CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Tuesday, July 15, 2014

JIFUNZE MBINU MPYA YA KUPIKA MAPISHI AINA YA CURRY NA MAYAI YA KUCHEMSHA

 
JIFUNZE JINSI YA KUPIKA CURRY KWA MBINU MPYA KWA MAPISHI TOFAUTI
 
MAHITAJI
  • 240 gram mtindi halisi ( yoghurt)
  • 2 kijiko kikubwa cha chakula unga wa dengu
  • 240 gram maji masafi
  • 3/4 kijiko kidogo cha chai Turmeric powder
  • 1 kijiko kidogo cha chai pili pili nyekundu ya unga
  • 5 gram chumvi
  • 1 kijiko kikubwa cha chakula mafuta ya kula
  • 1 kijiko kikubwa cha chakula samli sio lazima kama hupendi tumia siagi
  • 1 kijiko kidogo cha chai  Cumin seeds au jeera
  • 2 vitunguu maji chop chop
  • 3 vipande vya kitunguu swaumu visage 
  • 8 majani ya Curry
  • 8 au 10 mayai ya kuchemsha (Hard Boiled Eggs)
  •  
    JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI
     
     
    Tumia mchapo kwa kupiga mtindi au Yogurt

     
    Mpaka ilainike kabisa kama unavyoona kwenye picha.

     
    Kisha weka kwenye mtindi unga wa dengu, Turmeric, pilipili ya unga nyekundu na chumvi.

     
    Piga piga mpaka ichanganyike vizuri kabisa.

     
    Kisha ongeza maji na endelea kupiga piga mpaka ichanganyike vizuri kabisa 

     
    Baada ya kuchanganyika vizuri weka pembeni uendelee na atua nyingine

     
    Chukua kikaango kisha weka katika jiko lenye moto na umimine mafuta ya kupikia pamoja na samli.  Mafuta yakipata moto weka jeera na ikianza kupasuka ongeza vitunguu maji na kitunguu swaumu.

     
    Hakikisha unakoroga mpaka kitunguu kiwe laini, ongezea majani ya curry na uendelee kupika kwa dakika 2. Punguza moto uwe wa wastani

     
    Endelea kukoroga na pole pole mimina ule mchanganyiko wa mtindi na viungo. Hakikisha ulipunguza moto ili kuhakikisha mtindi hauungulii kwa chini.
     
     
    Wakati inaendelea kuiva, menya mayai na uweke pembeni. mimi nilitumia mayai 10 in this recipe but 8 should be good enough for 4 people normally.

     
    Hakikisha unaendelea kukoroga mara kwa mara. Zoezi hili linachukua muda kwani unatakiwa kua mvumilivu pika kwa dakika 20 mpaka chuzi wako uwe mzito, unaladha ya kuiva na rangi safi ya njano, tastes cooked and looks yellow.

     
    Onja tafadhali uone kama inatakiwa chumvi zaidi. Unaweza ongezea sukari kijiko kimoja kidogo cha chai kubalance test safi  .

     
    koroga vizuri ichanganyike.
     

    Kisha weka mayai na acha ichemke kwa dakika 5.

     
    Mpatie mlaji ikiwa yamoto pamoja rushia kwa juu majani yakijani ya vitunguu maji na giligilani au koriander.  unaweza kula pamoja na wali, mkate au chapati

    
     
     MUONEKANO SAFI KABISA WA CHAKULA HIKI
     
    1. kwa nyama ya ngombe, mbuzi, kondoo, kuku au samaki unatakiwa kuichemsha kwanza iive vizuri kasha una ichanganya kayika mchuzi huu wakati tulioweka mayai na uache ichemke kwa dakika 10 ili nyama ipate ladha ya mchuzi na viungo.
     
    WAANDALIE FAMILAI YAKO WAFURAHIE
     

    2 comments:

    smile said...

    du asante sana kwa mapishi mazuri ..ninaushauri mdogo tu ambao naamini utasaidia ili kuleta tija iliyokusudiwa.
    1.jitahidi utumie lugha moja sahihi mfano kiswahili kuliko kuchanganya lugha mbili kwa wakati mmoja...
    2.zingatia mtiririko wa maelezo huku ukijulisha majina rahisi ya viungo unavyotumia katika kuelewesha vizuri
    3.tumia lugha ya kitaalamu zaidi ya mtaani

    Anonymous said...

    nimeipenda mno