CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Friday, October 29, 2010

JIFUNZE KUTENGENEZA SUPU YA MABOGA NA KARANGA (peanut butter)


 RECIPE SAFI KABISA NA RAHISI KUTENGENEZA

Kwa kuchemsha maboga pembeni kisha unayasaga kwenye blenda,Pia bila ya kusahau viazi vitamu na peanut butter. Unapata mchanganyiko wa supu safi sana na tofauti kuliko supu nyingi ulizozizoea. Pia supu hii inavirutubish vingi sana katika mwili. Jenga tabia ya kunywa supu hii itakusaidia sana kujenga mwili na kukupa joto la kutosha hasa majira ya baridi (winters).

MAHITAJI

240 gram maboga yaliyomenywa yakachemshwa  pamoja na kitunguu maji kimoja na kusagwa katika blenda
1 kiazi ulaya kikubwa
60 gram Karanga ya kusaga (peanut butter) laini kabisa
1 kijiko kikubwa cha chakula siagi
480 gram za maji safi na salama
5 gram chumvi
5 gram pili pili manga
Majani ya chives au yeyote yale kwajili ya kupambia


JINSI YA KUANDAA FATILIA MAFUNZO NA PICHA HAPO CHINI


 
Safisha na katakata viazi vitamu kisha visteam katika chombo maalum kama huna basi chemsha tu kawaida katika sufuria.


Vikisha lainika safi toa katika combo hicho. Mi binafsi huwa napendelea sana ku steam badala ya kuchemsha.



Kisha weka katika blenda na uvisage pia unaweza menya ngozi mimi huwa napendelea kuiacha ngozi ili kupata harufu na ladha halisi ya kiazi. 



Katika kikaango, yeyusha siagi na ukaange ule mchanganyiko uliosagwa wa maboga, mchanganyiko wa viazi vitamu pamoja na peanut butter.


Kisha ongezea maji kufanya mchanganyiko wako uwe laini na uweke chumvi na pili pili manga kupata ladha safi. Koroga mpaka iwe laini na imechanganyika vizuri hakikisha unachemsha kwa dakika 10 tu inakua tayari kwa mlaji kumpatia.


 Juu kabisa baada ya kumimina katika bakuli pamba na chives na cream.




MUONEKANO HUU NI SAFI SANA LAZIMA MNYWAJI AVUTIWE HASA NA UKINYWA SUPU HII MARA MOJA TU BASI UTATAKA KUNYWA KILA SIKU. KWA WALE MLIO NA WATOTO MAPATIE SUPU HII MARA KWA MARA MTOTO ATARUDISHA AFYA HARAKA SANA. PIA MLIO KATIKA NCHI ZA BARIDI PATA SUPU HII KABLA YA CHAKULA ILIKUONGEZA JOTO MWILINI.






1 comment:

Anonymous said...

hayo no maboga au viazi