CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Monday, February 13, 2012

JIFUNZE KUTENGENEZA BAJIA HII YA MBOGA AINA YA CAULIMAUA


JIFUNZE KUPIKA KITAFUNWA HIKI SAFI KABISA NI RAHISI KINAVUTIA

MAHITAJI

250 gms Cauliflower, kata vipande
120 gram unga wa dengu (chickpea flour)
60 gram unga wa mchele
2 kijiko kikubwa cha chakula unga wa ngano
5 gram chumvi
5 gram unga wa pili pili (Chilli powder)

JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAFUNZO

Muda wa maandalizi : Dakika 15
Muda wa mapishi : Dakika 15
Idadi ya walaji : Watu 4



Pasha mafuta kwajili ya kukaangia. Huo ni muonekano safi kabisa wa colimaua za rangi tofauti ingawa nyumbani Tanzania ni adimu sana kupatikana kwa mchanganyiko huo wa rangi ya zambarau, orange na kijani ila kwa rangi nyeupe ni maarufu sana na zinapatikana kila sehemu.


Kisha kata kata coulimaua zote na kisha ziweke pembeni zikauke.


Chukua unga aina zote pamoja na chumvi na pili pili ya unga kisha changanya ichanganyike.



Kisha ongeza kijiko kidogo cha mafuta yamoto pamoja na maji ya uvugu vugu.



Hakikisha unachanganya ili kupata mchanganyiko mzito kama uonekanavyo katika picha.



Ukijaribu kumimina unapata mmiminiko mzito kabisa.


Kisha chukua kipande cha cauliflower chovya kwenye mchangantiko wa unga.



Hakikisha unachovya vizuri ili uweze kuenea sehemu zote.



. Unaweza weka vipande vingi kwa wakati mmoja ili kuokoa muda pia inategemea na ukubwa wa kikaango chako.



Kwa kikaango changu huwa natumia vipande vitatu hadi vinne kukaanga kwa wakati mmoja.



Kaanga kwenye moto wa wastani kwa dakika  2 au 3 mpaka iwe na rangi ya golden au reddish brown.



Ukizikaanga kwa moto unaotakiwa basi hazita meza mafuta ila kwauhakika zaidi weka karatasi katika bakuli au sinia kisha ukizitoa katika mafuta ziweke ili zijichuje mafuta.



Unaweza kula na tomato sauce au ketchup au hata chutney ya ladha yeyote na ukafurahia


Inavutia sana na itasaiaidia kuhamasisha ulaji wa mboga. Pia unaweza ukawashawishi watoto nyumbani kupenda kula mboga majani kwakua umeweza kutengeneza chakula chenye rangi mchanganyiko pia mkaanza mchezo wa kubahatisha nani kapata rangi gani na usishangae hata watu wazima wakajiunga kubahatisha nani kapata rangi ipi.  hahahaaaaaaaa!




AINA HII YA MAPISHI UNAWEZA FANYA KWA VIPANDE VYA SAMAHI, NYAMA YA NG'OMBE HATA NYAMA YA KUKU PAMOJA NA DAGAA. NA FAMILAI IKAFURAHIA SANA SANA.

3 comments:

Anonymous said...

inaelekea ni kitafunwa kitamu, lkn tunaomba maelezo kaka.... Kazi njema

Mija Shija Sayi said...

Safi sana. Sikuwahi kufikiri pishi hili kabisa.

Kaka naomba ukipata muda utupe mafunzo ya kutengeneza Fondant Icing

Natanguliza shukrani.

God Bless.

Anonymous said...

nimeipenda sana blog yako.