CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Monday, August 13, 2012

JIFUNZE KUTENGENEZA JUISI YA EMBE BICHI

JIFUNZE KUTENGENEZA KINYWAJI HIKI SAFI SANA CHENYE VIUNGO KWA KUTUMIA EMBE BICHI LA KUCHOMA

MAHITAJI


350 grams Embe la kijani, lioshe vizuri
5 pc ice cubes , Mapande ya barafu
1 lita maji safi baridi
 2 kijiko kidogo cha chai Cumin Powder
2 kijiko kidogo cha chai chumvi
1/4 kijiko kidogo cha chai pili pili manga
2 kijiko kidogo cha chai Sukari
majani fresh ya Mint kwa kupambia 

JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI

Muda wa maandalizi : Dakika 15

Muda wa mapishi : Dakika 15
Idadi ya walaji : Watu 2

Kuna njia 3 za kuandaa juisi hiib ya embe.


 1. Chemsha embe kisha liache lipoe na utoe ngozi ya juu. KIsha toa nyama yote na saga katika mashine kuanzai hapo unafata maelezo kama picha zinavyoonyesha kuanzia step ya saba.

 2. Chukua embe kisha lioshe na umenye katakata na weka katika preasure cooker kwa dakika kumi .Kisha cha lipoe na endelea na maelezo kama picha inavyoonyesha Step ya 7.


Asili ya juisi hii ni kutoka india na kinamama walikua wanachoma maembe kwa mkaa wakiamini hii ndio njia pekee ya kufanya juisi iwe tamu zaidi, Kwasasa technologia imekua unaweza rost embe lako kwa kutumia Oven au gas burner kama inavyoonekana katika picha. Hii ndio njia ya tatu ambayo ninaionyesha leo na juisi inakua na ladha safi sana ya moshi chukua embe lako na weka juu ya gas burner


 

Hakikisha unachoma pande zote mpaka ngozi inakua nyeusi


Kisha weka pembeni lipoe.


Kisha menya ile ngozi yote ya juu.


Kisha toa nyama yote bakisha kokwa tu na nyama weka katika blenda.


Saga iwe laini kabisa.


Kisha chukua ice cubes na weka katika kikombe kikubwa



Kisha chukua lile rojo la embe ulilosaga na weka kwenye vipande vya barafu.



Kisha weka cumin powder, pili pili manga, majani ya minti kidogo na sukari hakikisha unaweka kidogo kidogo mpaka upate ladha halisi unayoipenda wewe.



Kisha ongezea kiasi cha maji na na ukoroge angalia kiasi ya uzito unachopendelea wewe.



Kisha pambia na majani ya mint kwa juu kuongeza harufu nzuri na pia katika juisi yako weka vipande vya barafu zaidi wakati unamapatia mnywaji ili kinywaji hiki kiendelee kua baridi .


Kinywaji hiki anaweza kunywa mtu yeyote yule na kinaongeza sana hamu ya kula hasa kama mtu yeyote yule anaumwa au amepoteza hamu ya kula. Waaandalia familia yako wafurahie. 

Saturday, August 4, 2012

JIFUNZE JINSI YA KUTENGENEZA JUISI YA MCHANGANYIKO WA MATUNDA


KAMA WEWE NI MVIVU KUNYWA MAJI BASI ANZA KUJIFUNZA KWA KUNYWA KINYWAJI HIKI KILICHOKAMILIKA KISHA POLE POLE UTAANZA KUYAPENDA MAJI

MAHITAJI

450 grams Nanasi
 50 grams Tangawizi fresh osha vizuri menya
1 Carrot, chop chop
Ice cubes
 
JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAFUNZO HAPO CHINI

Muda wa maandalizi : Dakika 15 
Muda wa mapishi : Dakika 15
Idadi ya wanywaji : watu 2


Tunda la nanasi na carrot vinachangia sana sukari yote ambayo uisi inatakiwa iwenayo. Tangawizi inaweka uwiano sawa wa ladha kati ya nanasi na karoti. Kama sio mpenzi wa Tangawizi sio lazima kuitumia, pia kama ni mpenzi wa nanasi au karoti unaweza zidisha kimoja wapo ili upate ladha halisi ya unachokipenda.

Tangawizi: Inategemea na ubora wa tangawizi, unaweza kuhitaji nyingi zaidi au wastani chamsingi uweze pata harufu mwanana katika juisi yako {aroma}.

Thursday, August 2, 2012

NAFASI YA KAZI


HABARI YA SIKU WAPOENZI WA BLOG HII YA CHAKULA BORA NA SALAMA.
RAFIKI YANGU ANATANGAZA NAFASI YA KAZI KWA CHEF ANAEWEZA KUPIKA CONTINENTAL CUISIN MSHAHARA MZURI TUNA CV NA BARUA YA MAOMBI KWA EMAIL HII active.chef@yahoo.com, MAHALI NI MTWARA JIKO LINAVIFAA VYA KISASA SANA, MWISHO WA MAOMBI NI TAREHE 25/8/2012

NAWATAKIA SIKU NJEMA.

CHEF ISSA