye sufuria na uendelee kuichemsha kiasi kwa dakika 5 baada ya hapo unaweza mpatia mlaji na kwajuu ukapamba na majani ya giligilani na ukampatia mnywaji akafurahia sana.
 
 


JIFUNZE KUTENGENEZA VIAZI VYA LIMAO NA KITUNGUU SWAUMU

 
RECCIPE SAFI KABISA YA KUPIKA VIAZI ULAYA VYENYE MCHANGANYIKO WA LIMAO NA KITUNGUU SWAUMU
 
MAHITAJI
4 vikubwa viazi ulaya, osha vizuri
3 kijiko kikubwa cha chakula olive oil
2 kijiko kikubwa cha chakula juice ya limao
2 kijiko kikubwa cha chakula majani ya korienda au giligilani
4 kijiko kidogo cha chai kitunguu swaumu kilichosagwa
5 gram chumvi
5 gram pili pili manga
 
JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI

 
Osha vizuri viazi kasha kata vipande vine kwa kiazi kidogo na vipande sita kwa kiazi kikubwa kata kwa urefu kama inavyoonekana kwenye picha, watu wengi huwa menya maganda ya viazi lakini mimi simenyi naacha maganda ili nisipoteze virutubisho au nutrient zilizojaa kwenye ngozi.
 
 
Washa jiko katika moto wa kati kisha weka vijiko viwili vya mafuta yapate moto, mafuta yakishapata moto weka viazi vyako kwenye kikaango

 
Hakikisha viazi vyako vinakua na rangi ya kahawia pande zote na pika kila upande kwa sakika 5 hadi 6 ndio safi.

 
Punguza tena moto uwe wa kati ili usiunguze, kisha funika mfuniko na acha viendelee kuiva ili viwe laini kabisa na safi kwa mlaji.

 
Wakati huo huo chukua bakuli safi kavu na uchanganye mafuta ya olive vijiko viwili , juice ya limao, majani ya corriender au gili gilani, kitunguu swaumu, chumvi na pili pili manga. Hakikisha unachanganya vizuri.

 
Baada ya viazi kuwa laini, chukua ule mchanganyiko wenye mafuta na mwagia kwenye viazi hakikisha unachanganya pole pole bila kuvivunja.

 
Toa mfuniko na kasha endelea kuvipika kwa dakika 3 hadi 4. wakati mzuri ni pale unapomwagia ule mchanganyiko wa mafuta na kitunguu swaumu ooohh ghafla italipuka harufu safi ya kuvutia pia viazi vitakua na ngozi ya kukauka na yakuvutia kama unavyoona kwenye picha.

 
 Unaweza ongezea majani ya giligilani au korienda kwani pia inahusika sana kwenye kuongeza ladha ya viazi hivi
 
 
Viazi hivi ni maarufu sana kwa nyama choma au samaki choma au kuku choma waandalie familia au wateja hotelini kwako na watafurahia sana sana, ni niafuu na rahisi sana kuandaa.