CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Thursday, April 8, 2010

EGG AND POTATO GNOCCHI

Classic Italian Egg and potato Gnocchi


MAHITAJI

800 gram viazi ulaya
1 yai bichi
200 gram unga wa ngano



Kiazi hiki aina ya desiree ndio bora hasa kwa utengenezaji wa gnocchi il ukikosa unaweza tumia kiazi ulaya chochote ukinunua kiazi kiweke angalau siku 2 ili maji maji yapungue maana kikiwa fresha sana kinakua na maji na yanasababisha gnocchi iwe ngumu na nzito sana pia unaweza ukomba muuzaji sokoni akuuzie viazi ambayo sio fresha san vilivyokaa angalau siku 2 visiwe vya kuoza hahaaahahah!

Chukua viazi vyako vikiwa na maganda vioshe vizuri toa mchanga wote kishs vichemshe katika maji kwa dakika 20 hadi 25 hakikaisha vimeiva kwa kuchoma na uma au toothpick kisha  vitoe vimenye maganda vikiwa bado vyamoto kisha viponde ponge viwe tope kabisa.

Kisha weka unga wako na yai changanya vizuri kama unakanda unga wa mkate au maandazi usitumie muda mwingi utaaribu mchanganyiko wako unatakiwa ukande kiasi tukama bado unamaji maji basi ongeza unga kidofo tu ili ubaki laini usiwe mgumu sana mchanganyiko ukizidi una ukawa mkavu sana gnocchi inakua ngumu n nzito pia ukisha changanyika kata maumbo madogo madogo kama picha zinavyoonyesha hapo chini.



Kata umbo dogo la duara kisha kandamiza na uma ya chakula ili upate mistar mistari inayoweka muonekano mzuri


Weka maji katika sufuri chemsha mpaka yachemke kabisha kisha weka gnocchi zako mbichi zikiiva mara moja zitapanda juu ya maji zitoe na ziweke pembeni zipoe





Huu ni muonekano wa gnocchi zikiwa zimeiva na ziko pembeni zipoe





Kisha weka mafuta kidogo tu katika kikaango kilicho chemka sana ili uzikaange gnocchi kuongeza ladha ya kau kau pia zitabadilika na kua na rangi ya kahawia nzuri. kaanga kwa dakika 2 tu.



Weka kwenye kikaango chenye mafuta yaliyopata moto kisha kaanga


Huu ni muonekano wa gnocchi zilizokwisha kaangwa na kua na rangi nzuri ya kahawia



Huu ni mchanganyiko wa mboga za karoti, kitunguu na pili pili hoho kwajili ya kulia gnocchi



Weka mboga kwenye kikaangao chenye mafuta kiasi yaliochemka kisha kaanga kiasi tu kisha weka mchuzi wa nyanya safia kaanga kwa dakika 3 kisha itakua tayari kumbuka kuweka chumvi





Pakua zile gnocchi zilizokaangwa weka kwenye sahani



Kisha juu yake weka mboga mboga zenye mchuzi safi kabisa wa nyanya


Huu ni muonekano wa gnocchi tayari ikiwa na muonekano safi kabisa wa mchuzi wa nyanya na mboga mboga tayrai kwakuliwa kumbuka kumpa mlaji bado ikiw na moto.





Hii ndio GNOCCHI  yenyewe imeshapambwa na nynya ya kuchoma na jani la parsley inapendeza sana machoni na ladha yake ni safi sana.

Chakual hiki kinaweza kuliwa na mtoto na mtu mzima na wote wakafurahia pia ni rahisi sana kutengeneza.

Tunakaanga kuongeza ubora na kubadilisha ladha lakini unaweza zitoa katika maji baada ya kuchemsha na ukaziwekea mchuzi ukala safi kabisa bila kuzikaanga ili kubadilisha ladha.

Unaweza kula na nyama aina yeyote ile na ukafurahia sana sana.

IJALI FAMILIA YAKO KWA CHAKULA BORA NA SALAMA



4 comments:

Ruky said...

Sawa kaka tunasubiri maelekezo

Majoy said...

hiyo chakula inaonyesha ni tamu sana!nangoja recipe kwa hamu sana.

Flower said...

Sawa Chef Issa mi nasubiri kwa hamu hiyo recipe,nilishawahi kula hii gcocchi ila nilinunua supermarket!!sasa hii ya kutengeneza mwenyewe naamini itanoga zaidi!kazi njema.

Anonymous said...

ASANTE KWA MAPISHI YA AINA MBALIMBALI..........ME NAOMBA KUWEKEW MAPISHI YA KABABU,KACHORI,KATLESS,EGGCHOP NA SAMBUSA.