CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Sunday, September 7, 2014

JIFUNZE KUTENGENEZA JUISI YA MCHANGANYIKO WA TIKITI MAJI, LIMAO NA NAZI

 
PATA MBINU SAFI KABISA YA KUTENGENEZA JUISI HII SAFI NA MURUA YA MCHANGANYIKO WA TIKITI MAJI, LIMAO NA NAZI
 
MAHITAJI
 450 grams Vipande vya Watermelon vyenye ubaridi,
250 gram ya maji ya dafu au Nazi changa
1 limao kubwa
10 vipande vya barafu au Ice cubes,
Fresh Mint kwajili ya kupambia
 
JINSI YA KUANDAA FATILIA MAELEZO NA PICHA HAPO CHINI
 
 
Kata nusu tikiti maji zuri lililoiva kama unavyoona kwenye picha kisha likate kate vipande na uweke kwenye friji vipoe kabla ya kutengeneza juisi yako
 
 
Chukua maji ya dafu, limao, vipande vya barafu na vipande vya tikiti maji kisha weka kwenye blender. Lengo la kuweka limao ni kuongeza na kubalance ladha. kama wewe ni mpenzi sana wa maji ya madafu unaweza ongeza zaidi ili ladha ya madafu isikike sana.
 

Blend vizuri mpaka vitu vyote vichanganyike safi kabisa.
 

 
 
Perfect drink for your summer, waandalie familia wafurahie pia kama unabiashara waandalie wateja wako wafurahie sana hasa kipindi hiki cha majira ya joto. kumbuka tikiti maji na dafu vyote vinasukari kwahiyo huna haja ya kuongeza sukari kabisa na ukafurahia kinywaji hiki murua.
 


1 comment:

Anonymous said...

mbegu za tikiti wazitoa au wasagia then uchuje?