CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Saturday, April 24, 2010

JINSI YA KUANDAA CHAKULA CHA MTOTO KUTOKA KATIKA RATIBA

JINSI YA KUANDAA CHA CHAKULA CHA MTOTO KWA SIKU YA JUMANNE

KIFUNGUA KINYWA ( BREAKFAST)
Mtindi wa matunda, mkate wa mayai na nafaka za kukaushwa

Mtindi
100 gram Mtindi wa matunda ya ladha yeyote ile inaweza kua strawberry, passion, Embe, Nanasi au ndizi

Makate wa mayai
Chukua mayai 2
vipande 2 vya mkate

Vunja mayai katika sahani ili iwe rahisi kuupaka mayai mkate wako hakikisha vipande vyote viwili vinaenea mayai safi kabisa kisha chukua kikaango weka siagi kidogo kishaa kaanga mkate uwe na rangi kahawia mpatie mtoto ale ikiwa inamoto wa wastani isipoe itapoteza ladha na ni hatari kwa afya ya mtoto.

Nafaka za kukaushwa ( Cerials)
Unaweza mpatia nafaka za kukaushwa mfano Rice crisp, Coco pops, Wheetebix, Con flakes, All brain, Ban flakes na Muesli.

Unaweza chukua gram 100 ya moja wapo ya hizo nafaka pamoja na maziwa baridi 50 gram kisha changanya au unaweza ukachukua aina mbili za nafaka kila moja gram 50 ukazichnganya na maziwa kwahiyo mtoto anapata ladha ya nafaka aina mbili mfani corn flakes na coco pops.

CHAKULA CHA MCHANA
Chapati ya nyama ya kusaga, na chips au viazi vya kusaga na juisi ya nanasi

Chapati ya nyama ya kusaga
Chukua nyama ya kusaga 150 gram, kitunguu 30 gram , pili pili hoho 30 gram chumvi 5 gram na soya sauce 10 gram saga tena katika mashine ya kusagia nyama kisha changanya na yai moja.

Tengeneza umbo la duara safi kama chapati kisha choma katika kikaango chenye mafuta kiasi mpka iive mtoto anaweza kula na viazi vya kukaanga ( chips)


Hii ndio chapati ya nyama ya kusaga

Kama mtoto ni mdogo chemsha viazi na chumvi kisha viponde na maziwa kiasi mpatie na hiyo nyama atafurahia chakula.

Juisi ya nananasi
Menya nanasi kisha lisage na tangawizi kiasi kweye mashine ya kusagia chakula ( Blender) iweke katika friji bila sukari ili isiharibike weka sukari wakati wa kunya mtoto. Tangawizi inaongeza hamu ya kula.

CHAKULA CHA JIONI
Salad ya kuku wa kuchemsha, mtindi na matunda mchanganyiko

Chukua nyama ya kuku isiyo na mifupa 100 gram ichemshe na chumvi kiasi ikiisha iva iache ipoe. Kisha chukua mtindi usio na ladha ya matunda changanya na kuku pamona na matunda uliokata katika umbo dogo ili mtoto aweze kula.

CHAKULA CHA USIKU
Keki ya spinach, viazi vitamu na juisi ya maembe

200 gram Spinach mbichi
100 gram Maziwa
2 mayai
50 gram kitunguu

Chukua na kitunguu saga katika mashine ya kusagia nyama kisha changanya chumvi na yai na maziwa. Baada ya hapo chukua filo pastry itandaze katika mweza kisha juu yake weka mchanganyiko mzito wa spinach kisha funika na iweke kwenye oven oka kwa dakika 15 tu itakua tayari na rangi safi ya kahawia.


Hii ndio spinach cake filo pastry ipo kama manda inapatikana maduka ya chakula popote duniani na sio ghali
Viazi vitamu
Viazi vitamu unachemsha tu kawaida na chumvi

Juisi ya maembe
Menya embe 1 kisha unasaga katika mashine yakusagia chakula ( Blender) weka katangawizi kidogo kumuongezea mtoto hamu ya kula usiweke nyingi itamuwasha mtoto na hata furahia chakula.

ORODHA KWAJILI YA MANUNUZI

Mtindi wenye ladha ya tunda, Mtindi usio na ladha ya tunda, mkate, Yai, Nyama ya ng'ombe ya kusaga, Kitunguu, Viazi vitamu, Spinach, Maziwa, Embe, Papai, Tikiti maji, Filopastry, Nafaka za kukaushwa, Kitunguu, viazi ulaya, Nyma ya kuku na nanasi.


2 comments:

Anonymous said...

umesaidia sana mtoto wa rafiki yangu asiyependa kula kabisa

huu mlo umesaidia sana,niliprint na kumpelekea akafata aya mapishi yako

asante chef issa,keep on helping us

Anonymous said...

U are a star chef cook. Asante kwa ratiba safi na msaada wa kuandaa menu. Mungu akubariki sana.

thnkx, mama emery