CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Thursday, February 25, 2010

BEEF SEEKH KABAB



HISTORIA YA SEEKH KABAB:

Seekh kababs zina ladha safi sana kutokana na mchanganyiko wa viungo husika. Kawaida zinachomwa kwa makaa ya moto uliowaka vizuri na kua mekundu kabisa na ndio maana huwa zina harufu safi ya moshi wa kawaida. Kuchoma katika makaa kunasababisha kuleta ladha halisi.

Kebab hii hupendelewa sana na huliwa sana na watu wa Peshawar na kaskazini ya Pakistan na India. Wanapendelea kula na Mkate wa  nani, mint sauce na salad. Kawaida ya watu hawa wanapenda sana BBQ na kawaida ya BBQ lazima uchome katika eneo la wazi katika matamasha yao na sherehe zao na ndugu na jamaa hujumuika maeneo ya wazi ninaimani nawe mdau utafurahia sana chakula hiki.

MAHITAJI:

1kilo nyama ya kusaga ya ng'ombe

2 vitunguu
4 pilipili ndefu za kijani

1 corienda kavu kijiko kidogo cha chai

1ground garam masala kijiko kidogo cha chai

1 yai

Maji

½ Chumvi kijiko kidogo cha chai


2 pili pili nyekundu ya unga kijiko kidogo cha chai
1 jira (cumin seeds) kijiko kidogo cha chai


120gram tangawizi mbichi 

150gram Mafuta ya kupikia

JINSI YA KUTENGENEZA

Weka mchanganyiko wako wa kitunguu , pili pili ya kijani, coriender kavu, jira na tangawizi katika blender saga upae mchangyiko safi uwe mzito kama tope.

Chukua mchanganyiko huo mzito wa mboga weka katika nyama ya kusaga ongeza na yai changanya vizuri kabisa.

Kisha changanya chumvi, unga wa pili pili nyekundu na garam masala katika mchanganyiko wa nyama.

KIsha chukua vijiti virefu vya mwanzi au cha chuma maalumu kwajili ya mshikaki au BBQ kisha weka nyama yako kuzunguka huo mshikaki mapaka ishikamane vizuri na kutengeneza umbo zuri weka katia jiko la mkaa la kuokea au kama hutumii mkaa weka katika oven.

kwa anetumia oven ili vijiti vya mwanzi vya mshikaki (bamboo skwers) tumia aluminium foil kuzungushia havitaungua kabisa. Kumbuka kugeuza mara kwa mara mshikaki wako ili uive pande zote.

Msikaki wako ukishakua mwekundu saafi pande zote mbili nyunyizia mafuta pande zote weka kidogo katika moto tena kwa dakika 3 tu kisha toa utakua umengaa na muonekano safi kabisa.

KUMBUKA

Tumia mkono wako kuweka nyama katika mti wa mshikaki

Loanisha mikono yako ili nyama ising'ang'anie mikononi kama itatokea hali hiyo

Kama utaona haishikani vizuri na ni kavu unaweza ongeza yai

UNAWEZA LISHA FAMILIA YA WATU 12 KWA MCHANGANYIKO HUU. WAWEZA KULA NA UGALI, WALI AU CHIPS NA SALAD.

3 comments:

Born 2 Suffer said...

Safi sana ndugu yani denda zinanitoka hapa.

Mama Jeremiah said...

Asante sana Issa, hizi recipes si mchezo. Watu tushindwe tuu wenyewe

Mama Jeremiah

Anonymous said...

corienda kavu ndo nini