CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Thursday, May 27, 2010

CHAPATI NA NYAMA YA MBUZI

CHAPATI HIZI NI SAFI KABISA KWA FAMILIA KUBWA KUTOPIKA MARA KWA MARA UNAPIKA NYINGI NA UNAZITUNZA WIKI MOJA NA ZIKABAKI NA UBORA ULEULE, PIA NYAMA HII YA MBUZI INAKUA HAINA HARUFU MTU YEYOTE ANAWEZA KULA KWA AINA HII YA MAPISHI NA AKAFURAHIA SANA 

MAHITAJI

1 kg unga wa ngano
1 kikombe kimoja
1 kijiko kidogo cha chai chumvi
nusu kikombeha chai mafuta ya kupikia
2 mayai kuongeza ladha

JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA NA MAELEKEZO CHINI

unga wa ngano

Weka mafuta katika unga

kisha weka moto sana katika unga

kisha changanya kwa kutumia mwiko maana maji ni yamoto sana

weka chumvi

kishaanza kukanda kwa mkono maji yatakua yameshapoa

kanda unga safi kabisa uchanganyike

kisha anza kusukuma unga wote

baad ya hapo mwagia kwa juu mafuta ya kula pakaza eneo lote

hakikisha mafuta yameenea unga wote

kisha kunja pole pole unga wote kutengeneza mduara

kisha kata maumbo madogo ya usawa kwa kutumia kisu

baada ya hapo chuku yale maumbo uliyokata geuza na uyakandamize safi mpka chini

hapa ni baada ya kuzikandamiza


kisha chukua mti wa kusukumia na zisukume mapak upate upana wa kawaida tayari kwa kuzichoma


weka katika kikaango kikavu kisha zungusha chapati hiyo kw kutumia mkono


iache kidogo ichomwe


kisha igeuze baada ya kuiva upande mmoja

ikandamize tena kwa upande wa pili bado ikiwa kavu bila mafuta kama ni yamoto sana basi tumia karatasi kukandamizia


weka mafuta ya kupikia kwa juu hakikisha unasambaza chapati yote ienee


kisha geuza a upande wa pili paka pia mafuta


Toa weka katika sahani itakua imeiva safi kabisa tayari wa kuliwa

weka pembeni zipoe kisha unaziwekakatika sahani unatumbukiza katik mfuko wa plastiki usiweke kwenye friji weka tu nje zitakua safi na laini zinakaa wiki 1 baada ya hapo zitapoteza ubora ukitaka kula unatoa unapasha kwenye kikaango au kwenye micro wave inakua yamoto na laini zaidi na iliyochambuka kwa ubora uleule
MAHITAJI NYAMA YA MBUZI

1 kilo nyama ya mbuzi
1 kitunguu kikubwa
1 nyanya ya kopo
1 kijiko kidogo cha chai kitunguu swaumu
3 viazi ulaya
1 kikombe kilichojaa mchanganyiko w mboga majani
1 kikombe cha maji baridi
1/2 kikombe mafuta ya kupikia

weka mafuta katika sufuri yakishapata moto weka kitunguu maji kaanga


hii ni nyama ya mbuzi ya mifupa inaladha yake ya kipekee sana

kaanaga vitunguu mpaka viwe vya kahawia ili kuleta ladha nzuri katika mchuzi wako na kuondoa harufu ya mbuzi ili mtu yeyote yule aweze kula

baada ya kitunguu kuwa kahawia weka nyama ya mbuzi piaendkea kukaanga

ongeza maji kiasi ili sufuria isiungue pamoja na nyama

kisha weka chumvi

acha mbuzi ichemke na itakua na mchuzi wa kahawia

kisha weka kitunguu swaumu hicho ni kifaa maalumu cha kusagia kitunguu swumu

baada yahapo weka viazi uklaya vilivyomenywa safi na kukatwa katwa vidogo

kisha weka nyanya ya kopo

kisha weka mchanganyiko wa mboga majani ( caroti, njegere na pili pili hoho, mahindi machanga ya njano)

kuongeza ladha zaidi unaweza weka unga wa binzali au rojo la binzali


MAFUNZO SAFI KABISA YA CHAPATI NA NYAMA YA MBUZI WAPIKIE FAMILIA YAKO CHAKULA BORA NA SALAMA WAFURAHIE





18 comments:

Disminder orig baby said...

Mume wangu anavyopenda chapati kwa maharage! ebu tupe recipe za chapati tupate kuongeza ujuzi.
Mbuzi itakuwa kiongezeo poa katika mlo huo.

