CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Thursday, December 26, 2013

JIFUNZE KUTENGENEZA KITAFUNWA HIKI CHA KARANGA NA CHOCOLATE


 RECIPE SAFI KABISA YA KITAFUNWA HIKI CHA KARANGA NA CHOCOLATE
 
MAHITAJI
360 gram peanut butter
1 kg high quality chocolate chips, milk chocolate nzuri kwa family

 360 gram sukari ya unga ( icing sugar)
 6 kijiko kikubwa cha chakula siagi iliyoyeyushwa
Cooking Spray
Mini Cupcake Papers
JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI

 
Haya ni maandalizi ya vitu vyote unavyohitaji kwakutengeneza kitafunwa hiki
 

 
Yeyusha siagi kwenye microwave. Kisha chukua peanut butter weka kwenye bakuli safi na kisha changanya na icing sugar pamoja na vijiko 4 vya siagi liyoyeyushwa. ukiona bado ni kavu sana ongeza vijiko viwili vilivyobakia. endelea kukoroaga upate mchanganyiko laini.
 

 
Yeyusha chocolate kwenye microwavehakikisha unaikoroga koroga mara kwa mara mpaka itakapo yeyuka nikiwa na maana weka dakika 1 toa koroga kisha rudihs kwenye microwave kwa dakika 1 toa koroga mpaka iyeyuke na kua laini safi kabisa.

 
Panga hizo cupcake papers kwenye tray ya kuokea baking sheet paka mafut ya siagi hizo cupcake zote mimi huw anatumia spray special. Chukua chocolate iliyoyeyuka kisha mimina kijiko kimoja tu kwenye cupcake papers, hakikisha imeenea vizuri kwa chini. tumia kidole chako kuisambaza vizuri na uhakikishe imeshika saf kabisa. fanya hivyo kwa cupcake zote na hakikisha mchanganyiko wa chocolate umebaki pembeni kwajili ya matumizi mengine.
 
 
Baada ya kumaliza oezi hili, chukua trayweka kwenye friji poe kwa dakika 5 hadi 10
 

 
baada y dakika 5 hadi kumi utapata muonekano huu na chocolate itakua imeganda

 
Chukua piping bag au mfuko wa nailoni na kisha tumia glasi kwa kukusaidia kumiminia mchanganyiko wao wa peanut butter kwa urahisi tumbukiza mfuko wako ndni ya glasi na kisha anza kumimina mchanganyiko wa peanut butter


 
kisha anza ku Pipe au unaweza kutumia kijiko kuweka mchanganyiko wa peanut butter kwenye chocolate cupszilizotoka katika friji.Tumia piping bag ni nafuu na haraka zaidi!

 
Huu ndio muonekano baada ya kuweka peanut butter katika chocolate cupcakes
 
 
Tumbukiza kijiko chako kwenye maji na kisha kandamiza moja baada ya nyingine kutengeneza umbo zuri. Chukua chocolate iliyobakia iliyokwisha yeyushwa na mimina juu ya peanut butter na urudishie tray kwenye friji kwa dakika 30 iweze kuset completely. Recipe nzima inaweza kutoa vipande 55 mini peanut butter cups.

 
Baada a dakika 30 itakua imeset safi kabisa na tayari kuliwa
 

 
Ukitoa kwenye cup cakes utapata muonekano huu safi saaafi sanaaaaa
 

 
Ukiuma na kuikata katikati utapata muonekano huu na ladha safi sana ya hali ya juu mchanganyiko wa peanut butter na chocolate.


Unaweza ongezea urembo juu yake............….lakini......….from the bottom of my heart….I have to say….these are D E L I C I O U S ! ! ! !  The peanut butter filling is soooooooo creamy and each splendid little bite is the perfect ratio of chocolate to peanut butter.
Hopefully that wasn’t too hard watengenezee watoto nyumbani na watu wazima watafurahia candy hii ya aina yake.

ENJOY!

 

Sunday, December 8, 2013

JIFUNZE KUAMSHA LADHA KWENYE WALI ULIOPIKWA NA UKALALA

KAA TAYARI KWA RECIPE SAFI KABISA YA KUAMSHA LADHA KWENYE WALI ULIOPIKWA KISHA UKALALA ( KIPORO)
 
MAHITAJI
700 gram za wali uliolala ( Kiporo)
2pc kitunguu maji kikubwa
5 pc nyanya za kuiva
1 kijiko kidogo cha chai dengu
1/4 kijiko kidogo cha chai pili pili manga
1/4 kijiko kidogo cha chai Turmeric powder
kijiko kidogo cha chai Sambar Powder, 
1 pili pili moja kavu (siolazima)
kijiko kidogo cha chai mafuta ya kupikia
kijiko kidogo cha chai siagi
Majani ya Curry kiasi
majani ya giligilani kiasi
 
KUJIFUNZA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI
 
 
Chukua vitunguu maji 2 vikubwa kwani mimi napenda sana ladha ya kitunguu hivyo unaweza tumia hata kimoja kasha kata kata fine kabisa.

