CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Monday, June 7, 2010

WAPENZI WA PASTA NA NYAMA

MAHITAJI

1 kilo Nyama yeyote ile iwe kuku, mbuzi au ngombe
300 gram nyanya ya kopo au fresh ila katakata iwe ndogo ndogo kwa mchuzi
50 gram kitunguu swaumu
100 gram karoti
100 gram kitunguu maji
100 gram pili pili hoho
1 paketi la macaroni
300 gram viazi ulaya

JINSI YA KUANDAA FATILIA CHINI KATIKA PICHA


Huu ni muonekano wa nyama ya mbuzi naipenda sana



Weka kitunguu kwenye kwenye mafuta ya moto kisha kaanza mpaka kiwe na rangi ya kahawia


Kisha weka kiuongoa aina ya paprika kuongeza ladha kama hauna usiweke


kisha weka nyama kaanga pai mpka iive kumbuka kuweka maji kikombe kimoja kidogo kusaidia isiungue


huu ndio muonekano wa macaroni


Baada ya nyama kuiva weka viazi ulaya vibichi kaanga pia mpaka viive


kisha weka unga wa binzali kuongeza ladha


Kisha weka kitunguu swaumu kuongeza ladha  na harufu safi pia na kukata harufu ya nyama ya mbuzi


Kisha weka karoti na pili pili hoho pamoja na nyama ya kopo


Weka makaroni kwenye maji moto yaliyokiwsha chemka sana chemsha kwa dakika 7 tu


weka chumvi kwenye makaroni yaliyopo jikoni wakati yakiendelea kuchemka 


Baada ya makaroni kuchemka toa weka katika bakuli kisha yapoze ma maji baridi sana ili yasipondeke


Kisha chuja vizuri makaroni yako wasiwe na maji na chukua nyama yako ya mcuzi iliyokweisha iva changanya na makaroni yako yaliyoiva pia koroga ya changanyike vizuri


Kisha weka makaroni yako kwenye bakuli la kioo au la chuma ili uyaoke kwemye oven mchuzi ule ushikane safi na macaroni yako kua na muonekano na ladha safi


Kisha weka katika oven na oka kwa dakika 10 kumbuka kuweka aluminium foil kwa juu ili yasiungue

BAADA YA DAKIKA 10 MACARONI YAKO YATAKUA SAFI NA TAYARI KWA KULIWA WAPAKULIE FAMILIA YAKO YAKIWA YA MOTO KUMBUKA KUWEKA USAWA MACARONI , KIAZI NA NYAMA USIWEKE MAKARONI TUPU HAHAHAAAAAAAA





8 comments:

Anonymous said...

Uwiiiiiiiiii, watu people, yaani umenigusa kama niko ITALY VILE. CANT WAIT

Anonymous said...

im waiting in vain for the macaron recipe chef plz post!

Anonymous said...

jamani hata mimi nangoja sana recipe ya macaroni halafu naomba utupostie recipe ya biriani plzzzz chef

Anonymous said...

chef umepotelea wapi tena?

Anonymous said...

nasubiri kwa hamu kaka hiyo recipe ya macaron. lete vitu.

Anonymous said...

mambo chef,naoma unijuze kuhusu hiyo paprika,naitumia kwa nyama zote au?ni nini na inatumikaje?naomba jibu..halaf napata wapi hivo viungo unavotumia?
mungu akubariki uendelee kutupa mambo mazuri kama haya

ruky said...

Asante sana kaka. mimi mpenzi wa makaroni umenifikisha

Anonymous said...

kaka unatisha yaani mi binafsi nakukubali sana,nadhani mkeo atakuwa anafaidi sana.endelea kutupa maujuzi kaka na sisi tufanye maajabu kama yako.ahsante mrs.D