CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Friday, February 11, 2011

JIFUNZE KUPIKA MCHUZI SAFI WENYE VIUNGO PAMOJA NA VIAZI NA MCHANGANYIKO WA PRAWNS


MCHUZI HUU WENYE MCHANGANYIKO WA VIUNGO, VIAZI MBATATA (ULAYA) NA PRAWNS NI SAFI SANA KAA TAYARI KWA RECIPE SAFI SANA


MAHITAJI

 ½ kg ya prawns

 3 viazi vikubwa menya kisha katakata vipande
 2 vya ukubwa wa wasyani chop chop
5 gram kitunguu swaumu
5gram tangawizi
1 Nyanya ya kuiva  kubwa katakata
 2 Pili pili mbuzi ya kijani katakata
 1 kijiko kidogfo cha chai Coriander powder
 1 kijiko kidogo cha chai Turmeric powder
 ¼ kijiko kidogo cha chai  Fennel seeds powder ( sio lazima)
 ¼ kijiko kidogo cha chai Garam masala powder
  1 fungu la Coriander ( giligilani) chop chop
3 kijiko kikubwa cha chakula Coconut milk powder
3 kijiko kikubwa cha chakula mafuta ya kupikia
1 lita ya maji ya kupikia
 ½ kijiko kidogo cha chai sukari
5 gram chumvi

 



JINSI YA KUANDAA FATILIA MAELEZO HAPA CHINI

 
1. Chukua prawns wawekee maji ya limao pamoja na chumvi, pili pili manga kidogo na kitunguu swaumu kidogo kisha weka katika fridge kwa dakika 15 hadi 20.

2. Baada ya dakika 20 toa limao itakua imeingiza vizuri katika prawns.

3. Weka mafuta katika kikaango au sufuria kisha yapate moto wa wastani.

4. Baada ya mafuta kupata moto weka kitunguu na endelea kukaanga.

5. Kisha ongeza kitunguu swaumu na tangawizi endelea kukaanga mpaka harufu ya ubichi iishe.

6. Kisha weka pili pili mbuzi, turmeric powder endelea kukaanga mpaka mpaka upate harufu safi ya kunukia.

7. Kisha weka coriander powder, turmeric powder and fennel powder koroga ichanganyike vizuri. Viungo vingi ni vya unga weka maji kidogo kulainisha ili mchanganyiko wako usiungua na kushika sufuria. Acha iive pole pole mpaka ubichi na harufu ya masala upotee.

8. Kisha ongeza nyanya na piaka kwa muda.

9. Kisha ongeza vipande vya viazi, maji kiasi tena pamoja na chumvi.

10. Pika kwa moto wa wastani mpaka viazi viive na maji yapungue.

11. Wakati huo huo chukua wale prawn na uwakaange katika kikaango chenye mafuta kiasi kwa dakika 3.

12. Kisha chukua hao prawns na waweke katika ule mchanganyiko wenye viazi.

13. Chukua glasi na weka maji ya vugu vugu nusu na uchanganye na ile coconut milk powder hakikisha unakoroga vizuri kutoa mabonge mabonge.

14. Punguza moto tena na mimina na ukorogr coconut milk katka mchanganyiko wenye viazi na prawns.

15. Nazi ikisha iva ndani ya mchanganyiko wako hapo chakula kitakua taari kuliwa chukua majani ya coriander chop chop unaweza mpatia mlaji chakula hiki pamoja na wali au mkate au chapati na ikapendeza sana na familia ikafurahia sana.





CHAKULA HIKI KINATOSHA KWA WATU WA 5  AU ZAIDI INATEGEMEA NA UWEZO WA WALAJI.


 

2 comments:

Anonymous said...

Jamani brother Issa asante sana sana kwa hizi recipe. Huwa hatu comment but mimi naingia humu kwenye blog yako mara nyingi kupata idea ya vitu vya kupika. Umenifundisha mengi! Shukrani :)

Anonymous said...

Hi Chef, unatumia prawns gani? Peeled or unpeeled?