CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Thursday, October 28, 2010

JIFUNZE KUTENGENEZA CHATNEY YA NYANYA


NI RAHISI KUPIKA NA INAKAA MUDA MREFU KATIKA FRIJI BILA YA KUHARIBIKA

MAHITAJI

3 Nyanya kubwa zilizoiva
4 kitunguu maji katakata
3 pilipili kavu au ya unga
1 tangawizi imenye na uiponde ponde
3 kijiko kikubwa cha chakula tui la nzai (sio lazima)
1 fungu la majani ya gili gilani
1/2 kijiko kidogo cha cha mixed spice
10 gram chumvi
10 gram kitunguu swaumu
3 kijiko kikubwa cha chakula mafuta ya mahindi
1/2 1/2 kijiko kidogo cha cha mbegu za mustard
    1/2 kijiko kidogo cha chai dengu
    1/2 kijiko kidogo cha cha manajano (turmeric)
    3 majani mabichi ya binzali

    JINSI YA KUANDAA FATILIA PICHA CHINI



    1.weka katika sufuria au kikaanga mafuta ya mahindi kisha kaanga pamoja na kitunguu, kitunguu swaumu na tangawizi mpaka vilainike na kuweka harufu nzuri. Kishaongezea nyanya, chumvi, turmeric,pilipili,sunga wa mix spice, majani ya giligilani kisha kaanga kwa dakika 5 mpaka upate harufu nzuli na mchanganyiko wako ulainike na kua kahawia.
     

     
    2.Huu ni muonekano wa nyanya na vitunguu vikiendele akuiza ndani ya sufuria kisha ongezea tui la nazi.



    3.Kisha chukua unga wa manjano, majani ya binzali na dengu zilizochemshwa weka juu ya ule mchanganyiko wa nyanya kisha chemsha katika moto mdogo kwa dakika 5 kisha weka katika blenda na usage mpaka upate mchuzi mzito kabisa.




    Ni rahisi sana. Chatney hii inasaidia sana kuoneza ladha katika chakula chako na pia inaongeza sana hamu ya kula hasa kwa watu wasiopenda kula akishakula hii basi hatawea kula bila ya kua na chatney hii maana nitamua sana na inaoneza harufu nzuri na mvuto katika chakula.


    KAWAIDA UNAPOANDAA CHAKUA CHAKO SIO WALAJI WOTE WATAKUA NA HAMU YA KULA KWA KUONGEZEA CHATNEY HII MLAJI ATARUDISHA HAMUA YAKE NA ATAKULA CHAKULA CHAKUTOSHA.



    1 comment:

    Unknown said...

    Wow! inaelekea ni nzuri sana.
    kaka huweki ndimu hata kidogo?