CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Friday, February 11, 2011

JIFUNZE KUPIKA BIRIYANI SAFI NA RAHISI YA KUKU

 RECIPE SAFI SANA YA BIRIYANI YA KUKU

MAHITAJI

 ( Chakula hiki kinatosha watu 3 hadi 5 )



 600 gram mchele wa basmati basmati
 1 kuku mzima ( toa ngozi na kata vipande vikubwa kama kwenye picha)
6 Vitunguu umbo la kati
15 gram kitunguu swaumu cha kusagwa
10 gram tangawizi ya kusagwa
3 Nyanya katakat vipande vidogo
3 pili pili mbuzi za kijani
1 fungu la majani ya Mint
1 fungu la majani ya Coriander (giligilani)
3 kijiko kidogo cha chai Garam masala
100 gram Yogurt
1 kijiko kikubwa cha chakula juisi ya limao
3 kijiko kikubwa cha chakula mafuta ya samli
3 kijiko kikubwa cha chakula maziwa ya maji

VIUNGO VIZIMA VIZIMA PIA VINATAKIWA:

3 vipande vya mdalasini cinnamon stick
6 vipande vya karafuu
2 vipande vya hiriki ya kijani

KWA KUPAMBIA BIRIYANI YAKO:

Mafuta ya kukaangia
1 kitunguu kata slice
10 vipande vya korosho (Cashew nuts)
15 vipande vya zabibu kavu (Rasins)

JINSI YA KUPIKA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI



1. Loweka mchele kwenye maji kwa masaa 3.
2. Kisha chemsha mchele katika maji, chumvi na 1 kijiko cha garam masala kwa dakika 15, kisha toa mchele wako uchuje na weka pembeni. Wali huu ukiubonyeza kwa mikono utavunjika ingawa utakua haujaiva vizuri. Huu ndio ubora unaotakiwa kwani ukiivisha kabisa utakua umekosea.

3. Safisha kuku na kata katika vipande vikubwa.Kumbuka kukata kata mikato katika nyama ili iweze kuja kuiva haraka.



4. Chukua sufuria kubwa linaloweza kuingia mchele na kuku yoote wakati unapika. kisha weka samli iyeyuke
5.  Kisha weka viungo vyoote na kaanga mapaka upate harufu nzuri (aroma).
6. Kisha weka kitunguu na chumvi. Pika mapaka vitunguu vilainike. Kisha punguza moto uwe wa wastani.


7. Kisha weka kitunguu swaumu na tangawizi kaanga mpaka upate rangi ya kahawia.
8. Kisha weka nyanya na pili pili mbuzi. Acha mchanganyiko huu uive mpaka nyanya ipondeke .



9. Kisha weka majani ya mint na coriander . Funika na mfuniko na pika kwa dakika 10.



10. Kisha weka yogurt na unga wa garam masala.
11. Kisha ongeza limao juice na chumvi kidogo.


12.   Kisha chukua vipande vya kuku na weka katika mchanganyiko wako katika sufuria, funika na uache inaendelea kuiva.



13.   Kisha chukau wali na weka juu ya mchanganyiko wako wa kuku na mchuzi
14. Kisha mwagia maziwa juu ya wali.

15. Funika sufuri a yako hakikisha inafunika kabisa mvuke usitoke nje.
16. Baada ya hapo weka moto uwe mkali kabisa kwa dakika 2. KIsha punguza moto na acha ichemke kwa dakika 45.
17. Wakati huo huo pasha moto kikaango ili uweze kukaanga vitu utkavyopambia.




18. Choma vitunguu katika mafiuta mpaka upate rangi ya kahawia.
19. Kisha kaanga korosho mpaka rangi ya kahawia.
20. Kisha kaanga zabibu kavu kwa dakika 1 tu.
21. Baada ya kusubiri kwa dakika 45 sasa zungusha wali wako pamoja na nyama ya kuku vichanganyike pole pole.



22. Pakua chakula chako na ukipambe kisha mpatie mlaji kikiwa cha moto.

MBINU ENDAPO UNATAKA KUTUMIA NYAMA TOFAUTI:
1.Kama unataka kutumia nyama ya ngombe au ya mbuzi au yakondoo.

Unatakiwa nyama uiwekee viungo hivi na ikae usiku kucha katika friji ili iweze kua laini ( 100 gram yogurt, 1 kijiko cha chakula white vinegar- 1 kijiko cha chai garam masala powder).
Kwa mtindo huu wali itabidi upike kwa dakika 10 pembeni.
Katika sufuria ya mchanganyiko wa nyama kwa kufata hatua zile ziule kitakachoongezeka ni muda wa kupika ikiwa ni nyama pika kwa saa 1 na dakika 15.





CHAKULA HIKI NI KITAMU SANA NA NIRAHISI KUKITENGENEZA WAANDALIE FAMILIA YAKO WAFURAHIE CHAKULA HIKI.

5 comments:

Anonymous said...

Hey, great blog.. :)
Tunasubiri recipe ya Biriyan. I am in the same industry pia. Its nice to see this!
http://zibra.onsugar.com/

Sophie said...

Biriani yapendeza!kazi nzuri.

Flower said...

Nasubiri recipe kwa hamu,kwani hiki chakula nilikula zamani sana na sijawahi kukipika.na nikishatengeneza nitakutumia picha

mally said...

mashala t looks yummy! an easy 2make thanx 4d easy recipe

Unknown said...

naitaji sana kujua kupika na ningependekeza wewe kuwa mwalimu wangu, naomba msada kutoka kwako kaka!