CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Monday, May 17, 2010

JUISI YA PAPAYA AU PAPAI

FURAHISHA FAMILIA YAKO USIWACHOSHE KWA KUWAANDALIA JUISI ZA LADHA MABLI MABALI NA TAMU KAMA HII




MAHITAJI

480 gram papai lililoiva ( sawa na papai moja lililoiva)
240 gram sukari
1 juisi ya limao au ndimu kijiko kikubwa cha chakula ( swa na malimao au ndimu 2 - 3)
480 gram maji safi ya baridi

Jinsi ya kuandaa

Menya papai kisha tumia kijiko kuondoa mbegu na utando wa juu unaoshikilia hizo mbegu, kisha kata katika vipande vidogo vidogo.

Kisha chukua papai, sukari, juisi ya limao au ndimu na maji saga katika blender pamoja na kisha weka katika friji ipoe.




HUU NDIO MUONEKANO WA JUISI YA PAPAI SAFI KABISA IKIWA NA VIPANDE VYA CHOCOLATE PIA UNAWEZA WEKA PILI PILI MANGA KIASI SIO LAZIMA NI KATIKA KUONGEZA LADHA. LAZIMA NI LADHA YA LIMAO KWA MBALI NI NZURI KWA AFYA KWA MTU MZIMA NA MTOTO PIA INASAIDIA SANA KULAINISHA TUMBO NA KUTOA UCHAFU PIA INASAIDIA SANA KWA WATU WENYE MATATIZO YA GESI TUMBONI


3 comments:

Anonymous said...

mbona nyeusi nyeusi ndani?mbegu si natoa?nieleweshe kaka!

Anonymous said...

Anonymous hapo juu, soma vizuri maelezo yake!!! Nadhani kaelezea.

Anonymous said...

asante sana,nilishawai tengeneza hii juice ingawa izi new recipe ya ndimu/limao sikuwai weka,,,ntajaribu leo kwawel

lol kaka unatupa utamu sana wee hujui tu,asante mnoooo

endelea