Asante bro.

Anonymous said...

kAKA HIZO RECIPE ZIKO WAPI? UNATUJAZA MATE TU MIDOMONI1

Unknown said...

Tafadhali nitumie hiyo ratiba ya chakula cha mtoto maana vyakula vyote nanunua lakini mtoto wangu ana upungufu wa damu, pengine lishe siyo well controlled. Ntashukuru sana kwa hilo

Anonymous said...

kaka twaomba basi hizo recipe asante kwa kazi nzuri uifanyaoyo.

Anonymous said...

atleast kila picha iwe captioned

Flora said...

Tunaomba maelekezo kaka Chef!!!!

Anonymous said...

Woow nimependa sana style ya kukata chapati sijawahi ona natumia muda mrefu kufanya madonge madogo then nasukums naweka mafuta bt hiyo yako safi sana nasubiria sambusa maana kuzikunha style nying thanks sheffffff ybty

Disminder orig baby said...

Asante hiyo style ya kukata chapati nimeipenda ni rahisi sana.

Mimi uwa situmii mafuta kupika roast ya nyama lakini naenda steps kama zako. Asante sana.

Natengeneza nyama yangu, na kutayarisha vitu vingine.
Naichangaya na kitunguu maji, pili pili Manga ya unga, chumvi then nachemsha bila kuweka maji kwanza.
ikishaanza kukauka yale maji yake naongeza maji kwa kiasi ikiiva na kukaribia kukauka, naweka nyanya ya tunda, mbatambata (viazi ulaya) na kitunguu saumu, na nyaya ya paketi, naendelea kuchemsha mpaka nyanya ziive vizuri na kuangalia roast iwe ya kutosha.
Ikibaki kama dakika 5 kutoa ndiyo naweka karoti, hoho, na curry powder.

I hope niko sahihi kaka.

mama yangu ni mgonjwa anakula mafuta mara chache na kidogo sana na sunflower/oliveoil tu.

kashubi said...

Ahsante sana kwa upishi wa chapati maana umenipa mbinu mpya ya kusukuma unga wote uliokandwa, kupaka mafuta, kukunja na halafu kukata vipande. Kwa kweli hii inarahisisha kazi badala ya kukata donge moja moja. Ubarikiwe sana.

Anonymous said...

sijaelewa hapo katika chapati umesema mayai lakini hujatuelekeza yameenda wapi kwani chef hujasema tuyaweke wapi.please chef sie wengine ni copy and peste...

Noell said...

Asante kwa kuweka mazingira mazuri ya kiafya hii ni habari mpya toka kwangu kuhusu blog blog yako iko poa sana lakini jitahidi kuiboresha zaidi ipendeze hata mimi blog ninayo ila bado nahisi haijapendeza nafikiri kama unaushauri naomba unishauri bado sijamwambia Mr michuzi aitangaze lakini nategemea kuiboresha kama unaitaji kuiona tembelea www.mwangajamii.blogspot.com au kunipa ushauri niandikie ujumbe kwa barua pepe noellsaidi@gmail.com ushauri wako utaniweka karibu na wewe daima ubarikiwe kwa kuelimisha na kufundisha mapishi bora.

Anonymous said...

Asante kaka. nimepata mbinu mpya na rahisi ya kupika chapati!!

Anonymous said...

THANKS ALOT ISSA YAANI NILIKUA SIJUI KUPIKA CHAPATI NZURI NILIKUA NAONA NI KAZI NDEFU BUT WITH THIS WATANIKOMA UBARIKIWE

Anonymous said...

i love u bro kweli ubarikiwe blog yako imenifundisha mengi sana
love uuu

Anonymous said...

gud job aisee.. thumb up.

Anonymous said...

hey chef, hiyo mbuzi haitakua ngumu km usipoichemsha kwanza?? i love cooking am gladdy i hv found this group

Anonymous said...

Issa asante sana kwa kutufundisha kupika, mimi familia yangu hupenda sana Chapati. Sasa nimepata njia mpya ya kupika kwa urahisi kidogo badala ya kukunja moja moja kumbe naweza sukuma msukumo wa kwanza kwa mara moja.

Anonymous said...

nashukuru kwa kipindi chako kwa lishe za watoto naomba unitumie ratiba kwa mtoto wa miezi tisa hadi mwaka mmoja via josepheva95@yahoo.com,ratiba ya mtoto wa miaka miwili nakuendelea via pninje@yahoo.com