CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Monday, September 22, 2014

JIFUNZE KUTENGENEZA SUPU SAFI KABISA YA MCHANGANYIKO WA MBOGA MAJANI

 
RECIPE SAFI KABISA YA KUPIKA SUPU YENYE MCHANGANYIKO WA LEEKS, BROCCOLI NA ASPARAGUS SAFI SANA KWA AFYA YA MLAJI
 
MAHITAJI
1 kitunguu kikubwa kichop chop
1 leek, isafishe vizuri kasha kata kata
2 viazi vidogo safika vizuri kasha kata kata na maganda yake bila kumenya
1 lita ya maji au unaweza tumia vegetable stock
1 bay leaf
5 gram chumvi
5 gram pili pili manga
500 gram Asparagus osha kisha kata kata 
500 gram broccoli osha katakata
 
JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI
 
 
Chukua leeks, viazi ulaya, kitunguu maji na bay leaf kisha weka kwenye sufuria lenye maji au vegetable stock na funika chemsha kwa dakika 10.

 
Baada ya dakika 10 kisha weka broccoli na asparagus na uendelee kuchemsha

 
kisha punguza moto uwe wa chini na endelea kuchemsha kwa dakika  10min kumbuka kuweka chumvi na pili pili manga na uonje.

 
Toa kwenye jiko na uache ipoe kiasi baada ya hapo toa bay leaf weka pembeni na mimina mchanganyiko wako kwenye blender na usage.

 
Baada ya kusaga rudishia kwenye sufuria na uendelee kuichemsha kiasi kwa dakika 5 baada ya hapo unaweza mpatia mlaji na kwajuu ukapamba na majani ya giligilani na ukampatia mnywaji akafurahia sana.
 
 


No comments: