CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Sunday, July 25, 2010

JE UNAPENDA KULA BURGER YA NYAMA YA KIFUA CHA KUKU


BURGER HII SI MAARUFU SANA ILA NI NZURI SANA NA NI RAHISI KUTENGENEZA KAA TAYARI KWA KUWAKAMATA FAMILIA YAKO KWA RECIPE HII

MAHITAJI

200 gram kifua cha kuku
1 mkate wa mvirongo kwajili ya burger yako
50 gram vipande vya duara tango
50 gram vipande duara nyanya fresh iliyoiva vizuri
20 gram mayonaise
20 gram kitunguu maji slice
20 gram tomato ketchup au tomato sauce
20 gram BBQ sauce
5 gram chumvi
5 gram pili pili manga
30 gram matango machanga ya kopo ( Ghekins)



Huu ndio muonekano wa kifua cha kuku chukua chumvi, pilipili manga na BBQ sauce kipake vizuri kisha weka kweney friji kwa nusu saa au saa moja ili mchanganyiko huo uingie vizuri kwenye nyama na iwe na ladha safi.



Baada ya saa 1 chukua kifua hicho cha kuku weka kwenye jiko la kuchomea iwe ni la gesi au mkaa au jiko maalumu kwajili ya nyama choma. Pia kama huna unaweza tumia kikaango washa moto wa wastani kisha choma pole pole mpaka iive na iwe na rangi safi ya kahawia kama muonekano kwenye picha.

 

Nyama ikishaiva chukua mkate ukate kati kati na kisha paka mayonaise kwa juu, kisha paka tomato sauce kwa chini. kipande cha chini panga matango na nyanya pamoja na slice za kitunguu maji. Juu yake weka kifua cha kuku na funika na kipande cha pili kilichobakia.

WAPATIE FAMILA YAKO CHAKULA HIKI WAKATI WA MCHANA HASA SIKU ZA WEEKEND WAFURAHIE KWA KULA CHAKULA CHEPESI KWA KUSINDIKIZWA NA VIAZI VYA KUKAANGA NA SALAD.

1 comment:

Unknown said...

hii naisubiri kwa hamu