CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Thursday, October 28, 2010

JIFUNZE KUTENGENEZA CHATNEY YA KITUNGUU

 HII NDIO CHATNEY YA KITUNGUU NI SAFI SANA NA INAONGEZA LADHA KWA CHAKULA CHOCHOTE KILE UTACHOPENDA KUITUMIA

MAHITAJI

120 gram dengu
2 au 3 pili pili nyekundu kavu (dried red chillies)
2 au 3 mbegu za pili pili manga
2 vitunguu vikubwa cheupe au chekundu kata kata
3 mbegu za ukwaju 
4 majani  mabichi ya binzali (curry leaves) sio lazima
10 gram chumvi
2 kijiko kidogo cha chai limao
1 kijiko kidogo cha chai unga wa kitunguu swaumu au iliyosagwa
3 kijiko kikubwa cha mafuta ya mahindi au ya olive


JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI



Weka mafuta katika kikaango acha yapate moto kisha weka dengu, pili pili kavu, pili pili manga, kisha kaanga kwa dakia 2 mpka harufu nzuri ikianza kunukia.



Kisha ongeza kitunguu maji, kitunguu swaumu, kitunguu swaumu na chumvi kisha kaanga mapak kitunguu kiwe laini. Baada ya hapo oongewa mebu za ukwaju, maji ya limao na majani mabichi ya binzali kisha kaanga kwa dakia 1 tu na zima jiko.



Kisha weka mchanganyiko huu atika blenda na saga mpaka upate uzito kabisa na iwe imesagika yote.



Muonekano wa uzito huo katika blenda ndio kipimo sahii cha chatney yako. inaharugu safi sana na inavutia na inaongeza hamu ya kula sana.



HUU NI MUONEKANO SAFI KABISA BAADA YA CHATNEY YAKO KUA TAYARI KWA MLAJI KUITUMIA

FURAHIA NA FAMILIA YAKO



1 comment:

Anonymous said...

kwenye picha kunanonekana kama kuna viazi mviringo. Ni kitu gani hicho?