CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Saturday, September 27, 2014

JIFUNZE KUPIKA SUPU YA MAHARAGE AINA YA PINTO PAMOJA NA VIAZI ULAYA

 
JIFUNZE KUPIKA SUPU SAFI SANA YA MCHANGANYIKO WA VIAZI ULAYA NA MAHARAGE AINA YA PINTO
 
MAHITAJI
120 gram pinto beans au maharage ya kitenge
1 kitunguu maji kikubwa chop chop
2 pc za kitunguu swaumu saga
1 kiazi ulaya kikubwa kata kata vipande vidogo
 2 kijiko kikubwa cha chakula tomato paste au nyanya nzima 2
1/4 kijiko kidogo cha chai turmeric powder
1 bay leaf
5 gram chumvi
5 gram pili pili manga
majani ya korienda
 
JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO
 
 
Loweka maharage yako kwa masaa 2 kwenye maji baridi kama utakua unaharaka unaweza kuyapika maharage haya kwenye pressure cooker

 
Baada ya kuyaloweka unaweza kuyapika kwa dakika 20 tu yatakua yameiva na baada ya kuiva hakikisha humwagi maji ya maharage hayo baada ya kuchuja

 
Chukua sufuria na kisha weka katika moto na uweke kijiko kimoja kikubwa cha chakula mafuta ya kupikia, ikisha pata moto weka kitunguu maji, kitunguu swaumu, turmeric powder, bay leaf na pili pili hoho pamoja na chumvi kanga mapaka vilainike na kutoa harufu safi.

 
Kisha ongezea viazi ulaya pika kwa dakika 4 au mpaka vitakapokua laini. Baada ya kulainika viazi ongeza tomato pest na kumbuka kukoroga ili kila kitu kichanganyike.

 
Chukua yale maji yaliyobaki baada kuchemshwa pamoja na maharage weka kwenye mchanganyiko wako wa viazi na mboga majani unaweza ongeneza maji ya kawaida kidogo ili upate supu. Ikisha chemka tu ongezea maharage na pili pili manga acha ichemke dakika mbili itakua imeiva

 
Unapochemsha maharage hakikisha hayaivi yakapondeka kabisa yawe magumu, mpatie mlaji ikiwa bado ni yamoto na pamba kwa juu na majani ya korienda! Yum!

 
Unaweza maatia mlaji kwenye kikombe na bakupi na ukala pamoja na chapatti au makate na ukafurahia kabisa hasa kwa saubuhi au mchana.
 
 


No comments: