CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Monday, March 1, 2010

FILLET YA SAMAKI, VIAZI VYA KUCHEMSHA, VEGETABLE RATATOULA

JINSI YA KUANDAA VEGETABLE RATATOULA




Chukua mchanganyiko wa mboga pili pili hoho, bilinganya, Nyanya, Vitunguu na Nyanya kata mkato wa aina moja




weka mafuta mengi kwanye sufuria ili yasaidiea kukaanga mboga zako kwa muda mfupi, yakishapata moto wa kutosha mpaka yakaanza kutoa moshi weka bilinganya ndani ya sufuria



kisha koroga zisishike chini zikaungua.




Kisha weka vitunguu ndani ya sufuria na endelea kukoroga kumbuka jiko lako liwe na moto mkali ili mboga zipikike kwa muda mrefu bila kurojeka



Kisha weka vitunguu swaumu vilivyosagwa, tangawizi iliyosagwa kidogo, binzali ya unga kiasi, mdalasini ya unga kiasi, kungumanga ya unga kiasi kaanga kwa dakika 3 kisah weka nyanya ya kopo koroga isiungue mpaka nyanya ishikane na mboga kama mafuta yamekauka ongeza kidogo chakula hiki kinapikwa na mafuta mengi kiasi.




Kisha weka pili pili hoho ndani ya sufuri pika kwa dakika 2 huu ni muonekano baada ya  kukoroga ikachanganyika vizuri

 

Baada ya hapo weka nyanya ndani ya sufuria koroga pole pole zasipondeke ila zichanganyike na mboga zingine ili kulinda umbo halisi la nyanya



Huu ndio muonekano halisi baada ya kuchanganya nyanya kisha weka chuvi kulingana na ladha yako binafsi.


JINSI YA KUANDAA NYAMA YA SAMAKI



weka maji katika kikaango au sufuria kisha kata malimao mkato wowote ule, kata kitunguu mkato wowote ule pia kata karoti makato wowoete ule weka ndani ya chombo chako cha kupikia



Kisha weka nyama yako ya samaki ndani ya chombo chako cha kupikia katika maji yaliyochemka vizuri ipike kwa dakika 5 tu kisha itoe itakua imeiva safi kabisa tayari kwa kuliwa


NAMNA YAKUPANGA KATIKA SAHANI IVUTIE MLAJI

 


Weka vugeteble ratatoula yako mwisho wa sahani kati kati kisha weka viazi vya kuchemsha viwili kama inavyoonekana katika picha

Kisha chukua nyama yako ya samaki weka juu ya mboga mboga zakosaafi kabisa


Mwisho weka kipande cha limao kama pambo pamoja na jani la lettuce maana hii ni nyama nyeuoe lazima ipate limao kiasi kwa kuongeza ladha.


FURAHIA CHAKULA CHAKO NA FAMILIA YAKO



3 comments:

Anonymous said...

S.a maashallah mwenyewe mjuzi kweli yaani unapangalia vzuri hadi raha shukran kwa kutufunza.tunakutakia afya njema. ybty

Anonymous said...

Jani la letus?kiswahil.alafu hayo maji. Uliochemshia samaki yenye carot. ....umetoa samaki ukaja kuipambie jehizo carot ndo basi tena huzitumii

Issa Kesu said...

Nashukuru sana kwa swali zuri hayo maji ya karoti hayatumiki tena nikwajili ya kuchemshia samaki tu.

Chef Issa