CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Sunday, May 23, 2010

KUKU WA UFUTA NA KARANGA

KUKU HUYU NI RAHISI SANA KUPIKA, UNAWEZA HIFADHI KATIKA FRIJI KWA MUDA WA MWEZI NA CHAKULA BADO KIKAWA NA LADHA SAFI KABISAWAANDALIE FAMILIA YAKO WAFURAHIE

MAHITAJI

1 kitunguu kikubwa
1/2 kuku au 1 kuku mzima
4 nyanya zilizoiva vizuri katakata au saga katika blenda
2 vijiko vikubwa vya chakula nyanya ya kopo
3 ufuta mkavu kijiko kikubwa cha chakula
4 kijiko kikubwa cha chakula karanga ya kusaga iwe mbichi au ilyokaangwa sawa tu
2 kijiko cha chakula mafuta ya kupikia maana karanga inamafuta mengi
1 chumvi kijiko kidogo cha chai
2 fungu la majani ya girigilani ( corrender leaves)
1 kijiko kidogo cha chai kitunguu swaumu

weka mafuta ya kupikia na kitunguu katika sufuri kaanga kidogo kisha weka kitunguu swaumu

Kisha weka nyanya ya kopo endelea kukaanga

kisha weka kaanga iliyosagwa endelea kukoroga vizuri

baada ya kukorogasafi na mchanganyiko wako kua mzito na safi kabisa huu ndio muonekano wake kisha weka chumvi

kisha weka majani ya girigilani au corriender leaves na ukoroge vizuri

kisha weka nyanya uliyokua umesaga

koroga na acha ichemke vizuri ili nyanya iive vizuri

Hapa sasa nyanya imeiva safi na imechemka ya kutosha imeshabadilika rangi na mchuzi wote umekua na ladha ya karanga

Kisha weka vipande vya nyama ya kuku inapendez kama utakua umeichemsha ika iva pia usimwage ule mchuzi au maji uliyochemshia huyo kuku utayatumia hapa badala ya kuongexza maji unatumia mabaki ya mchuzi ulio chemshia huyio kuku ili kulinda ladha ya chakula hik


MWISHO KABISA PAKUA KUKU NA WEKA KATIKA CHOMBO CHA MLAJI KIHA MWAGIA JUU ULE UFUTA MALAJI ATAKAPOKUA ANAKULA UTAUTAFUNA UFUTA LIVE NA KUONGEZA LADHA SAFI KATIKA CHAKULA CHAKE KAMA UNAPIKA KWA FAMILIA AKUBWA BASI BAADA YA KUKU WAKO KUIVAMWAGIA UFUTA NDANI YA MCHUZI NA KOROGA VIZURI ILI UCHANGANYIKE KISHA WEKA MEZANI FAMILIA IFURAHIE






2 comments:

Unknown said...

hii nini hamu ya kui-test inaelekea ni tamu sana.
Tupe recipe kaka. Asante sana.

Anonymous said...

Chef Issa tunaomba ss usiwe na haraka maana unatowa picha alafu unasema subiri recipie kama hiyo ya kuku wa ufuta mbona kama kazi inakushinda bro??? ss tunabaki tunasubiri hatutaki mambo ya picha twataka vitendo haya ona ss usharukia mandazi ya iliki hujamaliza chapati yaaaaaaak!!!!!!!