CULINARY CHAMBER

LIBENEKE LA CHAKULA BORA WATU LAZIMA WALE MSOSI MTAMU NA SALAMA KUJIFUNZA NI BURE

Sunday, March 21, 2010

WAPENZI WA SUPU FAIDIKENI SASA KAZI IMEANZA

JINSI YA KUTENGENEZA SUPU YA SPINACHI

MAHATIJI

2 kilo Spinach
1/2 kilo Karoti
300 gram Kitunguu
500gram Kiazi ulaya
250 gram siagi
200 gram fresh cream kwa kupambia
250 gram maziwa ya maji/ fresh cream


FATA MAELEZO JINSI YA KUTENGENEZA SUPU YA SPINACH KAMA PICHA NA MAELEZO YANAVYOELEKEZA.




Kata mboga zako kama inavyoonekana katika picha kumbuka kuziosha vizuri sana na kausha maji



Kisha weka siagi katika sufuria acha iyeyuke vizuri



Kisha weka vitunguu ndani ya sufuria kaanga kidogo vilainike



Kisha weka mchanganyiko wa mboga zote zilizobaki changanya vizuri zichznganyike



Kisha weka maji baridi katika sufuria yenye mchanganyiko wa mboga na uiache ichemke



huu ni muonekano wa kuiva kwa mboga na maji yamebadilika rangi tayari kwa kusagwa na kua supu tamu kabisa



Chukua mchanganyiko wako safi kabisa wa mboga na maji kisha weka katika blender na saga mpaka upate rojo safi kabisa na laini




Baada ya kublend mchanganyiko wote huo rudisha supu yako katika jiko na ichemshe tena kwa uongeza ladha weka frsh cream au maziwa ya maji acha ichemke vizuri kisha weka chumvi kulingana na ladha yako ila supu haipendezi kua na chumvi nyingi kua makini



Kisha chota supu yako safi na mimina kwenye chombo maalumu cha kuhudumia mnywaji wa supu yako



Huu ndio muonekano wa supu yako katika bakuli maalumu la kunywea



Hii ni chupa maalumu kwajili ya kupambia supu yako, unachotakiwa kufanya ni kuweka fresh cream ndani yake.



Kisha tumia chombo hiki kumimina katika bakuli maalumu na uzungushe miduara eneo lote la bakuli kama picha inavyelekeza.




Pole pole zungusha mduara mapaka mwisho





Kisha tumia toothpik kuchorea michirizi mizuri amabyo itafanya muonekano tofauti katika supu yako na kumfanya mnywaji ashangae kabla ya kunywa supu hii anzia katikati kata mpaka mwisho wa bakuli.



Hivyo hivyo kata kuanzia kati kati mpaka mwisho huu ndio muonekano wako halisi wa supu kumbuka kufanya zoezi hili kwa haraka sana na mpatie mnywaji wa supu ikiwa ya moto.




2 comments:

Anonymous said...

we kiboko, i salute you

Anonymous said...

Asante sana Chef kwa maandalizi safi ya supu, imenivutia cos mi ni Vegetarian... swali je naweza andaa supu ikiwa baridi? yani baada ya kublend nikaweka kidogo kwenye friji!