CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Tuesday, June 1, 2010

DAGAA A KIGOMA YAM YAM!!!!!!!!!!!

DAGAA NI WAZURI NA WATAMU SANA ENDAPO UTAWAPIKA VIZURI KWA AFYA YA MLAJI
MAHITAJI
1/2 kilo ya dagaa wa Kigoma au wa Mwanza
2 nyanya kubwa
50 gram kitunguu swaumu
1 pili pili hoho kubwa
1 bilinganya saizi ya kati
35 gram mafuta ya kupikia
JINSI YA KUANDAA FATILIA MAFUNZO CHINI KATIKA PICHA

Muonekano wa mahitaji yako

weka mafuta katika kikaango yakipata moto kaanga vitunguu maji na kitunguu swaumu


kisha weka nyanya fresh iliyokwisha katwa katwa

kisha funika ichemke taratibu ili nyanya iive

baada ya dakika 5 funua nyanya itakua imelainika

weka mchanganyiko wa pili pili hoho na bilinganya pamoja na dagaa walioosha safi kabisa kwa maji

badaa ya hapo koroga vizuri mchanganyiko wote uchanganyike safi kabisa

kisha weka kitunguu swaumu hicho ni kifaa maalumu cha kuponde kitunguu kinauzwa madukani

Kisha weka binzali ya kopo iliyochanganywa na tui la nazi kama huna basi kuna nazi weka tui kuongeza ladha sio lazima

Nazi kawaida huwa ina mafuta lakini mafuta haya ni salama kwa mlaji ikiwa huli mara kwa mara pia yanasaidia kukaanga mchuzi wako uwe safi na mboga zilainike vizuri



HAYA NDIO MAPISHI YA DAGAA WA KIGOMAKUCHANGANYA PILI PILI HOHO NA BILINGANYA WAPIKIE FAMILIA YAKO WAFURAHIE CHAKLA HIKI UNAWEZA KULA NA MAHARAGE NA WALI AU UNAWEZA KULA NA UGALI KAMA WENGI TULIVYOZOWE NYUMBANI NA INAPENDEZA SANA SANA


11 comments:

Anonymous said...

Hapo sasa umetufikisha sisi waswahili.tupe vitu basi kaka.

Disminder orig baby said...

urakoze chane. Unaturudisha UJIJI.
FUNGA KOLOMO. Asante sana.

Anonymous said...

Yaani kaka Mungu akubariki zaidi, cant wait for the recipe yake na hiyo ya sambusa.

Anonymous said...

can't wait weka vitu kaka !!!!

Anonymous said...

tuna kusubiri kwa hamu kaka kwani recipe hii inatugusa sana sisi tuishio uswahilini. tupe vitu.

Yasinta Ngonyani said...

Yaani hapa karoho kamefanya pa paaa

Anonymous said...

Nimejaribu leo kupika kwa kweli ni watamu mno na familia yangu wamefurahia mno chakula hiki. Mungu akujaalie sana kaka kwa kutupa mambo mazuri.

mama Jeremiah said...

ahh yaani nimeangalia huku mate yanadondoka!!
Asante sana kaka

Anonymous said...

mmh mi hapa yani natamani ka ugali tu dah tena mida ya lunch. thanks bro mume wangu anavopenda dagaa.........

mwajuma said...

HEHEE KAKA HAPO UCPIME, HATA SISI WATANGA UMENIKUNA PALE ULIPOCHANGANYA NA BILINGANYA HAPO UMELIANZISHA BONGE LA UCHOKOZI. HONGERA SANA MUNGU AKUZIDISHIE INSHAALAH. NATUMAI TOLEO LAKO LA MAPISHI LINAZIDI KUTUTO SHAVU HASA WALE MABINGWA WA MENYU. SHUKRANI BRO.

Anonymous said...

Mm ni kapera ...lol nimejaribu hii recipe imetoka vizuri....Shukrani...kila la kheri