CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Monday, February 22, 2010

JINSI YAKUTENGENEZA CHICKEN SANDWICH


Muonekano chicken sandwich baada ya kuikata



Mchanganyiko halisi wa chicken mayonaise ukiwa juu ya jani la salad



unaweza tumia mkate wa aina yeyote ile slice au huu mrefu




Muonekano halisi wa sandwich ya kuku baada ya kukatwa tarayi kwa kula. kama unapenda kula ikiwa ya moto weka katika sandwich toaster funika ipate rangi ya kahawia toa na kula ikiwa ya moto kwa chipi na tomato sauce na salad saafi kabisa.





 
CHICKEN MAYONISE SANDWICH

Mahitaji:

Jinsi ya kupika kuku ya sandwich:

1 kilo ya kifua cha kuku au miguu  ya kuku toa ngozi ili kukwepa mafuta.
1 tangawizi kubwa
3 mbegu za  pili pili manga
Chumvi kulingana na ladha unayotaka

Chemsha mchangayiko huo wote pamoja na kuku mpaka kuku iive vizuri na iwe laini kabisa kisha toa katika jiko na uache upoe.


Mahitaji kwajili ya sandwich:

1 loaf of wholemeal bread or French wholemeal loaf (sliced)

1 pili pili hoho iliyokatwa saizi ndogo ndogo

1 kitunguu kilichokatwa saizi ndogondogo

3 au 4  mayonaisi kijikokikubwa cha chakula
3 nyanya nyekundu kata mviringo nyembamba (sliced)

1 tango zuri kata mviringo nyembamba (sliced)

1 lettuce salad nzuri ya kijani

Jinsi ya kuandaa:

Chukua  kuku aliepoa nyofoa nyofoa nyama ya kuku weka mifupa pembeni kisha weka ile nyama katika bakuli changanya mayonaise, chumvi, kitunguu, pili pli hoho na pili pili manga ya unga changaya vizuri kabisa.

Kama mchanganyiko wako ni mkavu ongeza mayonaise na lemon juice kidogo kuongeza ladha zaidi.

Chukua mchanganyiko wako wa kuku weka juu ya jani la salad panga vizuri usijaze sana ili uweze kufunika na kipande kingine cha mkate kilichobaki kisha weka slice ya tango na ya nyanya juu ya mchanganyiko wako wa kuku na mayonise.

Chukua kipande kingine cha mkate kilichobaki na funika kwa juu unaweza kula tayari au kama unapenda kau kau unaweza weka mkate wako huo kwenye toaster mashine na kuukausha kwa muda mapaka ukapata rangi ya kahawia na kua na ladha tofauti na ukala sandwich ya moto.

5 comments:

Anonymous said...

hapa umeniokoa, hapo kwenye MAYONNAISE ipi inafaa maana kuna aina tofauti tofauti nyingine chachuu, light

RK

Anonymous said...

Tumia mayonaise yeyote nzito kila nchi wanatumia brand tofauti za mayonaise kwa Tanzania tumieni american gadern mayonaise ni nzito na nzuri sana

Ruky said...

Hata mimi umeniokoa, thanks

Suzie said...

Sasa sisi wa diet tutumie brown bread sawa je mayonise embu nisaidie huwaga nailaga sana pale nanihiyo hii wananimaliziaga hela zangu.

Suzie

Issa Kesu said...

Si vibaya kutumia mayonaise mbaya ni kutumia nyingi kupiata kiasi enjoy sandwich yako