 
Weka mafuta katika kikaango yapate moto kasha tupia pili pili
 
 
KIsha weka kijiko cha dengu.

 
Endelea kukoroga hakikisha dengu hazi ungui la zinabadilika rangi kiasi kuwa kahawia.

 
Kisha weka vitunguu maji na chumvi na uendelee kukoroga kwa dakika 2 mpaka 3.

 
Wakati kitunguu kinaendela kuiva, Kata kata nyanya katika vipande vidogo vidogo. Mimi pianapenda sna ladha ya nyanya hivyo nilitumia pc 5 wewe unaweza tumia sawa au ukapunguza kua 3 au 2 kutokana na unavyopenda.

 
Ongeza moto kwenye jiko kisha mwagia nyanya ulizokwisha kata kata na uendelee kukoroga.

 
Weka turmeric au manjano, endelea kupika kwa moto mwingi mpaka nyanya yako iive iwe soft and mushy.

 
ongezea maji masafi kikombe kidogo kimoja cha chai  , na utupie majni ya curry

 
kisha weka sambar powder na ukoroge ili ichanganyike.

 
punguza moto uwe wa wastani kisha pika kwa dakika 5 mpaka 7 ukiwa umefunika mfuniko.

 
Hatua hii inafanya mchuzi wako uwe safi na wenye ladha. sasa hapo ni ruksa kuonja na ukiona nyanya imeleta ladha ya uchachu kisha ongezea sukari kidogo ili kusawazisha ladha kua ya kawaida. Hakikisha mchuzi wako una ladha safi kwani ndio itabeba ladha yooote ya huo wali.

 
Kisha weka wali uliopikwa au kiporo.  Weka kidogo kidogo hakikisha kuna mchuzi wa kutosha wali usizidi.

 

Hakikisha unakoroga pole pole mpaka wali unachanganyika na kua safi kabisa ila usiwe kavu sana au kua teke teke.

 
Funika mfuniko na pika katika moto wa wastani kwa dakika 5 hapawali utakopa ladha toka kwenye mchuzi na kua safi kabisa

 
Zima jiko kisha weka kijiko kimoja cha samli au siagi.
 
 

Unaweza ula wali huu pamoja na mtindi, pia rushi majani ya giligilani kwa juu kuongeza ladha na harufu nzuri pia unaweza kula na kachumbali au salad pamoja na parachichi au ndizi mbivu.


Saturday, December 7, 2013

JIFUNZE KUTENGENEZA PANCAKE SAFI NA NZITO KWAJILI YA KITAFUNWA

RECIPE SAFI KABISA YA PANCAKE NZITO NA SAFI KWA KITAFUNWA CHA ASUBUHI, MCHANA AU JIONI
 
MAHITAJI
240 gram unga wa ngano
3 kijiko kikubwa cha chakula sukari (white sugar)
1/2 kijiko kidogo cha chai Baking Soda
1/2 kijiko kidogo cha chai Baking Powder
1/2 kijiko kidogo cha chai chumvi
360 gram cups fresh cream
1 pc yai
kijiko kikubwa cha chakula butter  au (Siagi)
kijiko kikubwa cha chakula vanilla 
 
JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI
 
Chukua bakuli safi kavu kasha changanya unga wa ngano, sukari, chumvi, baking powder na baking soda.

Kisha chukua bakuli nyingine safi na kavu kasha changanya pamoja mayai, vanilla essence, siagi na fresh cream kama huna unaweza tumia maziwa badala yake.

Kisha chukua mchanganyiko wa mayai na maziwa mwagia kwenye mchanganyiko wa wa unga na koroga pole pole. Kisha weka pembeni acha kwa dakika 5 hadi 10 sio lazima lakini kama ukiweka kwa muda huo itulie pancake yako itatoka vizuri sana.

Chukua non stick pan, mwagia mafuta kiasi hakikisha jiko lako halina moto mkali au moto mdogo . Medium heat is perfect for pancakes. chukua kijiko kikubwa au upawa mmoja chota na mwagia katika kikaango.

Ukitaka kujua recipe umeipatia au jiko lako linamoto safi basi utaona  holes au bubbles zinatokea kwa juu sasa ujue ndio na muda wa kugeuza umefika igeuze pancake yako. Kawaida inachukua kama 50 sekunde mpaka dakika.

Turn the pancakes when golden brown and let it cook for another few seconds or until done.

Angalia pancake ilivyochambuka safi sana na nzito ukila unashiba

Hapa familia lazima ijiume videle bwana


Tumia kitambaa kizito au towel kuzifunika wakati unaendelea kupika ili zibaki na moto kwani zinapendeza kuliwa zikiwa za moto wakati wa kula unaweza mwagia maple syrup oooooh ladha yake itakua baabkubwa (a must! Dont even think of skipping it) and feel heaven coming down :) Pia unaweza kutumia chocolate sauce au strawberry syrup.