CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Friday, October 29, 2010

JIFUNZE KUTENGENEZA SUPU KWA KUTUMIA MBOGA AINA YA CERELY


KAA TAYARI KWA RECIPE SAFI KABISA

MAHITAJI

1 Kitunguu maji kikubwa
 6 au 7 miti ya  celery, safisha na kata ndogo ndogo
3 viazi ulaya vya umbo la kati
1 lita ya maji
1 kijiko kidogo cha chai aromati
1 kijiko kikubwa cha chakula unga wa binzali (curry powder) 
10 gram chumvi na pili pili manga
 5 gram kitunguu swaumu kilicho sagwa

JINSI YA KUTENGENEZA FATILIA PICHA NA MAELEZO HAPO CHINI

    weka katika kikaango kijiko kimoja cha siagi, kisha kaanga kitunguu maji na unga wa binzali (curry powder).


    Kisha ongeza celery na viazi ulaya kaanga kwa dakika 5 pia weka aromati na chumvi.


    Kisha ongezea maji. halafu funika sufuria yako kwa dakika 10 mpaka 15.



    Chukua mchanganyiko wako huu na weka katika blenda saga mpaka upate uji mzito kabisa



    Kisha mimina tena katika sufuria, mwisho kabisa weka pili pili manga na ukoroge.





    Hakikisha unampatia mlaji ikiwa yamoto kabisa toka jikoni ili kupasha tumbo na kuamsha hamu ya kula mlo kamili kisha pamba na majani ya celery.




    2 comments:

    Mama Jeremiah said...

    Asante kwa kutufundisha kupika kwa kutumia celery. Nitajaribu maana hili jani au miti nikiiona nashindwa hata kujua ni jinsi gani ya kuipika.
    Nitajaribu halafu nitakuambia kama nimepatia.
    Salaam kwa wote

    Mama Jeremiah

    Anonymous said...

    kaka hiyo celery kwa kiswahili inaitwaje