CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Friday, October 1, 2010

JIFUNZE KUTENGENEZA KEKI YA CHOCOLATE BILA YA KUTUMIA MAYAI


NI RAHISI SANA KUTENGENEZA KEKI HII NA INACHUKUA MUDA MFUPI SANA KUANDAA HAYA WAPENZI WA CHOCOLATE KAZI KWENU HATUA ZA UPISHI NI 5 TU KEKI IMEIVA.

MAHITAJI

2 Kijiko kikubwa cha chakula unga wa cocoa 

240 gram unga wa ngano 
1 kijiko kidogo cha chai baking powder
1/2 kijiko kidogo cha chai asoda bi-carbonate
400 grams maziwa ya maji
120 gram siagi iliyoyeyushwa
1 kijiko kidogocha chai  vanilla essence



JINSI YA KUANDAA FATILIA MAFUNZO CHINI





1.Changanya pamoja unga wa cocoa,unga wa ngano, baking powder na soda bi-carbonate.




2.Changanya mchanganyiko wote pamoja na 120 gram ya maji kwa kutumia mchapo mpaka vichanganyike vizuri. 

 


3.KIsha chukua chombo chako cha kuokea hiyo keki na kipake mafuta ya siagi kish mimina mchanganyiko wako wa keki katika chombo hicho.




4.Choma katika oven iliyona moto wa 180°C (360°F) kwa dakika 20 Kisha tumia kijiti choma kikitoka kisafi basi keki yako itakua imeshaiva.

 


5.Acha ipoe kwa dakika tano kisha itoe na iweke katika sahani chini kuwe juu na juu kuwe chini kisha mwagia juu sukari aya unga kuweka muonekano thabiti.






Kata vipande na mpatie mlaji afurahie
YAMY YAMY!!!!!!!


No comments: