CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Tuesday, March 16, 2010

CHICKEN STRIPED PICCATA OHHH TAMU SANA HII

MAHITAJI

3 Mayai
300 gram cheddah cheese ikwaruze
30 gram unga wa binzari
200gram mafuta ya kupikia
1 kijiko kidogo cha chai chumvi  


JINSI YA KUPIKA FATA MAELEZO CHINI KAMA PICHA ZINAVYOELEKEZA



Chukua cheese aina ya chedah ikwaruze vizuri



kata nyama ya kuku toa mifupa na ukate vipande vidogo kama umbo la kidole kwa urefu



Changanya mayai na cheese pamoja na chumvi na nyama ya kuku



Kisha ongezea unga wa binzali changanya vizuri upate rangi safi ya manjano




weka mafuta ya kupikia katika kikaango chako kisha chukua kipande kimoja kimoja weka kwenye kikaango au griller choma mayai ya kauke vizuri



Huu ni muonekano wa nyama ikiwa na mayai kwenye kikaango



Hapa ni muonekano baada ya mayai kukauka vizuri kweney nyama




Toa nyama ya ko na weka katika sinia ili uiweke katika oven ikauke kama huna oven tumia microwave iweke kwa dakika 3 tu itakua tayari kwa kula




HUU NI MUONEKANO WA CHAKULA CHAKO SAFI KABISA UNAWEZA KULA KWA CHIPS AU UGALI NA CHAPATI PIA BILA KUSAHAU MBOGA MAJANI NA MCHUZI WA NYANYA. LADHA YA MAYAI NA CHEESE OHHH SAFI SANA SANA NA INAONGEZA MADINI JOTO MWILINI.

5 comments:

Anonymous said...

Kaka sasa unauwa band!
Tumbo lishaanza kukoroma hapa.
Kuku? mtu asiyekula kuku kakatazwa na daktari au huyo ni strong veg.

Nitajaribu pishi hili siku mbili hizi Inshallah.


disminder.

Anonymous said...

hi issa pole sana na kazi za hapa na pale na mm napenda sana mapishi na kila siku lazima nianglie blog yako sasa kaka hapo kwenye rec yako naomba msaada kidogo tu kwenye mahitaji ulisema mafuta ya kukaangia je unayatumia wapi hayo mafuta

mdau

Anonymous said...

Kaka issa asante sana kwa kuanzisha blog hii, nina pendekezo moja unaonaje kama ukiweka labels kwenye posts zako (kwa mfano angalia http://changamotoyetu.blogspot.com/
au
http://www.mamanamwana.blogspot.com/)

hii itatusaidia sana wadau wako kuweza kupata recipe hizi wakati tunapozihitaji kuliko ilivyo sasa kwani ni lazima ukumbuke pishi unalolitafuta lilipostiwa wakati gani
ni hayo tu asante sana kwa kazi nzuri.

Anonymous said...

Wewe ni mkali!!!!

Anonymous said...

Kwa jinsi nilivyoona hizo kuku, na nipendavyo burger ya kuku, nimejaribu kuweka mayonise, salad na mooooose bado kidogo nijitafune vidole nikidhani ni burger.
Ni kawaida yangu kutunga tunga mapishi.

welldone.