CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Saturday, June 12, 2010

JINSI YA KUPIKA BIRIYANI KWA KUTUMIA WALI WA BASMATI NA NYAMA YA KUKU, MBUZI AU NG'OMBE

MAHITAJI

1 kilo mchele wa basmati mrefu

1 kilo nyama iwe ya kuku au ng'ombe au mbuzi kata katika umbo dogo la kutosha kula kisha ichemshe na tangawizi na kitunguu swaumu, unga wa binzari (turmeric powder) pili pili manga na chumvi ili kuweka ladha nzuri. Ikisha iva itoe iweke pembeni na mchuzi wake uweke pembeni utautumia baadae.
1 kilo ya vitunguu kata slice ( mviringo)
1 kilo nyanya nyekudu zilizoiva, osha vizuri kisha katakata saizi ndogo ndogo sana
240 gram ya Mafuta ya kupikia
240 gram ya samli au mafuta yeyote ya kupikia
2 maggi chicken soup cubes
3 kijiko kidogo cha chai unga wa pilipili mwekundu
1/2 kijiko kidogo cha chai unga wa binzari (turmeric powder)
3 kijiko kidogo cha chai unga wa girigilani (coriander powder)
2 kijiko kikubwa cha chakula mchanganyiko wa tangawizi na kitunguu swaumu vilivyosagwa (ginger-garlic paste )
50 gram korosho iliyo kaangwa usizisage zibaki nzima
50 gram majani ya girigilani (fresh coriander leaves, washed and chopped)
8-12 mbegu za nzima ya hiriki (green cardamoms)
4 bay leaves ( sifahamu kiswahili chake)
15 mbegu nzima ya pili pili manga (whole black peppercorns)
30 gram majani mabichi ya minti ( mint leaves )
salt kulingana na ladha yako binafsi
Jinsi ya kuanda

Weka mafuta katika sufuria yako iliyo juu ya moto tayari, kisha kaanga nyama yako iliyokwisha chemshwa mpaka iwe na rangi ya kahawia (golden brown)

Kisha itoe nyama hiyo na ichuje mafuta ili mafuta yanayobaki weka kitunguu na endelea kukaanga kwa dakika 7-10 kisha weka unga wa binzali, unga wa pili pili mwekundu, unga wa girigilani, bay leaves, mbegu za hiriki na nusu ya mbegu za pili pili manga.
Changanya vizuri mpaka utapata mchanganyiko mzuri mkavu miminia humo maji uliyotunza baada ya kuchemshia ile nyama yako na kuiweka pembeni ipoe. kisha weka nyanya fresh ndani ya sufuria yako pika mpaka maji yakauke na mafuta yaanze kuoneka kwa juu ndani ya sufuria.
Kisha weka nyama yako ndani ya sufuria pole pole halafu punguza moto acha ijipike kwa muda mpaka mchuzi wako na nyama vikamate ladha pia usisahau kuweka chumvi kulingana na ladha unayopenda.
Chukua sufuria nyingine weka mafuta ya samli na vitunguu ilivyoslice kisha kaanga na majani ya girigilani, majani ya mint na korosho funika kwa dakika 10 picha inaonyesha hapo chini, kisha weka wali wako mkavu uliokwisha oshwa vizuri na uchanganye vizuri ongeza vikombe 5 vya maji na chumvi kidogo mchele ukishaanza kuchemka funika sufuria lako na punguza moto maji yakisha kauka kiasi weka mchanganyiko wa ile nyama yako nusu tu juu ya wali wa basmati acha wali uive kabisa kisha itakua tayari kula na pakua chakula chako kikiwa cha moto,


Wali wa pishori ( Basmati rice) uliokwisha iva


muonekano wa majani ya girigirani wakati wa kukaangwa


 Wali wa pishori ( Basmati rice) uliokwisha iva ukakaangwa na vitungu na korosho


Nyama ya kuku iliokaangwa vizuri na viungo na nyanya ukapata mchanganyiko mzuri mzito




Muonekano halisi wa biriyani yako baada ya kuiva ikiwa imechanganyikana na nyama pia kumbuka kunamchuzi mzito na nyma ilibaki pembeni mlaji ataweza kujongezea kiasi apendacho.
Furahia chakula hiki pamoja na familia yako.

RECIPE HII NIMEIRUDIA KUTOKANA NA MAOMBI YA WADAU WENGI LENGO NI KILA MMOJA AFURAHIE NA AFAIDIKE

5 comments:

Anonymous said...

welcome back chef...hiyo biriani kama inwezekana iweke leo...please

Anonymous said...

kaka,haukaribishagi watu wa kuja kuonja,i wish nije kuonja biriani..yammii
Rose

Anonymous said...

Asante sana kwa kutugawia ujuzi kaka. Sio binadamu wote wanaoweza kuwagawia wenzao ujuzi. Mungu akujalie uendelee na moyo huo mwema,na akujalie mafanikio mema , maisha mema, familia njema na umri mkubwa kama Mandela na kikubwa zaidi Afya njema.

Anonymous said...

shukrani sana kaka issa, niliamua kukaa na karatasi jikoni nikafuata step by step jamani biryani ilikua tamu sana, familia yangu inasubiri kwa hamu nipike tena biryani! keep it up kaka, be blessed!

Anonymous said...

Hello kaka...mimi bado sijajaribu kupika...ila naomba jaribu kupiga hata picha ya `BAY LEAVES... hata niyaone kwa picha labda nitajua ni majani gani...maana hapa umesema hujui kiswahili chake.

pamoja na MAJANI MABICHI YA MINTI....sielewi ni majani ngani.

nipange siku ya kupika pishi hili.

MDAU
SWEDEN.