CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Saturday, November 27, 2010

JIFUNZE KUTENGENEZA WALI NA NYAMA PAMOJA NA YAI LA KUKAANGA


WALI HUU UNAWEZA KUPIKA KWA KUTUMIA AINA TOFAUTI ZA NYAMA MFANO NYAMA YA KUKU, NG'OMBE, MBUZI, KONDOO, SAMAKI KAMBA MAPISHI YA NYAMA ZOTE MTINDOO NI HUU HUU.


MAHITAJI

1 kikubwa Kitunguu
1 fungu Spinach
5 gram Chumvi
1 kg Wali ulioiva
5 Mayai
1 fungu majani ya korienda
1 kg nyama ( mbuzi au kuku au samaki kamba au ng'ombe)
2 kijiko kikubwa cha chakula Mafuta ya kupikia
1 kijiko kikubwa cha chakula Soya sauce
1 kijiko kikubwa cha chakula Oyster sauce
1 kijiko kikubwa cha chakula Hp sauce
1 kijiko kikubwa cha chakula Tomato sauce
1 fungu la Spring onion
10 gram Kitunguu swaumu cha kusagwa
10 gram Tangawizi yakusagwa


JISI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO CHINI



Kwanza kabisa unaanza kuandaa marination ili isaidie kuweka ladha safi katika nyama na kuifanya iwe laini, changanya katika bakuli Soya sauce, HP sauce, Tomato sauce, Oyster sauce, 5 gram kitunguu swaumu, 5 gram tangawizi, 1 kijiko kikubwa cha chakula mafuta ya kupikia na majani ya korienda



Kisha kata kata nyama na weka katika huo mchanganyiko wako iache katika friji kwa muda wa masaa 2 itakua tayari.



Kisha kata kata kitunguu na weka kijiko kimoja cha mafuta yakupikia katika kikaango na kaanga kwa dakika 1 tu


Kisha chukua mchanganyiko ule wa nyama na weka katika kikaango chenye vitunguu na uendelee kukaanga katika moto wa wastani kwa dakika 10 hadi 15 nyama yako itakua imeiva.



Chukua wali uliokwisha iva kisha weka katika sahani kama inavyoonekana katika picha



Juu ya wali weka spinach iliyokaangwa au iliyochemshwa hakikisha unasambaza vizuri juu ya wali wako



Kisha unaweka juu yake mchangayiko wa ile nyama yako saafi na tamu kuliko zoooote hahahahahahahaaaaaaaa!!!!




Mwisho kabisa unakaanga yai jicho la ng'ombe au "fried egg sun side up " kisha unaliweka juu ya nyama katika sahani kama muonekano wa picha hap juu.

FURAHIA NA FAMILIA YAKO MAPISHI HAYA MAARUFU SANA NCHI ZA MASHARIKI YA MBALI NI RAHISI KUENGENEZA HALICHUKUI MUDA MREFU NA NINAFUU KWA GHARAMA.



Friday, November 19, 2010

JIFUNZE KUTENGENEZA KIAZI CHA BINZALI NYEMBAMBA ( CUMIN au JEERA)


 RECIPE SAFI KABISA YA KIAZI HIKI KWA MATUMIZI YA NYAMA CHOMA


MAHITAJI

500 gram viazi vidogo vidogo osha vizuri na usivimenye
1 kijiko kikubwa binzali nyembamba (cumin seeds)
1 kijiko kidogo cha chai unga wa pili pili (chilli powder sio lazima)
1 kijiko kikubwa cha chakula unga wa giligilani (coriander powder)
1 kijiko kidogo cha chai mchanganyiko wa tangawizi na kitunguu swaumu (ginger-garlic paste)
1kitunguu kikubwa katakata
1/2 kijiko kidogo cha chai ungwa wa turmeric
5 gram za chumvi

JINSI YA KUANDAA FATILIA MAFUNZO HAPO CHINI



Chemsha viazi mpaka viive wastani. Hakikisha haviivi vikapondeka


Katika kikaango weka mafuta yakupikia yachemke, kisha kaanga mbegu za binzali nyembamba (cumin seeds) zikishabadilika na kua na rangi ya kahawia na harufu safi ongeza kitunguu maji na a ginger-garlic paste pamoja na chumvi kaaanga mapaka vilainike.



