CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Wednesday, June 30, 2010

CHOCOLATE SALAMI NI SAFI SANA

CHOCOLATE HUPENDWA SANA NA WATOTO PAMOJA NA WATU WAZIMA WASWIS WANAKULA SANA ILI KUJIBURUDISHA, KUCHANGAMSHA AKILI NA KUONGEZA NGUVU MWILINI

700 gram bittersweet chocolate au ( Chocolate bloc)
4 kijiko cha chakula siagi isiyo na chumvi
2 kijiko cha chakula cocoa powder
60 gram maji ya moto
150 gram korosho zilizo okwa katika oven
150 gram karanga zilizo okwa katika oven
1 box la biskuti ziponde ponde ziwe vipange kama ukubwa wa korosho
4 yai kubwa tumia ute wa njano tu
240 gram sukari ya unga
1kijiko cha chakula champagne au apple juice
1 chungwa kwaruza upate chenga chenga za maganda ya juu


JINSI YA KUANDAA

Fuata maelekezo na picha chini



Katika picha huo ni muonekano wa vitu vyote unavyotakiw akua navyo kabla ya kaunza kutengeneza chocolate salami yako.

Chukua maji moto changanya na cocoa powder pamoja na sukari

kisha chukua ute wa njao wa mayai piga kwa mchapo au mashine kama picha inavyoonyesha chini


Huu ni muonekano wa ute wa njano wa mayai weka na chenga chenga za chungwa ulizokwaruza pamoja na kijiko cha champagne au apple juice


Kisha chukua chocolate yako nyeusi yeyusha katika surufia kwa moto mdogo sana pamoja an siagi mpaka iyeyuke kabisa


Kisha changanya mchanganyiko wako wa siagi na chocolate pamoja na mchanganyiko wa kokoa kisha chukua na mchanganyiko wa mayai changanya pole pole mpaka ichanganyike vizuri


Mwisho chukua mchanganyiko wa karanga, korosho na biscuit chnagnya pia katika mchanganyiko wako wenye chocolate tayari



Kisha unaweza tumia njia mbili, yakwanza mwaga sukari ya unga juu ya meza kisha mwagia mchanganyiko wako wenye karanga na chocolate juu yake na viringisha juu ya hiyo sukari juu ya meza upate mviringo mzuri na kisha weka katika freeza ili ugande kwa masaa 2 baada ya hapo inakua tayari kuliwa na unaweza kukata katiaka mtindo tofauti.

Njia ya pili chukua aluminium foil kisha mwagia kuu yake mchanganyiko wako na kisha vingirisha kwa umbo la duara kwa upana wowote unaopenda wewe kisha weka kwenye freeza kwa masaa mawili itaganda safi nakua tayari kwa kuliwa.



Baada ya kutoa katika freeza unaweza kukata kwa umbo lolote unalopenda wewe ingawa inapendeza zaidi ukikata kwa umbo la duara kama inavyoonekana kwenye picha.

Wapatie familia yako kwa chai ya saa 4 au chai ya saa 10 jioni kwa family na wageni pia unaweza mfungashia mtoto akale shule.


1 comment:

Flora said...

Twaisubiria