CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Tuesday, March 5, 2013

JIFUNZE KUTENGENEZA KEKI HII YA MCHANGANYIKO WA KOKOA BILA YA KTUMIA MAYAI

 UTENGENZAJI WA KEKI HII YA MCHANGANYIKO WA KOKOA BILA YA KUTUMIA MAYAI
 
MAHITAJI
250 gms unga wa ngano
250 gms sukari
250 gms siagi
50 gms unga wa cocoa
1 kijiko kidogo cha chai baking soda
1/2 kijiko kidogo cha chai baking powder
1/2 kijiko kidogo cha chai chumvi
1 kijiko kidogo cha chai vanilla essence
250 gram pureed Mori Nu silken Tofu (Badala ya mayai 4)

JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAFUNZO HAPO CHINI

Muda wa maandalizi : Dakika 30 mpaka saa 1
Muda wa kupika 30 mpaka saa 1
Idadi ya walaji: Watu 4
 
Hii ni picha ya Tofu inauzwa madukani.
 
 
Washa oven katika moto wa 180 deg C (350 deg F). Paka siagi au mafuta pia nyunyizia unga kwa mbali kwenye pan  ya ukubwa huu (8″x8″), Fungua box lenye mchanganyiko wa tofu na upoige kama wewe hutumii mayai nakama unatumia mayai basi piga mayai 4 piga kwa mkono au mashine mpaka uone mapovu.

 
Weka katika chujio la chuma unga wa ngano, cocoa powder, baking powder, baking soda pamoja na chumvi.

 
Hakikisha umechekecha vizuri na kisha weka pembeni.

 
Chukua siagi na sukari pia piga kwa mashine au mchapo changanya na vanilla essence.

 
Chukua mchanganyiko wa tofu au mayai weka katika mchanganyiko wa siagi na sukari. 
 
 
Tumia mchapo au mashine chapa mpaka uchanganyike safi kabisa mchanganyiko wako.
 
 
Sasa mimina mchanganyiko wa unga pole pole katika mchanganyiko wa siagi na mayai au tofu

 
Kisha endelea kupiga kwa mchapo au mashine mpaka mchanganyiko wako uchanganyike vizuri.

 
Kama mchanganyiko wako umekua mzito basi unaweza mimina pole pole maziwa huku ukiendelea kuchanganya.

 
Kisha mimina mchanganyiko wako mzito katika pan,

 
Hakikisha unasambaza vizuri kwa juu iwe na muonekano mzuri kabisa.
 
 
Kisha choma kwa dakika 45 mpaka 5 itakua imeiva. ( oven yangu inachoma kwa dakika 32 tu )

 
Huu ndio muonekano wa keki baada ya kuiva, hapa nimeiweka ili ipoe.
 
 
 
Weka keki yako katika tray yake kisha mwagia sukari ya unga au icing sugar kwa juu kuongeza mvuto. Unaona muonekano safi kabisa. Pika kwa biashara au kitafunwa nyumbani.
 
 


3 comments:

Anonymous said...

Asante kwa mafundisho mazuri ya mapishi tofauti tofauti kaka.

Mimi naomba utuelekeze sehemu ya kununua vegetable salt kwa sababu nimeitafuta sana bila mafanikio.

Anonymous said...

MWANAUME UNAPIKA ADI HATARI...NIMEIPENDA HII KEKI

Tina said...

hii TOFU Tz ipo kwweli?