Kisha weka unga wa tumeric, unga wa giligilani na unag wa pili pili. kumbuka kuweka kijiko kimoja kikubwa cha maji ili viungo visiungulie katika chombo unachopikia.



Kaanga kwa dakika 2 mchanganyiko wako utakua umekauka kabisa.



Kisha ongeza moto uwemkali kabisa na weka viazi vyako vya kuchemshwa na kaanga kwa dakika 5. Kama una muda wa kutosha na hauna njaa sana acha moto mdogo na kaanga viazi vyako kwa dakika 2 hadi 3 mapak vianze kupata rangi ya kahawia kwa chini.




Hakiksiha unapopika dakika mbili kabla ya kuzima jiko lako katakata majani ya giligilani na rushia kwa juu kaanga kisha toa viazi katika jiko.


Huu ni muonekano wa viazi vikiwa vimeshaiva





WEKAKATIKA SAHANI SAFI NA WAPATIE FAMILIA YAKO WAFURAHIE KIAZI HIKI CHENYE LADHA SAFI SANA UNAWEKA KULA NA CHAPATI AU NYAMA CHOMA NA UTAFURAHIA SIKU YAKO.

UNAWEZA MENYA MAGANDA YA KIAZI BAADA YA KUCHEMSHA NA BADO UKAFURAHIA SANA CHAKULA CHAKO NA WENGI WETU TUMEZOEA KUMENYA VIAZI. USIPOMENYA MAGANDA YA KIAZI UNAKUA UMELINDA LADHA HALISI NA HARUFU NZURI YA KIAZI


JIFUNZE KUTENGENEZA MCHANGANYIKO SAFI WA KIAZI NA BILINGANYA


 RECIPESAFI KABISAYA MCHANGANYIKO WA CHAKULA HIKI CHA MBOGA MAJANI

MAHITAJI

 250 gram kiazi mabatata ( kiazi ulaya)
250 grams bilinganya ( egg plant)
1 kitunguu maji katakata
1 kijiko kidogo cha chai mbegu za cumin (cumin seeds)
1-kijiko cha pili pili ya unga (chilli powder)
1/2 Tangawizi mbichi menya na isage
2 kijiko kidogo cha chai coriander powder
1/2 kijiko kidogo cha chai unga wa manjano (turmeric powder)
1/2 kijiko kidogo cha chai garam masala
1 fungu la majani ya giligilani kwa kupambia na harufu safi
1 kijiko cha chai maji ya limao kuongeza ladha
5 gram chumvi


JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI



Chukua bilinganya zako kisha kata kata amaumbo madogo na hakikisha unaweka katika bakuli yenye maji ili kusaidia zisiaharibike rangi yake nzuri. 



Weka mafuta ya kupikia ili yapate moto katika kikaango. yakishapata moto weka cumin seeds, Kisha pili pili, tangawizi , na vitunguu maji endelea kukaanga.



Vitunguu vikilainika, Weka viazi mbatata, chumvi na turmeric powder. kisha mwagia kijiko kimoja cha maji ili kufanya unga wa manjano usiungulie katika kikaango.



Kisha ongezea bilinganya na  unga wa giligilani (coriander powder) na garam masala koroga ichanganyike vizuri


  
 Funika mfuniko wa sufuria au kikaango chako na acha kwa dakika 8 mpaka 10 hakikisha bilinganya inaiva vizuri.



Baada ya chakula chako kuiva katakata majai ya giligilina na pamba kwa juu husaidia kuleta harufu nzuri na kuongeza ladha ya chakula




Chakula hiki unaweza kula na ugali, wali au chapati pamoja na mtindi safi kabisa na ukafurahia sana sana.


JIFUNZE KUTENGENEZA MKATE AINA YA NAAN


WATU WENGI MMEKUA MKIULA MKATE HUU KATIKA RESTAURANT ZA KIHINDI NA UKIMUOMBA AKUFUNDISHE HAWEZI KUKUBALI MAANA HUTAKWENDA TENA KUNUNUA KWAKE LEO NAKUFUNDISHA RECIPE SAFI KABISA YA MKATE HUU MTAMU SANA KWAJILI YA KULIA MBOGA ZA NYAMA AU MBOGA MAJANI.

