CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Thursday, March 21, 2013

JIFUNZE KUTENGENEZA YAI JICHO LA NG'OMBE NA KIPANDE CHA MKATE

 
RECIPE SAFI KABISA YA KUTENGENEZA KITAFUNWA HIKI KWA WAKATI WA MAPUMZIKO YAHA MAREFU.
 
MAHITAJI
 
1 Yai
1 kipande cha mkate
1/2 kijiko kidogo cha chai siagi
5 gram chumvi
2 gram pili pili manga
 
JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI
 
 
Chukua kipande cha mkate kunja nusu kisha kata mduara kati kati.

 
Huu ndio muonekano wa mduara baada ya kukata

 
Chukua brush na kisha paka pande zote mbili siagi.

 
Chukua kipande cha mkate kisha weka katika kikaango chenye moto wa wastani ili isiungue.

 
Kisha pasua yai na mimina kati kati ya mkate

 
Kisha nyunyizia chumvi na pili pili manga kwa juu ya yai nali mkate.

 
Baada ya dakika 3 hadi 4, upande mmoja uta.kua umeiva geuza upande wa pili

 
Upande wa pili pika kwa dakika 2 tu utakua umeiva pia.


HUU NI MUONEKANO WA MKATE JICHO LA NG'OMBE UKIWA UMEIVA WAANDALIE FAMILIA WAFURAHIE.
 
UKITAKA KUENJOY ZAIDI FUNGUA FACEBOOK PAGE KWA KU CLICK HII LINK http://www.facebook.com/pages/Active-chef/509561519067534 KISHA CLICK LIKE NA UTAKUA MWANACHAMA UTAWEZA PATA HABARI ZOTE ZINAZOHUSU MAPISHI NA PIA MAPISHI MAPYA KILA SIKU.

1 comment:

Anonymous said...

SASA MBONA ILO JICHO LIMETOWEKA TENA ICHO KIINI CHA NJANO?