MAHITAJI

720 gram unga wa ngano
1 kijiko kidogo cha chai amira ya chenga (Active dry yeast)
180 gram ya maji ya uvugu vugu
5 gram chumvi
1/2 kijiko kidogo cha chai sukari
1 fungu la majani ya gili gilani ( Corriender chopped)
1-1/2 siagi kijiko kikubwa cha chakula (butter)

JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA  NA MAELEZO HAPO CHINI



Changanya katika bakuli amira ya chenga, maji ya uvugu vugu na sukari kisha koroga hakikisha mpaka amira inayeyuka kabisa kisha weka pemebeni kwa dakika 5


Kisha weka unga wa ngano, chumvi, majani ya gili gilani kisha changanya vizuri.


Tengeneza shimo kati kati kisha mwagia yale maji yenye mchanganyiko wa amira na uanze kukandaKanda vizuri unga wako na hakikisha umeshikana safi na ni laini.


.Baada ya kukanda safi kabisa hakikisha bakuli lako unafunika na taulo maalumu ya jikoni au nailoni kisha weka sehemu yenye joto la kutosha na acha iumuke mpaka ije katika bakuli lako kwa muda wa masaa2 au 3 tu. Hii inategemea na upo nchi gani na majira gani ya hewa.


Baada ya hapo toa mchanganyiko wako wa unga anza kuukanda tena kwa dakika 5 tu kisha gawanisha katika maumbo madogo.



Mwagia unga kidogo juu ya meza kusaidia isishike na anza kusukuma kwa kutumia mpini iwe wa mbao au wa chuma.


Hakikisha unaposukuma usitengeneze umbo la mduara tengeneza umbo la urefu. Kisha washa oven yako kwa moto wa kati ( Njia hii unatumia kama huna jiko la Tandoor) kisha chukua mkate wako wa Naan weka katika (baking sheet) chombo cha kuokea, paka juu ya mkate naan siagi kiasi na kisha weka katika oven. Ukisahona tu unaanza kubadilika rangi toa geuza na paka tena siagi upande wa pili.


Ukiona muonekano huu basi ujue upande wa chini tayari umeiva hapa ndio unatakiwa sasa kugeuza na kupaka siagi upande wa pili kisah rudisha katika oven.



Huu ni muonekano wa upande wa kwanza ulivyoiva hakikisha unapaka siagi safi kabisa ya kutosha na jina halisi la kate huu ni butter Naan kwakua unapata ladha safi toka katika siagi.



BAADA YA KUPIKA PANDE ZOTE MBILI NA UKAPATA RANGI SAFI KABISA YA KAHAWIA BILA KUUNGUZA MAKATE WAKO HAKIKISHA UNAMPATIA MALAJI HARAKA BADO UKIWA WAMOTO ATAFURAHIA SANA NA UNAWEZA KULA NA MCHUZI AU SUPU AU MBOGA YEYOTE ILE IWE YA MAJANI AU NYAMA.

FURAHIA NA FAMILIA YAKO.



Sunday, November 7, 2010

JIFUNZE KUCHONGA MBOGA NA MATUNDA SOON UTAPATA SHULE



KAA TAYARI KWA MAFUNZO HAYA YA UCHONGAJI WA MBOGA NA MATUNDA











JIFUNZE KUPIKA NJUGU MAWE KWA LADHA YA HALI YA JUU


MUONEKANO WA NJUGU MAWE HIZI NI KIVUTIO KIKUBWA SANA NA LADHA YAKE NI SAFI SANA 


MAHITAJI

360 gram njugumawe / Loweka usiku kucha
1 Kitunguu maji kikubwa,chop chop
5 gram kitunguu swaumu
5 gram tangawizi ya kusagwa
1/2 kijiko kidogo cha chai mbegu za binzali nyembamba
1 kijiko kidogo cha chai garam masala
1/4 kijiko kidogo cha chai unga wa manjano (turmeric powder)
1kijiko kidogo cha cha pilipili ya unga (chilli powder / sio lazima)
3 nyanya kubwa za kuiva , chop chop
1/2 kijiko kidogo cha chi sukari
10 gram chumvi
1 kikombe kikubwa cha chi maji safi na salama
majani ya coriander kwajili ya kupambiana kuleta harufu nzuri


MAELEZO NA JISNI YA KUPIKA FATILIA PICHA HAPO CHINI



Weka mafuta katika kikaango yapate moto kisha weka viungo vyote vya mbegu kaanga na ukishapata aharufu safi weka vitunguu maji, kitunguu swaumu na tangawizi kisha endelea kukaanga.


Vitunguu vikishalainika, Ongeza njugu mawe. KIsha weka unga wa pili pili na unga wa turmeric 



Kaanga kwa dakika 1 kisha ongeza nyanya ulizomenaya na kukatakata pamoja na  garam masala, sukari na chumvi pamoja na maji kikombe kimoja kikubwa.


Acha ichemke na funika sufuria yako kwa dakika 20 hadi 30 mpaka anjugu ziwe laini.


Hakikishs njugu mawe zinabaki na umbo lake zuri na haziharibiki kwa kupondeka pondeka. Kama unapenda zipondeke basi endelea kupika kwa muda mrefu :)


Baada ya hapo njugu zako zitakua zimeiva na tayari kwa mlaji kufaidi kata kata kajain ya korienda na pamba kwa juu yataleta harufu safi na ladha nzuri katika njugu zako.





 Aina hii ya upishi ni rahisi sana na wengi wenu tumeizoea kikubwa hakikisha viungo vinaungua katika moto na kuiva ili visikusababishie kiungulia.

Kwa kuongezea utamu wa njugu hizi unaweza ongezea tui la nazi baada ya njugu kuiva weka ichemke kwa dakika 2 tu kisha itakua tayari kwa kuliwa, lakini kama unaogopa kupta cholesterol, usitumie kabisa nazi acha vile vile ulivyokua umeshapika mwanzo. Pika kwa familia yako wafurahie :)



JIFUNZE KUTENGENEZA CHAKULA HIKI MCHANGANYIKO WA NJEGERE NA VIAZI MABATATA

MCHANGANYIKO HUU WA VIAZI MBATATA NA NJEGERE NI SAFI SANA KWA LADHA NA AFYA YA MLAJI PIA CHAKULA HIKI NI KIZITO NA KINA KAA SANA TUMBONI NA NI RAHISI KUANDAA.

MAHITAJI

1 Kitunguu maji kikubwa katakata
2 nyanya kubwa, chop chop
2 Kiazi mviringo au mbatata (Unaweza kumenya ua ukaosha vizuri na ukakata kata kikiwa na maganda yote sawa maganda yana saidia kupoata harufu na ladha halisi ya kiazi)
240 gram za njegere
5 gram za kitunguu swaumu
5 grama za tangawizi ya kusaga
1/2 kijiko kidogo cha chai unga wa mdalasini
2 pili pili mbichi
1/2 kijiko kidogo cha chi unga wa binzali (turmeric powder)
1/2 kijiko kidogo cha chai cumin powder
10 gram chumvi
1 fungu dogo la majani ya gili gilani kwa kupambia na kuleta ladha safi.
2 kijiko kikubwa cha chakula mafuta ya kupikia au siagi au samli.



JINSI YA KUANDAA FATILIA MAELEZO NA PICHA HAPO CHINI



Weka mafuta katika kikaango kisha weka vitunguu. Kaanga kwa dakika 1 , Kisha weka kitunguu swaumu na tangawizi ya kusagwa  , Pili pili (Kama unatumia sio lazima) endelea kukaanga mpaka vitunguu vilainike na kuiva.


KIsha weka viungo vyoote na kaanga kwa dakika 2 hadi3 viuobgo viive na kuondoa ukali utakaosababisha kiungulia kama havitaiva vizuri.



Kisha weka viazi vyako na kaanga kwa dakia 3mara nyingi mimi huwa sipendi kutoa ngozi ya kiazi ili kuoata ladha halisi ya kiazi.



Kisha weka nyanya, Kaanga kwa dakika moja na kisha weka 240 gram za maji safi sana salama funika na mfuniko acha ichemke kwa dakika 5.


Kisha weka njegere na pika mpaka maji yakauke na viazi vilainike na kuiva kabisa.


Kama unavyoona katika picha chakula chao kimeiva na mchuzi umekauka kabisa viazi na njegere zimeiva kabisa mwisho kata kata corrienda na pamba kwa juu.


Huu ndio muonekano halisi wa chakula chako na unaweza kula na ugali, chapati au wali na familia au mlaji yeyote yule akafurahia sana sana.